Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Zaidi ya mambo yenye Biblia inasema, kuko ushuhuda mwingine wenye unaonyesha kama Waisraeli walikuwa watumwa kule Misri?

Biblia inaonyesha kama kisha Wamidiani kumupeleka Yosefu kule Misri, Yakobo, muzee wa ukoo, na familia yake walitoka Kanaani na kuhamia Misri. Waliishi katika eneo la Misri lenye kuitwa Gosheni, katika Delta ya Muto Nile, ni kusema, eneo kwenye Muto Nile umejigawanya katika mito midogo. (Mwa. 47:1, 6) Waisraeli ‘waliendelea kuongezeka na kuwa wenye nguvu zaidi.’ Kwa hiyo, Wamisri walianza kuogopa sana Waisraeli na waliwalazimisha kuwa watumwa.​—Kut. 1:7-14.

Wachambuzi fulani wa Biblia wa siku zetu wamechekelea ile habari ya Biblia, wanasema kama ni habari ya kuwazia tu. Lakini, kuko ushuhuda wenye unaonyesha kama Washemu * walikuwa watumwa katika Misri ya zamani.

Kwa mufano, watu wenye kuchimbua vitu vya zamani wamepata mabaki ya makao ya zamani katika sehemu ya kaskazini ya Misri. John Bimson, mutu mwenye elimu ya Biblia, anasema kama kuko makao ya Washemu 20 ao zaidi katika eneo hilo la kaskazini mwa Misri. Zaidi ya hiyo, James Hoffmeier, mutu mwenye elimu ya mambo yenye kuhusu Misri ya zamani, anasema hivi: “Kuanzia mwaka wa 1800 mupaka 1540 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Washemu kutoka Asia mangaribi waliona inchi ya Misri kuwa nafasi ya muzuri ya kuhamia.” Anaongeza hivi: “Kipindi hicho cha wakati kinapatana na ‘Kipindi cha Wazee wa Ukoo’ na kwa hiyo, kinapatana na kipindi na hali zenye kitabu cha Mwanzo kinazungumuzia.”

Kuko ushuhuda mwingine kutoka sehemu ya kusini ya Misri. Kipande kimoja cha mafunjo (papyrus) cha wakati wa Ufalme wa Katikati (karibu mwaka wa 2000–karibu mwaka wa 1600 M.K.Y.) kiko na majina ya watumwa wenye walitumikia familia moja katika sehemu ya kusini ya Misri. Majina zaidi ya 40 kati ya ile majina ni ya Washemu. Watumwa hao, ao watumishi, walifanya kazi ya kupika chakula, kusuka, na kazi zingine za nguvu. Hoffmeier anasema hivi: “Kwa sababu kwa miaka zaidi ya makumi ine Washemu walitumikia familia moja tu katika Thébaïde [kusini mwa Misri], inaonekana kama hesabu yao ilikuwa kubwa sana, zaidi sana katika Delta ya Muto Nile.”

David Rohl, mutu mwenye kuchimbua vitu vya zamani, aliandika kama majina fulani ya watumwa hao “inafanana kabisa majina yenye kupatikana mu Biblia.” Kwa mufano, kipande hicho cha mafunjo kiko na majina yenye kufanana majina sawa vile Isakari, Asheri, na Shifra. (Kut. 1:3, 4, 15) Rohl anamalizia kwa kusema hivi: “Huu ni ushuhuda wa kweli wenye kuonyesha kama Waisraeli walikuwa watumwa kule Misri.”

Bimson, mutu mwenye elimu ya Biblia, anasema hivi: “Historia inahakikisha kabisa habari ya Biblia yenye kuzungumuzia utumwa wa Waisraeli kule Misri na namna walitoka Misri.”

^ fu. 4 Jina Washemu linatokana na Shemu, mumoja wa wana watatu wa Noa. Inaonekana kuwa wazao wa Shemu walitia ndani Waelamu, Waashuru, Wakaldayo wa zamani, Waebrania, Wasiria, na makabila mbalimbali ya Waarabu.