Hamia kwenye habari

Je, Biblia Ina Habari Sahihi Kuhusu Maisha ya Yesu?

Je, Biblia Ina Habari Sahihi Kuhusu Maisha ya Yesu?

Jibu la Biblia

 Mwandishi wa Biblia, Luka, alisema hivi kuhusu masimulizi aliyoandika kuhusu maisha ya Yesu: “nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi.”—Luka 1:3.

 Watu fulani wanadai kwamba masimulizi ya maisha ya Yesu yaliyoandikwa katika Vitabu vya Injili, yaani, maandishi ya watu walioishi wakati wake kama vile Mathayo, Marko, Luka, na Yohana, yalibadilishwa wakati fulani katika karne ya nne.

 Hata hivyo, sehemu fulani muhimu ya Injili ya Yohana ilipatikana nchini Misri mwanzoni mwa karne ya 20. Sehemu hiyo inajulikana kama Papyrus Rylands 457 (P52) na imehifadhiwa katika Maktaba ya John Rylands Library, huko Manchester, Uingereza. Ina kitabu cha Yohana 18:31-33, 37, 38 katika Biblia za leo.

 Hii ndiyo sehemu ya zamani zaidi ya hati za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Wasomi wengi wanaamini kwamba sehemu hiyo iliandikwa karibu mwaka wa 125 W.K., miaka 25hivi baada ya maandishi ya awali kuandikwa. Maandishi ya sehemu hii yanalingana kabisa na maandishi ya hati za baadaye.