Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini?

Yesu aliambia wanafunzi wake waombe Ufalme ukuje. Alijua kama mambo ya mubaya yenye kufanyika ku dunia haiko mambo yenye Mungu anapenda na kama Ufalme wa Mungu tu njo serikali yenye inaweza kumaliza ile magumu. Ufalme wa Mungu utafanya nini?

MAMBO YENYE UFALME WA MUNGU UMEKWISHA KUFANYA

Katika habari yenye kutangulia, tulizungumuzia alama yenye Yesu alitoa. Ile alama inahakikisha wazi kama Ufalme wa Mungu umesimamishwa mbinguni na kama Yesu Kristo njo Mufalme wa Ufalme huo.

Biblia inasema kama wakati Yesu alichukua mamlaka, alifukuza Shetani na pepo wake wachafu kutoka mbinguni. Sasa, ni ku dunia tu njo wako na uwezo wa kufanya mambo fulani, na ile ni kati ya sababu zenye zimefanya mambo ikuwe mubaya zaidi tangu mwaka wa 1914.​—Ufunuo 12:7, 9.

Hata kama hali za ulimwengu zinaendelea kuharibika, Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu, amefanya mambo mbalimbali ili kusaidia watu ku dunia. Kupitia kazi ya kufundisha watu Biblia mu dunia yote yenye Yesu alitabiri, watu wengi wako wanajifunza na kutumia kanuni za Biblia katika maisha yao ya kila siku. (Isaya 2:2-4) Mamilioni ya watu wamejifunza namna ya kuwa na maisha yenye furaha zaidi na kuepuka kufanya kazi ao vitu vya kimwili kuwa mambo ya maana sana katika maisha yao. Hawa watu wako wanajifunza namna ya kujipatia faida wao wenyewe na kufikia kuwa aina ya watu wenye Mungu anapenda wakuwe raia wa Ufalme wake.

UFALME WA MUNGU UTAFANYA NINI WAKATI WENYE KUJA?

Hata kama tayari Yesu iko anatawala mbinguni, serikali za wanadamu zingali zinatawala ku dunia. Lakini, Mungu amemuambia Yesu: “Uende utawale katikati ya maadui wako.” (Zaburi 110:2) Hivi karibuni, Yesu ataharibu kabisa wapinzani wote na kuletea kitulizo wale wote wenye wako tayari kumutii Mungu.

Ile wakati, Ufalme wa Mungu utachukua hatua ili

  • Kuharibu dini za uongo. Dini zenye zimefundisha uongo kumuhusu Mungu na zenye zimefanya maisha ya watu kuwa nguvu zitaharibiwa. Biblia inalinganisha dini za uongo na kahaba. Watu wengi watashangaa sana wakati dini hizo zitaharibiwa.​—Ufunuo 17:15, 16.

  • Kumaliza serikali za wanadamu. Ufalme wa Mungu utachukua hatua ili kumaliza serikali zote za wanadamu.​—Ufunuo 19:15, 17, 18.

  • Kutosha watu wabaya. Tuseme nini kuhusu wale wenye wameazimia kufanya mambo ya mubaya na wenye wanakataa kumutii Mungu? “Lakini waovu, wataondolewa katika dunia.”​—Mezali 2:22.

  • Kumuangamiza Shetani na pepo wachafu. Shetani na pepo wachafu hawatakuwa na uwezo wa ‘kupotosha mataifa tena.’​—Ufunuo 20:3, 10.

Ile yote itamaanisha nini kwa wale wenye wanaunga mukono Ufalme wa Mungu?

MAMBO YENYE UFALME WA MUNGU UTAFANYIA WANADAMU

Wakati atatawala akiwa Mufalme mbinguni, Yesu atatimiza mambo mingi sana kupita mambo yenye mutawala yeyote mwanadamu angeweza kutimiza. Atatawala pamoja na watu 144000, wenye walichaguliwa kutoka kati ya wanadamu. (Ufunuo 5:9, 10; 14:1, 3) Atahakikisha kama mapenzi ya Mungu imefanywa hapa ku dunia. Ufalme wa Mungu utafanyia nini wakaaji wa dunia?

  • Utamaliza magonjwa na kifo. “Hakuna mukaaji mwenye atasema: “Niko mugonjwa” na “kifo hakitakuwa tena.”​—Isaya 33:24; Ufunuo 21:4.

  • Utaleta amani na usalama wa kweli. “Amani ya wana wako itakuwa nyingi,” na “watakaa, kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini, na hakuna mutu mwenye atawaogopesha.”​—Isaya 54:13; Mika 4:4.

  • Utapatia wanadamu kazi ya muzuri sana. “Wachaguliwa wangu watafurahia kwa ukamili kazi ya mikono yao. Hawatafanya kazi ya jasho ya bure.”​—Isaya 65:22, 23.

  • Utamaliza matatizo ya mazingira. “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—Isaya 35:1.

  • Utafundisha watu kile wanapaswa kufanya ili waishi milele. “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.”​—Yohana 17:3.

Mungu anapenda ufurahie zile baraka zote. (Isaya 48:18) Habari yenye kufuata itazungumuzia mambo yenye unaweza kufanya sasa ili uweze kufurahia zile baraka wakati wenye kuja.