Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 2

Sababu Gani Ninajihangaisha Sana Juu ya Sura Yangu?

Sababu Gani Ninajihangaisha Sana Juu ya Sura Yangu?

SABABU GANI ULIZO HILO NI LA MAANA

Kuna mambo ya maana zaidi kuliko jambo lenye unaona katika kioo.

UNGEFANYA NINI?

Wazia jambo hili: Wakati Julia anajiangalia katika kioo, anaona kuwa ananenepa sana. Hata kama wazazi na marafiki wake wanamuambia kama iko “mwembamba sana,” yeye anajiambia hivi: “Ninapaswa kupunguza kilo fulani.”

Hivi karibuni, Julia alikuwa ameamua kujitesa sana ili kupunguza “hata kilo mbili.” Jambo lenye aliamua kufanya ni kujiima chakula kwa siku fulani . . .

Kama ungekuwa Julia, ungefanya nini?

WAZA KIDOGO!

Mambo yenye unawaza juu ya sura yako yanaweza kuwa kama kujiangalia katika kioo chenye kuharibisha sura

Haiko mubaya kujihangaisha juu ya sura yako. Kwa kweli, Biblia inatapa watu wenye walikuwa na sura ya muzuri sana, ikuwe wanaume ao wanawake, kama vile Sara, Raheli, Abigaili, Yosefu, na Daudi. Biblia inasema kama ule mwanamuke mwenye aliitwa Abishagi alikuwa ‘murembo zaidi.’—1 Wafalme 1:4.

Lakini, vijana wengi wanajihangaisha sana juu ya sura yao. Jambo hilo linaweza kuleta magumu sana. Fikiria mambo yenye kufuata:

  • Kulingana na uchunguzi moja, wanawake 58 juu ya 100, waliwaza kwamba walikuwa na kilo sana. Lakini, kwa kweli ni wanawake 17 tu juu ya 100 ndio walikuwa na kilo sana.

  • Katika uchunguzi mwengine, wanawake 45 juu ya 100 waliwaza kama walikuwa na kilo sana. Lakini, kwa kweli walikuwa na kilo ya chini sana!

  • Wakati walikuwa wanatafuta kupunguza kilo zao, vijana fulani walifikia kupata anoreksia, ni kusema, ugonjwa wenye kutokea kwa sababu ya mutu kujiima chakula.

Kama unaonyesha alama fulani za anoreksia ao tatizo lingine lenye linatokea kwa sababu ya kukosa kula muzuri, tafuta musaada. Kwanza, umuambie muzazi wako ao mutu mukubwa mwenye unatumainia. Biblia inasema hivi: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.”—Methali 17:17.

MABADILIKO YA MUZURI YENYE UNAWEZA KUFANYA!

Kusema kweli, ni tabia za mutu zinafanya avutie wengine ao hapana. Fikiria Absalomu, mutoto wa Mufalme Daudi. Biblia inasema hivi:

‘Hakuna mwanaume aliyekuwa na sura nzuri sana katika Israeli yote kuweza kusifiwa sana hivyo. Hakuwa na kasoro yoyote.’​—2 Samweli 14:25.

Lakini, kijana huyo mwanaume alikuwa na kiburi sana, alikuwa mwenye kutafuta mambo makubwa, na mudanganyifu! Biblia haimutape Absalomu, lakini, inamutaja kuwa mutu mwenye kukosa uaminifu sana na mwenye chuki ya kuua.

Ndiyo sababu Biblia inatutolea shauri hili:

‘Mujivike utu mupya.’—Wakolosai 3:10.

Kujipamba kwenu kusikuwe kwa inje . . . , bali [ao, lakini] kukuwe yule mutu wa siri wa moyoni.’—1 Petro 3:3, 4.

Hata kama haiko mubaya kutaka kuwa na sura yenye kupendeza, jambo la maana zaidi ni tabia zako. Kisha wakati fulani, utatambua kwamba sifa za muzuri zinavutia zaidi kuliko mwili muzuri ao sura yenye kupendeza! Kijana mumoja mwanamuke mwenye kuitwa Phylicia, anasema hivi: “Sura yenye kupendeza inaweza kuvutia wengine haraka, lakini watu wanakumbuka zaidi sana tabia zako za muzuri.”

CHUNGUZA NAMNA UNAONEKANA

Mara nyingi unahuzunika kwa sababu ya sura yako?

Umekwisha kufikiria kuuza mafuta fulani ya kugeuza ngozi ya mwili wako ao kufuata programu fulani ya kula chakula ili kubadilisha mwili wako?

Kama ungekuwa na uwezo, ungebadilisha nini kwenye mwili wako? (Tia kiviringo kwenye kila jibu lako.)

  • UREFU

  • KILO

  • NYWELE

  • UMBO LA MWILI

  • SURA

  • RANGI YA NGOZI

Kama umejibu ndiyo kwa maulizo mbili ya kwanza ao kutia kiviringo kwenye mambo tatu ao zaidi kwa ulizo la tatu, fikiria jambo hili: Inawezekana watu wengine hawachukie sura yako kama vile wewe unaichukia. Ni mwepesi kuvuka mipaka na kujihangaisha sana juu ya sura yako.—1 Samweli 16: 7.