Hamia kwenye habari

Masimulizi Yanayomhusu Yesu Yaliandikwa Lini?

Masimulizi Yanayomhusu Yesu Yaliandikwa Lini?

Jibu la Biblia

 Mtume Yohana aliandika hivi kuhusu mambo aliyoripoti kuhusu maisha ya Yesu: “Yeye ambaye ameona hilo ametoa ushahidi, nao ushahidi wake ni wa kweli, na mtu huyo anajua kwamba yeye husema mambo ya kweli, ili ninyi pia mweze kuamini.”—Yohana 19:35.

 Sababu moja ya kuamini masimulizi ya Injili yaliyoandikwa na Mathayo, Marko, Luka, na Yohana ni kwamba waliandika wakati watu wengi waliojionea matukio hayo bado walikuwa hai. Kulingana na chanzo kimoja cha habari, Injili ya Mathayo iliandikwa katika mwaka wa nane baada ya kifo cha Yesu, yaani, karibu mwaka wa 41 W.K. Wasomi wengi wanasema Injili hiyo iliandikwa baadaye, lakini wote wanakubali kwamba vitabu vyote vya Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki viliandikwa katika karne ya kwanza W.K.

 Watu waliomwona Yesu akiwa hai duniani, waliojionea akifa, na akifufuliwa na wangethibitisha masimulizi ya Injili. Pia, wangefunua mambo yoyote ambayo hayakuandikwa vizuri, ikiwa yalikuwapo. Profesa F. F. Bruce anasema hivi: “Mojawapo ya mambo yenye nguvu katika mahubiri ya awali ya mitume ni uvutio wenye uhakika kwa maarifa ya wasikiaji; si kwamba walisema tu, ‘Sisi ni mashahidi wa mambo haya,’ bali pia, ‘Kama mjuavyo nyinyi wenyewe’ (Matendo 2:22).”