Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuko Siku Ugaidi (Terrorisme) Itaisha?

Kuko Siku Ugaidi (Terrorisme) Itaisha?

 Kisha shambulio ya ugaidi, kwa kawaida unaweza kujiuliza: ‘Mungu anatuhangaikiaka? Juu ya nini hii mambo inatokea? Kuko siku ugaidi a itaisha? Namna gani nitaishi na woga yenye niko nayo?’ Biblia inatoa majibu yenye tunaweza kutosheka nayo.

Namna gani Mungu anaona ugaidi?

 Mungu anachukia jeuri na ugaidi. (Zaburi 11:5; Mezali 6:16, 17) Na Yesu, mwenye kumuwakilisha Mungu, alikaripia mitume wake wakati walitenda kwa jeuri. (Matayo 26:50-52) Hata kama watu fulani wanasema kama wanafanya jeuri kwa jina ya Mungu, Mungu hakubali matendo yao. Kwa kweli, hasikilize sala zao.—Isaya 1:15.

 Mungu anahangaikia wote wenye kuteseka, kutia ndani wale wenye wameguswa na mashambulio ya ugaidi. (Zaburi 31:7; 1 Petro 5:7) Biblia inaonyesha tena kama Mungu atamaliza jeuri.​—Isaya 60:18.

Sababu kubwa ya ugaidi

 Biblia inafunua sababu kubwa ya ugaidi: “Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Mu historia yote, watu wenye mamlaka wametumia matendo ya kuogopesha ili kutesa wengine. Wengine wanatumia ugaidi ili kulipisha kisasi.​—Muhubiri 7:7.

Mwisho ya ugaidi

 Mungu ameahidi kutosha woga na jeuri, na kuleta amani mu dunia. (Isaya 32:18; Mika 4:3, 4) Atatosha:

  •   Mambo yenye inaletaka ugaidi. Serikali ya Mungu itachukua nafasi ya utawala wa mwanadamu. Mutawala wa serikali ya Mungu, Yesu Kristo, atatendea kila mutu kwa haki, na atatosha mateso na jeuri. (Zaburi 72:2, 14) Kwa ile wakati, hakuna mwenye atafanya ugaidi. Watu “watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:10, 11.

  •   Matokeo yote ya ugaidi. Mungu atatosha matokeo yote ya ugaidi, ikuwe ya kimwili ao ya kiakili. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:3, 4) Ameahidi hata kama atafufua wafu, kuwarudishia uzima mu dunia yenye amani.​—Yohana 5:28, 29.

 Biblia inatupatia sababu za muzuri za kuamini kama karibuni Mungu atatenda. Lakini, unaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini Mungu hayamaliza ugaidi?’ Juu upate jibu, angalia video Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso?

a “Ugaidi” mara mingi inamaanisha kutumia jeuri ili kuogopesha watu, zaidi sana watu wenye hawako maaskari. Kuwaogopesha juu ya kufikia miradi ya politike, ya dini na ingine. Lakini, inawezekana watu wasikubaliane kama kitendo fulani ni ugaidi.