Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA

Ponografia—Ina Hatari ao Haina Hatari Yoyote?

Ponografia—Ina Hatari ao Haina Hatari Yoyote?

Leo, dunia inajaa mambo ya ponografia. * Mambo ya ponografia yanaweza kupatikana katika matangazo, mitindo, sinema, miziki, na magazeti, pia kwenye televisheni, michezo ya video, simu ao telefone za hali ya juu, mashini zingine za mukononi za kiteknolojia ambazo zinatumiwa siku hizi, adresi za Internete, na sehemu zingine za Internete ambazo zinawezesha watu kutumiana picha. Ponografia inaonekana kuwa imekubaliwa na watu wengi katika sehemu nyingi za dunia. Leo, katika maeneo mengi duniani, watu wengi zaidi wanatazama ponografia sana kuliko wakati mwengine wowote katika historia ya wanadamu.—Soma kisanduku  “Maelezo Mafupi juu ya Ponografia.”

Aina ya ponografia pia inaendelea kubadilika. Profesa Gail Dines aliandika hivi: “Leo, picha zimekuwa chafu sana hivi kwamba ponografia ambayo ilionekana kuwa mbaya sana wakati uliopita imeanza sasa kuonekana kuwa ponografia ya kawaida.”

Una maoni gani juu ya kuenea kwa ponografia na namna watu wanavyoiona? Je, ponografia ni jambo la kujifurahisha lisilokuwa na hatari, ao ni sumu yenye kuangamiza? Yesu alisema hivi: ‘Kila muti muzuri unazaa matunda mazuri, lakini kila muti uliooza unazaa matunda yasiyofaa.’ (Mathayo 7:17) Ponografia inazaa matunda gani? Ili kupata jibu, acheni tuzungumuzie maulizo fulani ya lazima juu ya ponografia.

Ponografia ina matokeo gani juu ya watu?

MAMBO AMBAYO WACHUNGUZI WANASEMA: Ponografia inafanya watu wawe watumwa wayo, wachunguzi fulani na watu waliosoma sana mambo ya matunzo wanalinganisha hata ponografia na dawa kali ya kulewesha inayoitwa kokaini.

Brian, * ambaye alizoea sana kutazama ponografia kwenye Internete, anasema hivi: “Hakuna kitu chochote ambacho kingenizuia. Nilikuwa ninajisikia sawa vile nilikuwa katika maono. Nilikuwa ninatetemeka na kusikia maumivu ya kichwa. Nilijikaza sana ili kuacha kutazama ponografia, lakini kisha miaka mingi nilikuwa bado na tabia hiyo.”

Watu ambao wanazoea kutazama ponografia mara nyingi wanaficha tabia yao mbaya. Wanaitazama kwa siri na ni wadanganyifu. Si jambo lenye kushangaza kwamba wengi kati yao wanajisikia kuwa wenye kujitenga, wenye haya, wenye wasiwasi, wenye kushuka moyo, na wenye hasira. Katika hali fulani, wengine hata wanatafuta kujiua. Serge, anayechukua mambo ya ponografia kwenye Internete kupitia simu ao telefone yake anasema, “Nilianza kuwa mwenye kujitenga na wengine na mwenye kuvunjika moyo. Nilijisikia kuwa mutu asiyefaa kitu, mwenye hatia, nikiwa peke yangu, na mwenye kunaswa katika mutego. Nilijisikia kuwa mwenye haya sana na niliogopa kuomba musaada.”

Hata kuona tu kidogo mambo ya ponografia bila kukusudia kunaweza kuwa na matokeo mabaya. Akishuhudia mbele ya Bunge la Juu la Amerika, daktari Judith Reisman, anayeongoza mambo ya utafiti kuhusu ponografia anasema hivi: “Picha ao habari za ngono ambazo mutu anatazama zinabana kabisa ao kuandikwa kwenye ubongo na zinabadilisha namna ya kufikiri, na wakati kwa wakati, zinaendelea kujitokeza bila kutaka, na zinaacha alama ambayo ni vigumu kuifuta ao hata haiwezekani kuifuta.” Susan, aliye na miaka 19, ambaye aliona mambo ya ponografia kwenye Internete, anasema hivi: “Picha hizo zimebandikwa katika akili yangu. Zinajitokeza akilini bila kutazamia. Ninajisikia kuwa siwezi kabisa kuzifuta katika akili yangu.”

JAMBO AMBALO UNAPASWA KUJUA: Ponografia inafanya watu kuwa watumwa na inaharibu kabisa wale ambao wanaitazama.​—2 Petro 2:19.

Ponografia ina matokeo gani juu ya familia?

MAMBO AMBAYO WACHUNGUZI WANASEMA: “Ndoa na familia zinavunjika kwa sababu ya ponografia.”​—Kitabu kinachoeleza mutego wa ponografia (Porn Trap) kilichoandikwa na Wendy na Larry Maltz.

Ponografia inaharibu ndoa na familia kwa

Biblia inawashauria bibi na bwana ‘wasitendeane kwa hila [ao udanganyifu].’ (Malaki 2:16) Kufanya ngono inje ya ndoa ni aina ya hila ambayo inaweza kuharibu ndoa na kufanya bibi na bwana watengane na hata kuvunja ndoa. Watoto wanaumia wakati baba na mama wanatengana ao kuvunja ndoa.

Ponografia inaweza pia kuumiza watoto moja kwa moja. Brian, aliyetajwa hapo juu, anaeleza hivi: “Wakati nilikuwa na miaka karibu kumi, nilipata bila kutazamia magazeti ya ponografia ya baba yangu nilipokuwa ninacheza muchezo wa kujificha na kufichuana. Nilianza kuyatazama kwa siri, bila kuelewa sababu gani nilivutiwa na picha hizo. Niliendelea na tabia hiyo ya kutazama picha chafu mupaka nilipokuwa mutu muzima.” Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba ponografia inaweza kuwachochea vijana waanze kufanya ngono wakiwa bado wadogo na pia wawe na mwenendo mupotovu na wenye jeuri kingono, na kuvurugika moyoni na katika akili.

JAMBO AMBALO UNAPASWA KUJUA: Ponografia inaharibu mahusiano yenye upendo na mwishowe inaleta maumivu makali ya moyoni na taabu.​—Methali 6:27.

Biblia inasema nini juu ya ponografia?

NENO LA MUNGU LINASEMA HIVI: ‘Muue viungo vya mwili wenu . . . kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye mazara, na kutamani, ambako ni ibada ya sanamu.’​—Wakolosai 3:5.

Kwa kifupi, Yehova * Mungu anachukia ponografia. Hilo si kwa sababu anachukia ngono. Aliumba uwezo wetu wa kufanya ngono na alikusudia bibi na bwana watumie uwezo huo ili kufurahishana, kufanya uhusiano wa karibu kwa kuambiana namna wanavyojisikia moyoni, na kushiriki jambo la ajabu la kuzaa watoto.​—Yakobo 1:17.

Kwa hiyo, sababu gani tunaweza kusema kwamba Yehova anachukia sana ponografia? Fikiria tu sababu chache.

JAMBO AMBALO UNAPASWA KUJUA: Ponografia inaharibu uhusiano wa mutu pamoja na Mungu.​—Waroma 1:24.

Hata hivyo, Yehova, ana huruma nyingi kuelekea wale wanaotaka kutoka katika mutego wa ponografia. Biblia inasema hivi: “Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema, si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fazili zenye upendo. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi.” (Zaburi 103:8, 14) Anawaalika watu wapole waje kwake ili ‘wapokee rehema na kupata fazili zisizostahiliwa kuwa musaada kwa wakati unaofaa.’​—Waebrania 4:16; soma kisanduku “Namna ya Kuacha Kabisa Tabia ya Kutazama Ponografia.”

Watu wengi sana wamekubali musaada wa Mungu. Je, musaada wa Mungu ni wenye kufaa? Ona mambo ambayo Biblia inasema juu ya watu fulani ambao waliacha kabisa tabia hiyo mbaya: ‘Mumeoshwa mukawa safi, . . . mumetakaswa, . . . mumetangazwa kuwa waadilifu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa roho ya Mungu wetu.’ (1 Wakorintho 6:11) Kama mutume Paulo, watu kama hao wanaweza kusema hivi: “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye anayenipa nguvu.”​—Wafilipi 4:13.

Susan, ambaye ameshinda tabia yake ya kutazama mambo ya ponografia, anasema hivi: “Ni Yehova tu ndiye anaweza kumusaidia mutu ashinde tabia ya kutazama ponografia. Ikiwa mutu anamuomba musaada na mwongozo, anaweza kuwa na musimamo muzuri mbele yake. Hawezi kumuacha mutu ashindwe na tabia hiyo.”

^ Neno “ponografia” linamaanisha habari za waziwazi za ngono ambazo zina kusudi la kuamusha hamu ya ngono kwa mutu ambaye anatazama, anasoma, ao kusikiliza habari hizo. Ponografia inaweza kuwa picha, habari zilizoandikwa ao habari za kusikiliza tu.

^ Majina yamebadilishwa katika habari hii.

^ Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.