Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ufalme wa Mungu Utatawala Dunia Wakati Gani?

Ufalme wa Mungu Utatawala Dunia Wakati Gani?

Wamoja kati ya wafuasi waaminifu wa Yesu walipenda kujua wakati wenye Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala. Yesu alijibia ulizo lao kwa kusema kama hawangejua kabisa wakati wenye ule Ufalme ungeanza kutawala dunia. (Matendo 1:6, 7) Lakini, mbele kidogo, aliwaambia kama wakati wanafunzi wake wangeona matukio fulani ikifanyika kwa wakati mumoja, ‘wangejua kwamba Ufalme wa Mungu ulikuwa karibu’ na kwamba wakati wa ule Ufalme kutawala ulimwengu umefika.​—Luka 21:31.

NI MATUKIO GANI YENYE YESU ALISEMA KAMA INGETOKEA?

Yesu alisema: “Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme. Kutakuwa matetemeko makubwa ya inchi, na mahali pamoja kisha pengine kutakuwa upungufu wa chakula na magonjwa ya kuambukiza.” (Luka 21:10, 11) Wakati ile matukio yote ingefanyika kwa wakati mumoja, ile ingeonyesha wazi kwamba “Ufalme wa Mungu unakaribia.” Ile matukio imekwisha kuonekana kwa wakati mumoja na mu dunia yote? Fikiria ushuhuda fulani.

1. VITA

Katika mwaka wa 1914, kulitokea vita yenye ilikuwa na matokeo ya mubaya kwa watu wengi sana na katika maeneo mingi kuliko zamani! Mara mingi, wanahistoria wanasema kama mwaka wa 1914 ni mwaka wa mabadiliko katika historia kwa sababu njo wakati wenye vita ya kwanza ya ulimwengu ilianza. Ni mu ile vita njo silaha hatari kama vile magari ya vita, mabombe yenye kutupwa mu hewa, bunduki zenye kumwanga masasi kwa uwingi, gaze zenye kuwa na sumu, na silaha zingine zenye kuua zilitumiwa sana kwa mara ya kwanza. Ilifuatwa na vita ya pili ya ulimwengu yenye ilianzisha matumizi ya silaha za atomu. Kuanzia mwaka wa 1914, vita vimekuwa vikitokea katika maeneo mbalimbali ya dunia, na vimeua mamilioni ya watu.

2. MATETEMEKO YA INCHI

Kitabu Britannica Academic kinasema kama kila mwaka kunakuwa matetemeko ya inchi karibu 100 yenye kuleta “uharibifu mukubwa.” Shirika la Marekani la Uchunguzi wa Jiolojia (USGS) linasema kama “kulingana na habari yenye imechungwa kwa muda murefu (kuanzia mwaka wa 1900 hivi), tunatazamia kuwa kutatokea matetemeko makubwa ya inchi karibu 16 kila mwaka.” Hata kama watu fulani wanaweza kuwaza kama hakuna matetemeko mingi ya dunia, na kusema kama inaonekana kuwa mingi juu tu wanadamu wamekuwa na njia mbalimbali za kuivumbua, ukweli ni kwambamatetemeko makubwa ya inchi iko inafanya watu wengi wateseke na kufa kuliko zamani.

3. UPUNGUFU WA CHAKULA

Mara mingi upungufu wa chakula unatokana na vita, rushwa, matatizo ya kupata feza, ao kuharibika kwa mimea. Ripoti ya Shirika la Chakula Ulimwenguni ya 2018 inasema kama: “Katika ulimwengu, watu milioni 821 wako na njaa, na watu millioni 124 wako na njaa sana.” Kula mubaya kumechangia vifo vya watoto karibu milioni 3,1 kila mwaka. Katika mwaka wa 2011, ile ilifanya karibu asilimia 45 (45%) ya watoto katika ulimwengu wote wakufe.

4. MAGONJWA NA MAGONJWA YENYE KUENEA SANA

Kichapo kimoja cha Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) kinasema hivi: “Kipindi cha kuanzia mwaka wa 2001 mupaka leo kimejulikana kuwa kipindi cha magonjwa makubwa yenye kuenea sana. Magonjwa ya zamani, kama vile kolera, homa ya manjano (fièvre jaune) na magonjwa ingine ya kuambukiza imerudia; pia magonjwa ya mupya imetokea, kama vile mafua ya ndege (SARS), homa yenye kuenea, MERS (aina ya ugonjwa wenye unafanya mutu apatwe na homa, kikohozi, na apumue kwa shida), Ebola na Zika.” Hata kama wanganga na wanasayansi wamejifunza mambo mingi kuhusu magonjwa, hawajawezaka kupata dawa ya kuponyesha magonjwa yote.

5. KAZI YA KUHUBIRI MU DUNIA YOTE

Yesu alizungumuzia sehemu ingine ya ile alama wakati alisema hivi: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.” (Matayo 24:14) Katika ulimwengu huu wenye kuwa na matatizo makubwa, watu zaidi ya milioni munane kutoka katika mataifa yote wako wanatangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu katika inchi 240 na wanahubiri katika luga zaidi ya 1000. Ile haijafanyikaka katika historia yote ya wanadamu.

ILE ALAMA IKO NA MAANA GANI KWETU?

Ni wazi kuwa matukio yenye kufanyiza alama yenye Yesu alitoa iko inaonekana leo. Juu ya nini tunapaswa kufurahishwa na jambo hilo? Ni juu Yesu alisema: “Wakati mutaona mambo hayo yanatokea, mujue kwamba Ufalme wa Mungu unakaribia.”​—Luka 21:31.

Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utahakikisha kama mapenzi ya Mungu imefanyika ku dunia

Kuonekana kwa alama yenye Yesu alitoa, pamoja na namna matukio ya Biblia inafuatana, vinatusaidia kuelewa kwamba Mungu alisimamisha Ufalme wake mbinguni katika mwaka wa 1914. a Wakati huo, alimufanya Mutoto wake, Yesu Kristo, kuwa Mufalme. (Zaburi 2:2, 4, 6-9) Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utatawala dunia, na utaondoa falme zote zenye kuupinga na utafanya dunia kuwa paradiso ili wanadamu waishi ndani milele.

Hivi karibuni, maneno hii ya sala ya mufano yenye Yesu alifundisha itatimia: “Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.” (Matayo 6:10) Lakini, Ufalme huo umekuwa ukifanya nini tangu uanze kutawala katika mwaka wa 1914? Na ni mambo gani yenye tunaweza kutazamia wakati Ufalme huo utatawala wanadamu wote?

a Ili kupata habari zaidi kuhusu mwaka wa 1914, ona Maelezo Ingine ya 22, ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova.