Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inaweza Kukusaidia Uache Kuwa Mutumwa wa Dawa za Kulewesha?

Biblia Inaweza Kukusaidia Uache Kuwa Mutumwa wa Dawa za Kulewesha?

 Kila mwaka, watu wengi wanakufa juu ya matokeo ya moja kwa moja ao yenye haiko ya moja kwa moja ya kutumia mubaya dawa fulani, kutia ndani dawa za kulewesha. Na mu hii kipindi ya coronavirus, ile shida imeongezeka sana. Hekima yenye kuwa mu Biblia imesaidia watu wengi waache kuwa watumwa wa dawa za kulewesha. Kama uko napambana na ile tatizo, hekima ya Biblia inaweza kukusaidia pia. a

Mu hii habari

 Juu ya nini utafute mashauri ya Biblia juu ikusaidie uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha?

 Watu wenye kutafuta-tafuta habari wamevumbula kama, mara mingi, watu wengi wamekuwa watumwa wa dawa za kulewesha kwa sababu ya mambo kama vile hali ya mutu kujisikia kuwa peke yake, mahangaiko ya akili, na kushuka moyo. Lakini, Biblia inaweza kukusaidia ukuwe na imani yenye itakupatia nguvu ya kupambana na magumu yenye inaweza kufanya mutu akuwe mutumwa wa dawa za kulewesha. Biblia inaonyesha pia namna unaweza kuwa na urafiki wa karibu sana pamoya na Mungu. (Zaburi 25:14) Na Mungu anaweza kukusaidia upiganishe magumu yenye unaona ni nguvu kwako kupambana nayo weye mwenyewe.​—Marko 11:22-24.

 Mambo ine yenye Biblia inakuomba ufanye juu uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha

  1.  1. Ujifunze kumujua Yehova Mungu. b (Yohana 17:3) Yeye njo Muumbaji, na nguvu yake haina mipaka. Zaidi ya ile, ni Baba yako wa mbinguni mwenye upendo. Anapenda ukuwe rafiki yake, na anapenda kutumikisha nguvu yake juu ya kukusaidia. (Isaya 40:29-31; Yakobo 4:8) Atakupatia wakati wenye kuya wa muzuri kama unakubali kuwa rafiki yake.​—Yeremia 29:11; Yohana 3:16.

  2.  2. Umuombe Yehova akusaidie. Sali kwa Mungu, umuombe akusaidie uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha juu ukuwe ‘takatifu [ao, safi] na mwenye kukubalika’ kwake. (Waroma 12:1) Kupitia roho yake takatifu, ao nguvu yake ya utendaji, atakupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Wakorinto 4:7; Luka 11:13) Ile nguvu itakusaidia uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha na uvae “utu mupya” wenye unamufurahisha.​—Wakolosai 3:9, 10.

  3.  3. Ujaze akili yako na mawazo ya Mungu. (Isaya 55:9) Atakusaidia ‘ufanywe upya katika mutazamo wenye unatawala akili” yako ao ubadilishe namna yako ya kuwaza; ile itakusaidia uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha. (Waefeso 4:23) Mawazo ya Mungu iko mu Biblia, njo maana ni jambo ya lazima kuisoma kwa ukawaida. (Zaburi 1:1-3) Watu wengi wanapata faida kabisa wakati mutu fulani anawasaidia kuelewa mafundisho ya Biblia. (Matendo 8:30, 31) Mashahidi wa Yehova watafurahi kujifunza Biblia pamoya na weye bila kulipa. Tunakualika pia ufike ku mikutano yetu; kule tunajifunza namna ya kutumia mafundisho ya Biblia mu maisha yetu.

  4.  4. Uchague marafiki wazuri. Marafiki wanaweza kukusaidia uendelee ao uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha. (Mezali 13:20) Mungu anatupatia marafiki wazuri kati ya waabudu wake, na anapenda ufurahie urafiki wao. (Zaburi 119:63; Waroma 1:12) Uchague kwa uangalifu mambo ya kujifurahisha, sababu mambo yenye unaona, yenye unasikia, na yenye unasoma, inaweza kukuchochea sawa tu vile marafiki. Epuka kila kitu yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kwako kufanya mambo ya muzuri.​—Zaburi 101:3; Amosi 5:14.

 Maandiko ya Biblia yenye inaweza kukusaidia uache kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha

 Zaburi 27:10: “Hata kama baba yangu na mama yangu wananiacha, Yehova mwenyewe atanikaribisha.”

 “Sijue baba yangu, na ile inanifanyaka nijisikie sawa nina kosa kitu fulani. Wakati tu nilifikia kujua kama Yehova Mungu iko kabisa na ananipenda, nilipata kusudi mu maisha na niliweza kuacha kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha.”​—Wilby, wa inchi ya Haiti.

 Zaburi 50:15: “Uniitie wakati wa taabu. Nitakuokoa.”

 “Hii andiko inanipatiaka nguvu ya kuendelea kujikaza kuacha kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha hata wakati ninaangukia tena mu ile tabia. Yehova anatimizaka ahadi yake.”​—Serhiy, wa inchi ya Ukraine.

 Mezali 3:5, 6: “Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote, na usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue katika njia zako zote, Naye atanyoosha mapito yako.”

 “Hii andiko imenisaidia nisijitegemee, lakini nimutegemee njo Yehova. Kupitia nguvu yake, niliweza kubadilika kabisa.”​—Michele, wa inchi ya Italia.

 Isaya 41:10: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia, Nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.”

 “Nilihangaika sana wakati sikutumia tena dawa za kulewesha. Hii andiko ilinihakikishia kama Mungu atanisaidia niache kuhangaika, na alifanya vile.”​—Andy, wa inchi ya Afrika ya Kusini.

 1 Wakorinto 15:33: “Musidanganywe. Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.”

 “Marafiki wabaya njo walinifundisha kutumia dawa za kulewesha na kunifanya nikuwe mutumwa wa zile dawa. Niliweza kuachana na dawa za kulewesha wakati tu niliachana na marafiki wabaya, na kuunga urafiki na watu wazuri wenye kuishi namna ninapendaka.”​—Isaac, wa inchi ya Kenya.

 2 Wakorinto 7:1: “Tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho.”

 “Hii maneno ilinisaidia niendelee kujisafisha kimwili na kuacha kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha na mambo ingine yenye inaweza kuharibu afya yangu.”​—Rosa, wa inchi ya Colombia.

 Wafilipi 4:13: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”

 “Nilijua kama kwa nguvu yangu sitaweza kuacha kutumia dawa za kulewesha, kwa hiyo niliomba Mungu anisaidie. Alinipatia nguvu yenye nilikuwa nayo lazima.”​—Patrizia, wa inchi ya Italia.

 Mifano ya watu: Biblia iliwasaidia waache kuwa watumwa wa dawa za kulewesha

 Joseph Ehrenbogen alikomalia fasi kwenye kulikuwa jeuri na akakuwa mutumwa wa pombe, tumbako, marijuana na héroïne. Juu alikuwa napitisha mipaka sana, mara mingi alikuwa anaona kifo na macho yake. Andiko moya ya Biblia ilimuhakikishia kama anaweza kubadilika. Soma historia yake mu habari “Nilijifunza Kujiheshimia na Kuheshimia Wanawake.”

 Dmitry Korshunov alijikaza mara mingi kuacha kuwa mutumwa wa pombe. Angalia video ‘Maisha Yangu Yalinichokesha’ juu uone nini njo ilimusaidia.

 Biblia inakataza mutu apate matunzo yenye itamusaidia aachane na dawa za kulewesha?

 Hapana. Biblia inasema hivi: “Watu wenye afya ya muzuri hawana lazima ya munganga, lakini wagonjwa ndio wako na lazima yake.” (Matayo 9:12) Vilevile, shirika moya ya Amerika yenye kuangalia mambo ya dawa za kulewesha inasema hivi: “Kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha ni ugonjwa kabisa, na inaomba kufanya mambo mingi zaidi ya kupenda tu kuacha kutumia dawa za kulewesha juu mutu apone.” Ni kweli, namna Mungu atatusaidia inapita namna tunaweza kujikaza siye wenyewe. Lakini, watu wengi wenye walifuata shauri ya Biblia na kuacha kuwa watumwa wa dawa za kulewesha walikuwa pia na lazima ya matunzo fulani. c Kwa mufano, Allen anasema: “Wakati nilikuwa naacha pombe nilikuwa nasikia maumivu mingi mu mwili, nilielewa kama, nilikuwa na lazima ya matunzo fulani zaidi ya musaada wa kiroho wenye nilipata.”

 Biblia inakataza kutumia dawa za kulewesha kwa ajili ya matunzo?

 Hapana. Biblia inazungumuzia matumizi ya pombe juu ya kutunza ugonjwa fulani ao juu ya kutuliza maumivu yenye inaweza kuuwa mutu. (Mezali 31:6; 1 Timoteo 5:23) Kwa hiyo, kama vile inakuwaka juu ya pombe, dawa za kulewesha zenye zinatumiwa juu ya kupunguza maumivu zinaweza kufanya mutu akuwe mutumwa. Hata vile, ni jambo ya hekima kujua hatari yenye inaweza kutokea wakati uko natumikisha dawa za kusaidia kuzuia maumivu.​—Mezali 22:3.

a Hata kama hii habari inazungumuzia sana namna ya kuacha kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha, kanuni zenye kuwa ndani zinaweza pia kusaidia wale wenye wako wanapambana na magumu ingine sawa vile kuacha kuwa mutumwa wa pombe, tumbako, chakula, michezo ya makuta, pornografia, na site za Enternete za kupashana habari (réseau sociaux).

b Yehova njo jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Soma habari “Yehova Ni Nani?

c Hopitale mingi na programu fulani zinapatiaka watu matunzo juu ya kuwasaidia waache kuwa watumwa wa dawa za kulewesha. Lakini kila mutu anapaswa kujichagulia aina ya matunzo yenye anapenda.​—Mezali 14:15.