Methali 10:1-32

  • Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie (1)

  • Mikono yenye bidii huleta utajiri (4)

  • Kusema maneno mengi husababisha makosa (19)

  • Baraka ya Yehova hutajirisha (22)

  • Kumwogopa Yehova hurefusha maisha (27)

10  Methali za Sulemani.+ Mwana mwenye hekima humfanya baba yake ashangilie,+Lakini mwana mpumbavu ni huzuni kwa mama yake.   Hazina zilizopatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,Lakini uadilifu ndio unaookoa kutoka katika kifo.+   Yehova hatamwacha mwadilifu akae njaa,+Lakini atawanyima waovu wanachotamani.   Mikono milegevu italeta umaskini,+Lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.+   Mwana anayetenda kwa ufahamu hukusanya mazao wakati wa kiangazi,Lakini mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+   Baraka ziko juu ya kichwa cha mwadilifu,+Lakini kinywa cha mwovu hufunika ukatili.   Kumbukumbu* ya mwadilifu itabarikiwa,+Lakini jina la mwovu litaoza.+   Mwenye hekima moyoni atakubali mafundisho,*+Lakini mtu anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+   Anayetembea kwa utimilifu atatembea kwa usalama,+Lakini anayepotosha njia zake atajulikana.+ 10  Anayekonyeza jicho lake kwa hila husababisha huzuni,+Na yule anayezungumza maneno ya upumbavu atakanyagiwa chini.+ 11  Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uzima,+Lakini kinywa cha mwovu hufunika ukatili.+ 12  Chuki ndiyo inayochochea ugomvi,Lakini upendo hufunika makosa yote.+ 13  Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye utambuzi,+Lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu asiye na busara.*+ 14  Watu wenye hekima huhifadhi ujuzi kama hazina,+Lakini kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.+ 15  Mali ya* tajiri ni jiji lake lenye ngome. Ufukara wa maskini ndio unaowaangamiza.+ 16  Kazi ya mwadilifu huongoza kwenye uzima;Lakini mazao ya mwovu huongoza kwenye dhambi.+ 17  Anayetii nidhamu ni kijia kinachoelekea kwenye uzima,*Lakini anayepuuza karipio huwapotosha wengine. 18  Anayeficha chuki yake husema uwongo,+Na yule anayeeneza habari zinazodhuru* ni mpumbavu. 19  Maneno yanapokuwa mengi, makosa hayawezi kuepukwa,+Lakini yeyote anayedhibiti midomo yake anatenda kwa busara.+ 20  Ulimi wa mwadilifu ni kama fedha bora kabisa,+Lakini moyo wa mwovu una thamani ndogo. 21  Midomo ya mwadilifu huwalisha* wengi,+Lakini wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa ufahamu.+ 22  Baraka ya Yehova ndiyo inayomtajirisha mtu,+Naye haichanganyi na maumivu.* 23  Kutenda mambo ya aibu ni kama mchezo kwa mpumbavu,Lakini hekima ni ya mtu mwenye utambuzi.+ 24  Anachoogopa mwovu kitamjia;Lakini tamaa ya mwadilifu itatoshelezwa.+ 25  Dhoruba ikipita, mwovu hatakuwepo tena,+Lakini mwadilifu ni msingi milele.+ 26  Kama siki kwenye meno na moshi machoni,Ndivyo alivyo mtu mvivu kwa yule anayemtuma.* 27  Kumwogopa Yehova hurefusha maisha,+Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+ 28  Matarajio ya* waadilifu huleta shangwe,+Lakini tumaini la waovu litatokomea.+ 29  Njia ya Yehova ni ngome kwa mtu asiye na lawama,+Lakini ni maangamizi kwa watenda maovu.+ 30  Mwadilifu hataangushwa kamwe,+Lakini waovu hawataendelea kukaa duniani.+ 31  Kinywa cha mwadilifu huzaa* hekima,Lakini ulimi uliopotoka utaangamizwa. 32  Midomo ya mwadilifu inajua mambo yanayopendeza,Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.

Maelezo ya Chini

Au “Sifa.”
Tnn., “amri.”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Au “Kitu chenye thamani cha.”
Au labda, “yuko kwenye kijia kinachoelekea kwenye uzima.”
Au “uvumi unaodhuru.”
Au “huwaongoza.”
Au “huzuni; dhiki.”
Au “mwajiri wake.”
Au “Tumaini la.”
Au “huzaa tunda la.”