Isaya 35:1-10

  • Paradiso yarudishwa (1-7)

    • Vipofu wataona; viziwi watasikia (5)

  • Njia ya Utakatifu kwa ajili ya waliokombolewa (8-10)

35  Nyika na nchi iliyokauka zitafurahi,+Na jangwa tambarare litashangilia na kuchanua maua kama zafarani.+   Hakika itachanua maua;+Itashangilia na kupiga vigelegele vya shangwe. Itapewa utukufu wa Lebanoni,+Fahari ya Karmeli+ na ya Sharoni.+ Watauona utukufu wa Yehova, fahari ya Mungu wetu.   Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu,Na myaimarishe magoti yanayotetemeka.+   Waambieni wale wanaohangaika moyoni: “Iweni na nguvu. Msiogope. Tazameni! Mungu wenu atakuja na kisasi,Mungu atakuja na malipo.+ Atakuja na kuwaokoa ninyi.”+   Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa,+Na masikio ya viziwi yatazibuliwa.+   Wakati huo kilema ataruka kama paa,+Na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.+ Kwa maana maji yatabubujika nyikani,Na vijito katika jangwa tambarare.   Na ardhi iliyokaushwa na joto itakuwa kama dimbwi lenye matete,Na ardhi yenye kiu itakuwa kama mabubujiko ya maji.+ Katika makao ambamo mbwamwitu walipumzika,+Kutakuwa na majani mabichi na matete na mafunjo.   Na huko kutakuwa na barabara kuu,+Naam, njia inayoitwa Njia ya Utakatifu. Mtu asiye safi hatasafiri kwenye njia hiyo.+ Imetengwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo;Hakuna mtu yeyote mpumbavu atakayepotea na kuingia katika njia hiyo.   Hakuna simba atakayekuwa huko,Na hakuna wanyama hatari wa mwituni watakaokuja kwenye njia hiyo. Hawatapatikana huko;+Wale waliokombolewa tu ndio watakaotembea katika njia hiyo.+ 10  Wale waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa kilio cha shangwe.+ Shangwe isiyo na kikomo itakuwa taji la vichwa vyao.+ Watapata shangwe na furaha,Na huzuni na kilio cha uchungu vitatoweka.+

Maelezo ya Chini