Kwa Waroma 14:1-23

  • Msihukumiane (1-12)

  • Msiwakwaze wengine (13-18)

  • Jitahidi kupata amani na umoja (19-23)

14  Mkaribisheni mtu aliye na udhaifu katika imani yake,+ lakini msihukumu kuhusu maoni yanayotofautiana.*  Mtu mmoja ana imani ya kula kila kitu, lakini mtu aliye dhaifu hula mboga za majani tu.  Yule anayekula asimdharau yule asiyekula, na yule asiyekula asimhukumu yule anayekula,+ kwa maana Mungu amemkaribisha.  Wewe ni nani ili umhukumu mtumishi wa mwingine?+ Kwa bwana wake yeye husimama au kuanguka.+ Kwa kweli, atasimamishwa, kwa maana Yehova* anaweza kumsimamisha.  Mtu mmoja anahukumu siku moja kuwa muhimu kuliko nyingine;+ mwingine anahukumu siku moja kuwa sawa na nyingine zote;+ kila mtu na asadikishwe kikamili katika akili yake mwenyewe.  Yule anayeishika siku huishika kwa ajili ya Yehova.* Pia, yule anayekula, anakula kwa ajili ya Yehova,* kwa maana yeye humshukuru Mungu;+ na yule asiyekula, hali chakula kwa ajili ya Yehova,* na bado yeye humshukuru Mungu.+  Hakuna hata mmoja wetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe tu,+ na hakuna yeyote anayekufa kwa ajili yake mwenyewe tu.  Kwa maana tukiishi, tunaishi kwa ajili ya Yehova,*+ na tukifa, tunakufa kwa ajili ya Yehova.* Basi tukiishi na tukifa, sisi ni wa Yehova.*+  Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na akawa hai tena, ili awe Bwana juu ya waliokufa na walio hai pia.+ 10  Lakini kwa nini unamhukumu ndugu yako?+ Au kwa nini pia unamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.+ 11  Kwa maana imeandikwa: “‘Kwa hakika kama ninavyoishi,’+ asema Yehova,* ‘kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utakiri waziwazi kwa Mungu.’”+ 12  Hivyo basi, kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.+ 13  Kwa hiyo tusiwe tukihukumiana tena,+ badala yake tuazimie kutoweka kikwazo au kizuizi mbele ya ndugu.+ 14  Ninajua, nami ninaamini katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu ambacho ndani yake chenyewe ni kichafu;+ isipokuwa tu mtu anapokiona kitu kuwa kichafu, kwake yeye hicho huwa kichafu. 15  Kwa maana ikiwa unamkasirisha ndugu yako kwa sababu ya chakula, wewe hutembei tena kulingana na upendo.+ Kwa chakula chako usimwangamize* yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+ 16  Kwa hiyo, msiache mema mnayofanya yasemwe vibaya. 17  Kwa maana Ufalme wa Mungu haumaanishi kula na kunywa,+ bali unamaanisha uadilifu na amani na shangwe pamoja na roho takatifu. 18  Kwa maana yeyote anayemtumikia Kristo kwa njia hii anakubalika kwa Mungu naye ana kibali cha wanadamu. 19  Hivyo basi, na tufuatilie mambo yanayoleta amani+ na mambo ya kujengana.+ 20  Acheni kuibomoa kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula tu.+ Ni kweli, vitu vyote ni safi, lakini ni vibaya* kwa mtu kula ikiwa itasababisha kikwazo.+ 21  Ni vema kutokula nyama au kunywa divai au kufanya jambo lolote ambalo litamkwaza ndugu yako.+ 22  Imani uliyo nayo, endelea kuwa nayo mbele za Mungu. Mwenye furaha ni mtu asiyejihukumu mwenyewe kwa yale anayokubali. 23  Lakini ikiwa ana shaka, yeye akila tayari atakuwa amehukumiwa kuwa mwenye hatia, kwa sababu hali kwa imani. Kwa kweli, kila kitu ambacho hakitokani na imani ni dhambi.

Maelezo ya Chini

Au labda, “maswali ya ndani.”
Au “usimharibu.”
Au “kosa.”