Mwanzo 2:1-25

  • Mungu apumzika siku ya saba (1-3)

  • Yehova Mungu, Muumbaji wa mbingu na dunia (4)

  • Mwanamume na mwanamke katika bustani ya Edeni (5-25)

    • Mtu aumbwa kutokana na mavumbi (7)

    • Mti uliokatazwa wa ujuzi (15-17)

    • Kuumbwa kwa mwanamke (18-25)

2  Basi mbingu na dunia na kila kitu kilichomo vikakamilika.*+  Na kufikia siku ya saba, Mungu alikuwa amemaliza kazi aliyokuwa akifanya, naye akaanza kupumzika siku ya saba kutoka katika kazi yake yote aliyokuwa amefanya.+  Na Mungu akaibariki siku ya saba na kuitangaza kuwa takatifu, kwa kuwa katika siku hiyo Mungu amekuwa akipumzika kutokana na kazi yake yote ya kuumba, vyote alivyokusudia kuumba.  Hii ndiyo historia ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa, siku ambayo Yehova* Mungu aliumba dunia na mbingu.+  Dunia bado haikuwa na kichaka chochote na hakuna mmea wowote uliokuwa umeanza kuchipuka, kwa sababu Yehova Mungu hakuwa amefanya mvua inyeshe duniani na hapakuwa na mtu wa kuilima ardhi.  Lakini ukungu ulikuwa ukipanda kutoka duniani, nao uliinywesha ardhi yote.  Kisha Yehova Mungu akamuumba mtu kutokana na mavumbi+ ya ardhi na kupuliza katika mianzi ya pua yake pumzi ya uhai,+ na mtu huyo akawa mtu aliye hai.*+  Zaidi ya hilo, Yehova Mungu akapanda bustani kule Edeni,+ kuelekea mashariki; na humo akamweka huyo mtu aliyemuumba.+  Kwa hiyo Yehova Mungu akachipusha ardhini kila mti wenye kupendeza macho na unaofaa kwa chakula na pia mti wa uzima+ katikati ya bustani na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.+ 10  Sasa kulikuwa na mto uliotiririka kutoka Edeni ili kuinywesha bustani, na kutoka huko uligawanyika na kuwa mito minne.* 11  Jina la mto wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu. 12  Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri. Pia kuna utomvu wa mbedola na madini ya shohamu. 13  Jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. 14  Jina la mto wa tatu ni Hidekeli;*+ ndio unaoelekea upande wa mashariki wa Ashuru.+ Na mto wa nne ni Efrati.+ 15  Yehova Mungu akamchukua huyo mtu na kumweka katika bustani ya Edeni ili ailime na kuitunza.+ 16  Pia, Yehova Mungu akampa huyo mtu amri hii: “Unaweza kula matunda ya kila mti katika bustani mpaka ushibe.+ 17  Lakini kuhusu mti wa ujuzi wa mema na mabaya, usile matunda yake, kwa maana siku utakapokula matunda yake hakika utakufa.”+ 18  Kisha Yehova Mungu akasema: “Si vema mwanamume huyu aendelee kuwa peke yake. Nitamuumbia msaidizi, awe kikamilisho chake.”+ 19  Sasa Yehova Mungu aliumba kutoka mavumbini kila mnyama wa mwituni na kila kiumbe anayeruka angani, naye akaanza kuwaleta kwa mtu huyo ili aamue jina atakalompa kila kiumbe; na jina lolote ambalo mtu huyo alimpa kila kiumbe aliye hai, likawa jina lake.+ 20  Basi mtu huyo akawapa majina wanyama wote wa kufugwa na viumbe wote wanaoruka angani na kila mnyama wa mwituni, lakini mwanamume huyo hakuwa na msaidizi ambaye angekuwa kikamilisho chake. 21  Kwa hiyo Yehova Mungu akamletea mwanamume huyo usingizi mzito, na alipokuwa akilala, akachukua ubavu wake mmoja na kufunika nyama mahali hapo. 22  Na Yehova Mungu akaufanya ubavu aliochukua kutoka kwa mwanamume uwe mwanamke, naye akamleta kwa mwanamume huyo.+ 23  Ndipo mwanamume huyo akasema: “Hatimaye huyu ni mfupa wa mifupa yanguNa nyama ya nyama yangu. Huyu ataitwa Mwanamke,Kwa sababu alitolewa+ katika mwanamume.” 24  Ndiyo sababu mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana* na mke wake, nao watakuwa mwili mmoja.+ 25  Na wote wawili wakaendelea kuwa uchi,+ huyo mwanamume na mke wake; lakini hawakuona aibu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “na jeshi lake lote likakamilika.”
Hili ndilo andiko la kwanza kutaja jina la pekee la Mungu, יהוה (YHWH). Angalia Nyongeza A4.
Au “nafsi hai.” Kiebrania, neʹphesh, ambalo kihalisi linamaanisha “kiumbe anayepumua.” Angalia Kamusi.
Tnn., “na kuwa vichwa vinne.”
Au “Tigri.”
Au “ataendelea kuwa.”