Isaya 42:1-25

  • Mtumishi wa Mungu na kazi yake (1-9)

    • ‘Jina langu ni Yehova’ (8)

  • Wimbo mpya wa kumsifu Yehova (10-17)

  • Israeli ni kipofu na kiziwi (18-25)

42  Tazama! Mtumishi wangu,+ ninayemtegemeza! Mchaguliwa wangu,+ ambaye nimemkubali!*+ Nimeitia roho yangu ndani yake;+Atayaletea mataifa haki.+   Hatalia kwa sauti wala kupaza sauti yake,Naye hatafanya sauti yake isikike barabarani.+   Hataponda tete lililovunjika,Wala hatazima utambi unaofifia.+ Ataleta haki kwa uaminifu.+   Hatafifia wala kupondwa mpaka atakapoimarisha haki duniani;+Na visiwa vinaendelea kungojea sheria* yake.   Hivi ndivyo anavyosema Mungu wa kweli, Yehova,Muumba wa mbingu na Mkuu aliyezitandaza,+Yule aliyeitandaza dunia na mazao yake,+Yule anayewapa pumzi watu waliomo+Na kuwapa roho wale wanaotembea humo:+   “Mimi, Yehova, nimekuita katika uadilifu;Nimekushika mkono wako. Nitakulinda na kukutoa uwe agano kwa ajili ya watu+Na uwe nuru kwa mataifa,+   Ili uyafungue macho yaliyopofuka,+Ili umtoe mfungwa katika gereza lililo chini ya ardhiNa wale wanaoketi gizani kutoka gerezani.+   Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu;Simpi yeyote utukufu wangu,*Wala kuzipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.+   Tazameni, mambo ya kwanza yametokea;Sasa ninatangaza mambo mapya. Kabla hayajatokea, ninawaambia kuyahusu.”+ 10  Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+Sifa yake kutoka kwenye miisho ya dunia,+Ninyi mnaoshuka baharini na pia vyote vinavyoijaza,Ninyi visiwa na wakaaji wake.+ 11  Nyika na majiji yake na yapaze sauti yao,+Makao ambamo Kedari anaishi.+ Wale wanaokaa kwenye jabali na wapige vigelegele kwa shangwe;Na wapaze sauti kutoka kwenye vilele vya milima. 12  Na wamtukuze YehovaNa watangaze sifa zake katika visiwa.+ 13  Yehova atatoka kama mwanamume hodari.+ Ataamsha bidii yake kama shujaa.+ Atapaza sauti, naam, atapiga kelele za vita;Ataonyesha kwamba ana nguvu kuliko maadui wake.+ 14  “Nimenyamaza kwa muda mrefu. Niliendelea kukaa kimya na kujizuia. Kama mwanamke anayezaa,Nitalia kwa uchungu, nitahemahema, na kutweta wakati uleule. 15  Nitaiharibu milima na vilimaNa kukausha kabisa majani yake yote. Nitaibadili mito iwe visiwa*Na kuyakausha kabisa madimbwi ya maji yenye matete.+ 16  Nitawaongoza vipofu kwenye njia wasiyoijua+Na kuwafanya watembee kwenye vijia wasivyovijua.+ Nitabadili giza lililo mbele yao liwe nuru+Na kubadili eneo lenye mawemawe kuwa nchi tambarare.+ Hivyo ndivyo nitakavyowatendea, nami sitawaacha.” 17  Watarudishwa nyuma na kuaibishwa kabisa,Wale wanaotumaini sanamu za kuchongwa,Wale wanaoziambia sanamu za chuma:* “Ninyi ni miungu yetu.”+ 18  Sikilizeni, ninyi viziwi;Tazameni na mwone, ninyi vipofu.+ 19  Ni nani aliye kipofu isipokuwa mtumishi wangu,Aliye kiziwi sana kama mjumbe ninayemtuma? Ni nani aliye kipofu sana kama yule ambaye amethawabishwa,Aliye kipofu sana kama mtumishi wa Yehova?+ 20  Unaona mambo mengi, lakini huendelei kukaa macho. Unafungua masikio yako, lakini husikilizi.+ 21  Kwa sababu ya uadilifu wake,Yehova amependezwa kuitukuza sheria* na kuifanya iwe na utukufu. 22  Lakini watu hawa ni watu walioporwa na kutekwa nyara;+Wote wamenaswa katika mashimo na kufichwa magerezani.+ Wameporwa na hakuna yeyote wa kuwaokoa,+Nao wametekwa nyara na hakuna yeyote wa kusema: “Warudisheni!” 23  Ni nani kati yenu atakayesikia jambo hili? Ni nani atakayetega sikio na kusikiliza kwa ajili ya wakati ujao? 24  Ni nani aliyemtia Yakobo mikononi mwa watekaji nyaraNa Israeli mikononi mwa waporaji? Je, si Yehova, Yule ambaye tumemtendea dhambi? Walikataa kutembea katika njia Zake,Nao hawakutii sheria* Yake.+ 25  Basi Yeye akaendelea kummwagia ghadhabu,Hasira yake na ghadhabu ya vita.+ Iliteketeza kila kitu kumzunguka, lakini hakulikazia jambo hilo fikira.+ Iliwaka dhidi yake, lakini hakulitia jambo hilo moyoni.+

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yangu imemkubali.”
Au “mafundisho.”
Au “Sishiriki utukufu wangu na yeyote.”
Au “maeneo ya pwani.”
Au “sanamu za kuyeyushwa.”
Au “mafundisho.”
Au “mafundisho.”