Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawajibu Mashtaka Yote Yanayotolewa Dhidi Yao?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawajibu Mashtaka Yote Yanayotolewa Dhidi Yao?

 Mashahidi wa Yehova wanafuata ushauri wa Biblia wa kutojibu mashtaka na dhihaka zote. Kwa mfano, methali moja ya Biblia inasema hivi: “Anayemrekebisha mtu mwenye dhihaka anajipatia aibu yeye mwenyewe.” (Methali 9:7, 8; 26:4) Badala ya kukengeushwa na kuanza kubishana kuhusu shtaka la uwongo, sisi hukazia fikira kumpendeza Mungu.​—Zaburi 119:69.

 Bila shaka, kuna “wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” (Mhubiri 3:7) Hivyo, tunajibu watu wanyoofu wanaotaka kujua kweli, lakini tunaepuka mabishano yasiyo na maana. Kwa kufanya hivyo, tunafuata mafundisho na kielelezo cha Yesu na Wakristo wa mapema.

  •   Yesu hakujibu lolote aliposhtakiwa kwa uwongo mbele ya Pilato. (Mathayo 27:11-​14; 1 Petro 2:​21-​23) Vivyo hivyo, Yesu hakujibu mashtaka kwamba yeye ni mlevi na mlafi. Badala yake, aliacha matendo yake yathibitishe yeye ni mtu wa aina gani kupatana na kanuni hii: “Hekima huonyeshwa kuwa yenye uadilifu kwa matendo yake.” (Mathayo 11:19) Hata hivyo, hali zilipodai aseme, alifanya hivyo kwa ujasiri mbele ya wale waliomchongea.​—Mathayo 15:​1-3; Marko 3:​22-​30.

     Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasivunjwe moyo na mashtaka ya uwongo. Alisema hivi: “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanapowashutumu na kuwatesa na kusema kwa uwongo kila namna ya jambo baya juu yenu kwa ajili yangu.” (Mathayo 5:11, 12) Hata hivyo, Yesu alisema kwamba ikiwa mashtaka kama hayo yangewapa wafuasi wake nafasi ya kutoa ushahidi, yeye angetimiza ahadi hii: “Nitawapa ninyi kinywa na hekima, ambayo wapinzani wenu wote wakiwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.”​—Luka 21:12-​15.

  •   Mtume Paulo aliwashauri Wakristo waepuke kubishana bila kusudi na wapinzani, akisema kwamba mabishano kama hayo “hayana faida na ni ya ubatili.”​—Tito 3:9; Waroma 16:17, 18.

  •   Mtume Petro aliwatia moyo Wakristo watetee imani yao wakati wowote wanapoweza. (1 Petro 3:​15) Hata hivyo, alitambua kwamba mara nyingi inafaa zaidi kufanya hivyo kwa matendo badala ya maneno. Aliandika hivi: “Kwa kutenda mema mzibe maneno ya ujinga ya watu wasio na akili.”​—1 Petro 2:12-15.