Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Meza ya Bwana Tofauti na Dini Zingine?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Meza ya Bwana Tofauti na Dini Zingine?

 Tunafuataka kabisa mambo yenye Biblia inasema wakati tunafanya chakula cha mangaribi cha Bwana, yenye inaitwa pia “Meza ya Bwana” na Ukumbusho wa kifo ya Yesu. (1 Wakorinto 11:20; King James Version) Lakini, mambo yenye dini za mingi zinaamini na kufanya wakati wa Meza ya Bwana haipatane na Biblia.

Juu ya nini tunafanyaka Meza ya Bwana?

 Tunafanyaka Meza ya Bwana juu ya kukumbuka kifo ya Yesu na kuonyesha shukrani juu ya zabihu yenye alitoa kwa ajili yetu. (Matayo 20:28; 1 Wakorinto 11:24) Watu fulani wanawazaka kama zambi zao zitasamehewa kama wanakula Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Lakini Biblia haiseme vile. Inafundisha kama tunapaswa kumuamini Yesu juu zambi zetu zisamehewe, hapana kufanya desturi fulani ya kidini.​—Waroma 3:25; 1 Yohana 2:1, 2.

Tunapaswa kufanya Meza ya Bwana mara ngapi?

 Yesu aliambia wanafunzi wake wakuwe wanafanya Meza ya Bwana, lakini hakuwaambia waziwazi wanapaswa kuifanya mara ngapi. (Luka 22:19) Watu fulani wanaona kama wanapaswa kuifanya kila mwezi, wengine kila juma, wengine kila siku, ao mara mingi kwa siku, na wengine wanaona kama wanaweza kuifanya kila wakati kama wanaona kuwa ni lazima. a Lakini, tuone mambo fulani ya kufikiria.

 Yesu alianzisha Meza ya Bwana siku ya Pasaka ya Wayahudi, na ni ileile siku njo alikufaka. (Matayo 26:1, 2) Juu ya nini alianzisha Meza ya Bwana siku ya Pasaka? Biblia inalinganisha zabihu ya Yesu na zabihu ya mwana-kondoo wa Pasaka. (1 Wakorinto 5:7, 8) Pasaka ilikuwa nafanywa mara moya ku mwaka. (Kutoka 12:1-6; Mambo ya Walawi 23:5) Vilevile, Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa nafanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu mara moya ku mwaka. b Ni vile Mashahidi wa Yehova nao wanafanyaka.

Tunapaswa kufanya Meza ya Bwana tarehe gani, na saa gani?

 Tarehe na saa yenye Yesu alifanyaka Ukumbusho njo yenye tunapaswa kufuata. Alianzishaka Ukumbusho tarehe 14, mu mwezi wenye kuitwa Nisani, mwaka wa 33. Ilikuwaka mangaribi kisha jua kushuka. (Matayo 26:18-​20, 26) Kila mwaka tunafanyaka Ukumbusho ile tarehe, sawa vile Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwaka nafanya. c

 Mu mwaka wa 33, tarehe 14 ya mwezi wa Nisani ilikuwaka Siku ya Tano. Lakini kila mwaka ile tarehe haikuwake tu Siku ya Tano. Inaweza kuwa siku ni siku. Kuliko kufuata kalendari ya sasa ya Wayahudi juu ya kujua ikiwa tarehe 14 Nisani itakuwa siku gani, kila mwaka tunatumiaka njia yenye Wayahudi wa wakati wa Yesu walikuwa natumia ili kujua tarehe ya Pasaka. d

Mukate na Divai

 Wakati Yesu alifanya Meza ya Bwana, alitumia mukate wenye hauna chachu na divai nyekundu vyenye vilibakia kisha wao kumaliza kula Pasaka. (Matayo 26:26-​28) Na siye tunatumiaka mukate wenye hauna chachu ao wenye haukuongezewa kitu yoyote, na divai nyekundu yenye haikuongezwa kitu, hapana maji ya matunda ya mizabibu ao divai yenye kuongezwa sukari ao vikolezo fulani.

 Dini za mingi zinatumiaka mukate wenye kuwa na chachu, lakini mara mingi mu Biblia chachu inafananisha zambi na kuharibika. (Luka 12:1; 1 Wakorinto 5:6-8; Wagalatia 5:7-9) Njo maana, mukate wenye hauna chachu na wenye haukuongezwa kitu yoyote njo unastahili kabisa kufananisha mwili wa Yesu wenye hauna zambi. (1 Petro 2:22) Pa nafasi ya divai, dini zingine zinatumikishaka maji ya matunda yenye haikuchachishwa. Ile nayo haipatane na maandiko. Wanafanyaka vile juu wanakatazaka watu kunywa pombe, lakini Biblia haikataze watu kunywa pombe.​—1 Timoteo 5:23.

Mukate na divai ni mifano, haiko mwili na damu ya kweli kweli

 Mukate wenye hauna chachu na divai nyekundu yenye inatumiwaka ku ukumbusho ni mifano tu. Mukate unafananisha mwili wa Kristo na divai inafananisha damu yake. Havibadilikake kwa muujiza na kuwa mwili na damu ya Yesu ao kuchangwa na mwili ao damu ya Yesu sawa vile watu fulani wanawazaka. Ona mawazo ya Biblia yenye inatusaidia kuelewa vile.

  •   Kama Yesu angewaambia wanafunzi wake wakunywe damu yake, ile ingekuwa kuwaambia wavunje sheria ya Mungu yenye inakataza kula damu. (Mwanzo 9:4; Matendo 15:28, 29) Haiwezi kuwa vile, juu Yesu hawezi kuwaambia watu wavunje sheria ya Mungu yenye inahusu utakatifu wa damu.​—Yohana 8:28, 29.

  •   Wakati mitume walikuwa nakunywa divai, Yesu aliwaambia kama damu yake itamwangwa. Ile inaonyesha kama ile divai haikukuwa damu yake.​—Matayo 26:28.

  •   Zabihu ya Yesu ilifanywa “mara moja kwa wakati wote.” (Waebrania 9:25, 26) Lakini, kama mukate na divai vilibadilishwa na kuwa mwili na damu ya Yesu wakati ya Chakula cha Mangaribi cha Bwana, ni kusema wale wenye kutumia mukate na divai wako nafanya ile zabihu tena na tena.

  •   Yesu alisema: “Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi,” hakusema “kwa kunitoa zabihu.”​—1 Wakorinto 11:24

 Wale wenye wanaamini kama mukate na divai vinabadilikaka na kuwa mwili na damu ya Yesu, wanateteaka ile fundisho kwa kutumia maneno ya maandiko fulani ya Biblia. Kwa mufano, maneno yenye Yesu alisema mbele apitishe divai inatafsiriwa hivi mu tafsiri za mingi za Biblia: “Hii ni damu yangu.” (Matayo 26:28) Lakini, ile maneno ya Yesu inaweza pia kutafsiriwa hivi: “Hii inamaanisha damu yangu” ao “Hii inafananisha damu yangu.” e Yesu alizoea kutumia maneno ya mufano, na ni vile alifanya wakati alitumia ile maneno.​—Matayo 13:34, 35.

Nani njo wanapaswa kula mukate na kunywa divai?

 Wakati Mashahidi wa Yehova wanafanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu, ni watu kidogo njo wanakulaka mukate na kunywa divai. Juu ya nini?

 Damu ya Yesu ilisaidia kuanzisha “agano jipya” yenye ilikamata nafasi ya agano yenye Mungu alifanyaka pamoya na taifa ya Israeli. (Waebrania 8:10-​13) Ni wenye kuwa mu ile agano njo wanakulaka mukate na kunywa divai ku Ukumbusho. Haiko Wakristo wote njo wako mu ile agano, lakini wale tu wenye “wameitwa” kwa njia ya pekee na Mungu. (Waebrania 9:15; Luka 22:20) Wale njo watatawala pamoya na Kristo mbinguni, na Biblia inasema kama ni watu 144 000 tu.​—Luka 22:28-​30; Ufunuo 5:9, 10; 14:1, 3.

 Tofauti na ile “kundi ndogo,” ni kusema wale wenye watatawala na Yesu, wengi kati yetu wanafanyiza “kundi kubwa” ya watu wenye wataishi milele ku dunia. (Luka 12:32; Ufunuo 7:9, 10) Wale wenye wako na tumaini ya kuishi ku dunia hawakulake mukate ao kunywa divai ku ukumbusho, lakini wanafikaka ku Ukumbusho juu ya kuonyesha shukrani yao kwa ajili ya mambo yenye Yesu alitufanyia.​—1 Yohana 2:2.

a Tafsiri fulani za Biblia zinatumia maneno “mara mingi” wakati zinazungumuzia Chakula cha Bwana cha Mangaribi. Na ile maneno imetumiwa juu ya kuamua ni mara ngapi njo Ukumbusho wa kifo ya Yesu unapaswa kufanywa. Lakini maana ya kweli ya neno yeye ilitumiwa mu luga ya kwanza-kwanza ni “kila mara” ao “kila wakati.”​—1 Wakorinto 11:25, 26; La Sainte Bible en swahili de la R.D.Congo.

b Ona kitabu The New Schaff-Herzog Encyclopedia of Religious Knowledge, Buku ya IV, ukurasa wa 43-​44, na Cyclopedia ya McClintock na Strong, Buku ya VIII, ukurasa wa 836.

c Ona kitabu The New Cambridge History of the Bible, Buku ya 1, ukurasa wa 841.

d Kalendari ya sasa ya Wayahudi inatumia makadirio ya watu wenye kujifunza nyota juu ya kujua mwezi wa Nisani unaanza wakati gani. Lakini ile haikutumiwa mu karne ya kwanza. Mu ile wakati, Nisani ilikuwa inaanza wakati mwezi mupya ulikuwa unaonekana Yerusalemu, na ile inaweza kuwa siku moya ao mbili kisha tarehe yenye wale wenye kujifunza nyota wanatoa. Ile ni sababu moya yenye inafanya tarehe yenye Mashahidi wa Yehova wanafanya Ukumbusho isikuwe kila mara sawasawa na tarehe yenye Wayahudi wa leo wanafanya Pasaka.

e Ona A New Translation of the Bible, ya James Moffatt; The New Testament—A Translation in the language of the People, ya Charles B. Williams; na The Original New Testament, ya Hugh J. Schonfield.