Isaya 2:1-22

  • Mlima wa Yehova wainuliwa (1-5)

    • Panga zitakuwa majembe ya plau (4)

  • Siku ya Yehova itawafedhehesha wenye majivuno (6-22)

2  Hili ndilo jambo ambalo Isaya mwana wa Amozi aliona katika maono kuhusu Yuda na Yerusalemu:+   Katika siku za mwisho,*Mlima wa nyumba ya YehovaUtaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+Nao utainuliwa juu ya vilima,Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+   Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema: “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+ Naye atatufundisha njia zake,Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+ Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+   Atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifaNa kunyoosha* mambo kuhusiana na watu wengi. Watafua panga zao ziwe majembe ya plauNa mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa lingine,Wala hawatajifunza vita tena kamwe.+   Enyi nyumba ya Yakobo, njooni,Na tutembee katika nuru ya Yehova.+   Kwa maana umewaacha watu wako, nyumba ya Yakobo,+Kwa sababu wamejaa vitu vya kutoka Mashariki;Wanafanya uchawi+ kama Wafilisti,Nao wana watoto wengi wa wageni.   Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,Na hazina zao hazina kikomo. Nchi yao imejaa farasi,Na magari yao hayana idadi.+   Nchi yao imejaa miungu ya ubatili.+ Wao huinamia kazi ya mikono yao wenyewe,Kile ambacho vidole vyao vimetengeneza.   Basi mtu huinama chini, hujishusha chini,Nawe huwezi kuwasamehe. 10  Ingia ndani ya mwamba, ujifiche mavumbiniKwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopeshaNa fahari yake kuu.+ 11  Macho ya mwanadamu yenye majivuno yatashushwa,Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.* Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo. 12  Kwa maana hiyo ni siku ya Yehova wa majeshi.+ Itakuja dhidi ya kila mtu mwenye majivuno na anayejiinua,Itakuja dhidi ya kila mtu, aliyekwezwa au aliye chini,+ 13  Dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni ambayo ni mirefu na iliyo juuNa dhidi ya mialoni yote ya Bashani, 14  Dhidi ya milima yote mirefuNa dhidi ya vilima vyote virefu, 15  Dhidi ya kila mnara mrefu na kila ukuta wenye ngome, 16  Dhidi ya meli zote za Tarshishi+Na dhidi ya mashua zote zinazotamanika. 17  Majivuno ya mwanadamu yatashushwa,Na kiburi cha wanadamu kitainama chini.* Yehova peke yake ndiye atakayekwezwa siku hiyo. 18  Miungu ya ubatili itatoweka kabisa.+ 19  Na watu wataingia ndani ya mapango ya miambaNa ndani ya mashimo ardhini,+Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopeshaNa fahari yake kuu,+Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu. 20  Siku hiyo wanadamu watachukua miungu yao ya ubatili ya fedha na dhahabuAmbayo walijitengenezea ili waiinamieNao watawatupia panya* na popo,+ 21  Ili kuingia katika mashimo yaliyo kwenye miambaNa ndani ya mipasuko ya majabali,Kwa sababu ya uwepo wa Yehova unaoogopeshaNa fahari yake kuu,Anapoinuka ili kuifanya dunia itetemeke kwa hofu. 22  Kwa faida yenu wenyewe, acheni kumtumaini mwanadamu,Ambaye ni pumzi tu iliyo katika mianzi ya pua yake.* Kwa nini afikiriwe?

Maelezo ya Chini

Au “Katika kipindi cha mwisho cha zile siku.”
Au “mafundisho yatatoka.”
Au “kurekebisha.”
Au “kitanyenyekezwa.”
Au “kitanyenyekezwa.”
Au “wanyama wanaoguguna ambao hula sana.”
Au “Ambaye pumzi yake iko katika mianzi ya pua yake.”