Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutiwa Damu Mishipani?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutiwa Damu Mishipani?

Jibu la Biblia

 Biblia inatukataza kula damu. Kwa hiyo, hatupaswi kukubali damu ao sehemu zake katika hali yoyote, hatuitumie kama chakula wala kuingiza mishipani. Fikiria maandiko haya:

  •   Mwanzo 9:4. Mungu alimuruhusu Noa na familia yake kula nyama kisha Garika lakini alimukataza kula damu. Mungu alimuambia Noa hivi: ‘Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi yake—damu yake—musile.’ Amri hii inawahusu wanadamu wote kuanzia wakati huo kwa sababu wote ni wazao wa Noa.

  •   Mambo ya Walawi 17:14. ‘Hamutakula damu ya mwili wa namna yoyote, kwa sababu nafsi ya kila mwili wa namna yoyote iko katika damu yake. Mutu yeyote atakayeila atakatiliwa mbali.’ Mungu aliona kwamba nafsi, ao uzima, uko katika damu na uzima huo ni mali yake. Hata ikiwa sheria hiyo ilitolewa kwa taifa la Israeli, inaonyesha maoni ya Mungu kuhusu kula damu.

  •   Matendo 15:20. ‘Mujiepushe . . . na damu.’ Mungu aliwatolea Wakristo sheria hiyohiyo ambayo alikuwa amemutolea Noa. Historia inaonyesha kwamba Wakristo wa kwanza-kwanza walikataa kula damu na hata hawakuitumia kama dawa.

Sababu gani Mungu anatuamuru tujiepushe na damu?

 Kuna sababu za kiganga zinazoonyesha kwamba kutia damu mishipani ni hatari kwa afya yetu. Lakini, jambo la maana ni kwamba, Mungu anatuamuru tujiepushe kwa sababu damu ni takatifu kwake.—Mambo ya Walawi 17:11; Wakolosai 1:20.