Kwa Waroma 13:1-14

  • Kujitiisha chini ya mamlaka (1-7)

    • Kulipa kodi (6, 7)

  • Upendo hutimiza Sheria (8-10)

  • Jiendesheni kama wakati wa mchana (11-14)

13  Kila mtu na ajitiishe* kwa mamlaka zilizo kubwa,+ kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kupitia Mungu;+ mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.+  Kwa hiyo, yeyote anayepinga mamlaka amechukua msimamo dhidi ya mpango wa Mungu; wale ambao wamechukua msimamo dhidi ya mpango huo, watajiletea hukumu wao wenyewe.  Kwa maana watawala ni kitu cha kuogopesha, si kwa tendo jema, bali kwa baya.+ Je, unataka usiogope hiyo mamlaka? Endelea kufanya mema,+ nayo itakusifu;  kwa maana hiyo ni mhudumu wa Mungu kwako kwa faida yako. Lakini ikiwa unafanya mabaya, ogopa, kwa maana haichukui upanga bila kusudi. Hiyo ni mhudumu wa Mungu, nayo hulipiza kisasi ili kuonyesha ghadhabu* dhidi ya yule anayefanya mabaya.  Kwa hiyo kuna sababu ya lazima kwenu kujitiisha, si kwa sababu ya ghadhabu hiyo tu, bali pia kwa sababu ya dhamiri yenu.+  Ndiyo maana mnalipa kodi pia; kwa kuwa wao ni watumishi wa Mungu kwa watu wote wakitumikia daima kwa kusudi hili.  Wapeni wote haki zao: yule anayetaka kodi, kodi;+ yule anayetaka ushuru, ushuru; yule anayetaka woga, woga huo;+ yule anayetaka heshima, heshima hiyo.+  Msiwe na deni lolote kwa mtu yeyote, isipokuwa kupendana,+ kwa maana yeyote anayempenda mwanadamu mwenzake ameitimiza sheria.+  Kwa maana sheria zinazosema, “Usifanye uzinzi,+ usiue,+ usiibe,+ usitamani,”+ na amri nyingine yoyote iliyopo, zimejumlishwa katika maneno haya: “Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”+ 10  Upendo haumfanyii uovu jirani;+ kwa hiyo, upendo ndio utimizo wa sheria.+ 11  Nanyi fanyeni hivi kwa sababu mnayajua majira, kwamba tayari ni saa yenu ya kuamka kutoka usingizini,+ kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko wakati tulipoanza kuamini. 12  Usiku umesonga sana; mchana umekaribia. Kwa hiyo, na tuyaache matendo ya giza+ na tuvae silaha za nuru.+ 13  Na tujiendeshe kwa adabu+ kama wakati wa mchana, si katika karamu zenye vurugu* na ulevi, si katika ngono isiyo halali na mwenendo mpotovu,*+ si katika mizozo na wivu.+ 14  Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo,+ na msiwe mkipanga mapema kwa ajili ya tamaa za mwili.+

Maelezo ya Chini

Au “Kila nafsi na ijitiishe.”
Au “kuleta adhabu.”
Au “karamu za kupindukia.”
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Wingi wa neno la Kigiriki a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.