Kulingana na Yohana 14:1-31

  • Yesu ndiye njia pekee ya kumkaribia Mungu (1-14)

    • ‘Mimi ndiye njia, kweli, na uzima’ (6)

  • Yesu awaahidi wanafunzi roho takatifu (15-31)

    • “Baba ni mkuu kuliko mimi” (28)

14  “Mioyo yenu isitaabike.+ Iweni na imani* katika Mungu;+ iweni na imani pia katika mimi.  Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi. Kama sivyo, ningewaambia kwa maana ninaenda zangu kuwatayarishia mahali.+  Pia, nikienda na kuwatayarishia mahali, nitakuja tena nami nitawapokea nyumbani kwangu, ili mahali nilipo, ninyi pia muwe hapo.+  Nanyi mnajua njia ya mahali ninakoenda.”  Tomasi+ akamwambia: “Bwana, sisi hatujui unakoenda. Tunawezaje kuijua njia?”  Yesu akamwambia: “Mimi ndiye njia+ na kweli+ na uzima.+ Hakuna mtu anayekuja kwa Baba bila kupitia kwangu.+  Kama ninyi mngenijua, mngemjua Baba yangu pia; tangu sasa na kuendelea ninyi mnamjua na mmemwona.”+  Filipo akamwambia: “Bwana, tuonyeshe Baba na hilo linatutosha.”  Yesu akamwambia: “Je, hata baada ya kuwa pamoja nanyi kwa muda mrefu hivyo, bado Filipo hujanijua? Yeyote ambaye ameniona mimi amemwona Baba pia.+ Kwa nini unasema, ‘Tuonyeshe Baba’? 10  Je, huamini kwamba mimi nimo katika muungano pamoja na Baba, naye Baba yumo katika muungano pamoja nami?+ Mambo ninayowaambia sisemi kwa kujitungia,+ bali Baba ambaye hukaa katika muungano pamoja nami anafanya kazi zake. 11  Iweni na imani kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba na Baba yumo katika muungano pamoja nami; kama sivyo, iweni na imani kwa sababu ya kazi zenyewe.+ 12  Kwa kweli ninawaambia, yeyote anayeniamini atafanya pia kazi ambazo mimi hufanya; naye atafanya kazi kubwa kuliko hizi,+ kwa sababu ninaenda zangu kwa Baba.+ 13  Pia, lolote mtakaloomba katika jina langu nitalifanya, ili Baba atukuzwe kuhusiana na Mwana.+ 14  Mkiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya. 15  “Ikiwa mnanipenda, mtazishika amri zangu.+ 16  Nami nitamwomba Baba, naye atawapa msaidizi* mwingine awe pamoja nanyi milele,+ 17  roho ya ile kweli,+ ambayo ulimwengu hauwezi kuipokea, kwa sababu hauioni wala kuijua.+ Ninyi mnaijua, kwa sababu hiyo hukaa pamoja nanyi na imo ndani yenu. 18  Sitawaacha ninyi mayatima. Ninakuja kwenu.+ 19  Bado muda kidogo nao ulimwengu hautaniona tena, lakini ninyi mtaniona,+ kwa sababu ninaishi, nanyi mtaishi. 20  Siku hiyo mtajua kwamba nimo katika muungano pamoja na Baba yangu nanyi mumo katika muungano pamoja nami, nami nimo katika muungano pamoja nanyi.+ 21  Yeyote aliye na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye anayenipenda. Na yeyote anayenipenda atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujionyesha waziwazi kwake.” 22  Yuda,+ sio Yuda Iskariote, akamuuliza: “Bwana, imekuwaje kwamba unakusudia kujionyesha waziwazi kwetu bali si kwa ulimwengu?” 23  Yesu akamjibu: “Ikiwa yeyote ananipenda, atalishika neno langu,+ naye Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake na kukaa pamoja naye.+ 24  Yeyote asiyenipenda hayashiki maneno yangu. Neno mnalolisikia si langu, bali ni la Baba aliyenituma.+ 25  “Nimewaambia mambo haya nikiwa bado pamoja nanyi. 26  Lakini msaidizi, roho takatifu, ambayo Baba ataituma katika jina langu, hiyo itawafundisha mambo yote na kuwakumbusha mambo yote niliyowaambia.+ 27  Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu.+ Siwapi amani kwa njia ile ambayo ulimwengu huitoa. Mioyo yenu isitaabike wala kuogopa. 28  Mlisikia nikiwaambia, ‘Ninaenda, nami nitakuja tena kwenu.’ Kama mngenipenda, mngeshangilia kwamba ninaenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.+ 29  Kwa hiyo sasa nimewaambia kabla jambo hilo halijatokea, ili litakapotokea mwamini.+ 30  Sitasema nanyi tena mambo mengi, kwa maana mtawala wa ulimwengu+ anakuja, naye hana uwezo juu yangu.*+ 31  Lakini, ili ulimwengu ujue kwamba ninampenda Baba, ninafanya kama vile Baba alivyoniamuru.+ Simameni tuondoke hapa.

Maelezo ya Chini

Au “Onyesheni imani.”
Au “mfariji.”
Au “hana nguvu juu yangu.”