Kulingana na Yohana 18:1-40

  • Yuda amsaliti Yesu (1-9)

  • Petro atumia upanga (10, 11)

  • Yesu apelekwa kwa Anasi (12-14)

  • Petro amkana Yesu mara ya kwanza (15-18)

  • Yesu mbele ya Anasi (19-24)

  • Petro amkana Yesu mara ya pili na ya tatu (25-27)

  • Yesu mbele ya Pilato (28-40)

    • “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu” (36)

18  Baada ya kusema mambo hayo, Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake, wakavuka Bonde la Kidroni*+ na kufika kwenye bustani, naye akaingia humo pamoja nao.+  Sasa Yuda msaliti wake alijua mahali hapo, kwa sababu mara nyingi Yesu alikutana hapo na wanafunzi wake.  Basi Yuda akaja na kikosi cha wanajeshi, maofisa wa wakuu wa makuhani na wa Mafarisayo, wakafika hapo wakiwa na mienge, taa, na silaha.+  Kisha Yesu akijua mambo yote ambayo yangempata, akawakaribia na kuwauliza: “Mnamtafuta nani?”  Wakamjibu: “Yesu Mnazareti.”+ Akawaambia: “Ni mimi.” Basi Yuda msaliti wake, alikuwa pia amesimama pamoja nao.+  Hata hivyo, Yesu alipowaambia, “Ni mimi,” wakarudi nyuma na kuanguka chini.+  Basi akawauliza tena: “Mnamtafuta nani?” Wakasema: “Yesu Mnazareti.”  Yesu akajibu: “Niliwaambia ni mimi. Basi, ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni wanaume hawa waende.”  Hilo lilitimiza maneno aliyokuwa amesema: “Kati ya wale ulionipa, sikumpoteza hata mmoja.”+ 10  Simoni Petro alikuwa na upanga, basi akauchomoa na kumpiga mtumwa wa kuhani mkuu na kumkata sikio la kulia.+ Jina la mtumwa huyo lilikuwa Malko. 11  Hata hivyo, Yesu akamwambia Petro: “Rudisha upanga ndani ya ala yake.+ Je, sipaswi kukinywa kikombe ambacho Baba amenipa?”+ 12  Ndipo wanajeshi na kamanda wa jeshi na maofisa wa Wayahudi wakamkamata Yesu na kumfunga. 13  Kwanza wakampeleka kwa Anasi, kwa maana alikuwa baba mkwe wa Kayafa,+ ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo.+ 14  Kwa kweli, Kayafa ndiye aliyewashauri Wayahudi kwamba ilikuwa kwa faida yao mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.+ 15  Sasa Simoni Petro na mwanafunzi mwingine wakamfuata Yesu.+ Mwanafunzi huyo alijulikana na kuhani mkuu, naye akaingia pamoja na Yesu ndani ya ua wa kuhani mkuu, 16  lakini Petro alikuwa amesimama nje kwenye mlango.* Basi yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akatoka nje na kuzungumza na mlinzi wa mlango, akamwingiza Petro ndani. 17  Basi kijakazi, aliyekuwa mlinzi wa mlango, akamuuliza Petro: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu, sivyo?” Petro akajibu: “Hapana.”+ 18  Sasa wale watumwa na maofisa walikuwa wamesimama kuzunguka moto wa makaa waliokuwa wameuwasha, kwa sababu kulikuwa na baridi nao walikuwa wakiota moto. Petro pia alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto. 19  Basi mkuu wa makuhani akamuuliza Yesu kuhusu wanafunzi wake na kuhusu mafundisho yake. 20  Yesu akamjibu: “Nimezungumza na ulimwengu hadharani. Sikuzote nilifundisha katika sinagogi na hekaluni,+ ambapo Wayahudi wote hukusanyika, nami sikusema jambo lolote kwa siri. 21  Kwa nini unaniuliza? Waulize wale waliosikia nilichowaambia. Ona! Hawa wanajua nilichosema.” 22  Baada ya kusema hivyo, mmoja wa maofisa aliyekuwa amesimama hapo karibu akampiga Yesu kofi usoni+ na kusema: “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu mkuu wa makuhani?” 23  Yesu akamjibu: “Ikiwa nimesema vibaya, toa ushahidi kuhusu kosa hilo; lakini ikiwa nimesema jambo lililo sawa, kwa nini unanipiga?” 24  Kisha Anasi akaagiza Yesu apelekwe kwa kuhani mkuu Kayafa,+ akiwa amefungwa. 25  Sasa Simoni Petro alikuwa amesimama hapo akiota moto. Ndipo wakamwambia: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wake, sivyo?” Akakana na kusema: “Hapana.”+ 26  Mmoja wa watumwa wa kuhani mkuu, aliyekuwa mtu wa ukoo wa yule aliyekatwa sikio+ na Petro, akasema: “Nilikuona katika bustani pamoja naye, sivyo?” 27  Hata hivyo, Petro akakana tena, na papo hapo jogoo akawika.+ 28  Kisha wakamtoa Yesu kwa Kayafa na kumpeleka kwenye makao ya gavana.+ Ilikuwa asubuhi mapema. Lakini wao hawakuingia ndani ya makao ya gavana, ili wasitiwe unajisi+ kwa sababu walitaka kula mlo wa Pasaka. 29  Basi Pilato akatoka nje na kuwauliza: “Mna mashtaka gani kumhusu mtu huyu?” 30  Wakamjibu: “Kama mtu huyu hangekuwa mkosaji,* hatungemkabidhi kwako.” 31  Basi Pilato akawaambia: “Mchukueni mkamhukumu kulingana na sheria yenu.”+ Wayahudi wakamwambia: “Si halali kwetu kumuua mtu yeyote.”+ 32  Hilo lilitimiza maneno aliyosema Yesu ili kuonyesha angekufa kifo cha aina gani.+ 33  Basi Pilato akaingia tena ndani ya makao ya gavana, akamwita Yesu na kumuuliza: “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?”+ 34  Yesu akajibu: “Je, unauliza hivyo kwa kujitungia, au uliambiwa na watu wengine kunihusu?” 35  Pilato akajibu: “Mimi si Myahudi, sivyo? Taifa lako na wakuu wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Ulifanya nini?” 36  Yesu akajibu:+ “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.+ Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi.+ Lakini, kama ilivyo, Ufalme wangu hautoki katika chanzo hiki.” 37  Basi Pilato akamuuliza: “Kwa hiyo, wewe ni mfalme?” Yesu akajibu: “Wewe mwenyewe unasema kwamba mimi ni mfalme.+ Nimezaliwa kwa ajili ya hili, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi kuhusu kweli.+ Kila mtu aliye upande wa kweli huisikiliza sauti yangu.” 38  Pilato akamuuliza: “Kweli ni nini?” Baada ya kusema hivyo, akatoka nje tena na kuwaambia Wayahudi: “Sijampata na kosa lolote.+ 39  Isitoshe, mna desturi kwamba niwafungulie mtu siku ya Pasaka.+ Basi, mnataka niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?” 40  Wakasema tena kwa sauti kubwa: “Si mtu huyu, bali Baraba!” Baraba alikuwa mwizi.+

Maelezo ya Chini

Au “bonde la majira ya baridi kali la Kidroni.”
Au “mwingilio.”
Au “mhalifu.”