Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

alfa27/stock.adobe.com

KAMPENI YA UKUMBUSHO

Yesu Atakomesha Uhalifu

Yesu Atakomesha Uhalifu

 Yesu anajua maana ya kuteseka kwa sababu ya uhalifu na ukosefu wa haki. Alishtakiwa kwa uwongo, akapigwa ingawa hakuwa amekosea, akafikishwa mahakamani kwa tuhuma za uwongo, akahukumiwa kimakosa, na akauawa kikatili. Licha ya kwamba hakuwa na hatia, alikubali bila ubinafsi kudhabihu “uhai wake uwe fidia badala ya wengi.” (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Sasa, akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, hivi karibuni atahakikisha haki inatendeka duniani kote, na kukomesha uhalifu kabisa.​—Isaya 42:3.

 Biblia inafafanua jinsi ulimwengu utakavyokuwa baada ya Yesu kuchukua hatua:

  •    “Watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo. Lakini wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.”​—Zaburi 37:10, 11.

 Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo yote ambayo Yesu ametufanyia na ambayo atatufanyia wakati ujao? Kwenye Luka 22:19, Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake. Hiyo ndiyo sababu kila mwaka Mashahidi wa Yehova hukutana ili kuadhimisha kifo chake. Tunakualika ujiunge nasi kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu Jumapili, Machi 24, 2024.

Tafuta Mahali Ukumbusho Utakapofanyika