Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Nilipenda Kuwa Padiri”

“Nilipenda Kuwa Padiri”
  • ALIZALIWA MWAKA WA 1957

  • ALIZALIWA KATIKA INCHI YA MEXIQUE

  • ALIKUWA MWANAFUNZI KWENYE SEMINERE NA PIA MUTU MWENYE HASIRA KALI

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa katika muji mudogo wa Texcoco. Wakati huo, barabara nyingi zilikuwa za udongo na zenye vumbi. Tulizoea kuona watu wa vijiji vya karibu wakileta vitu vya kuuzisha katika muji kwenye punda zao. Familia yetu ya watoto kenda ilikuwa masikini sana, mimi nilikuwa mutoto wa saba. Baba yangu alikuwa anashona viatu ili kutegemeza familia. Lakini alikufa wakati nilikuwa na miaka saba. Tangu wakati huo, mama yangu alijikaza ili kupata chakula kwa ajili ya familia.

 

Baba muzaa-mama alikuwa anacheza fidla (chombo fulani cha muziki kinachofanana na gitare) na alikuwa kiongozi wa kikundi cha wanamuziki wanaoimba nyimbo za kidini. Karibu watu wote wa familia yetu walikuwa wanacheza chombo fulani cha muziki. Mama yangu alikuwa katika kikundi cha waimbaji wa kanisa, na mujomba wangu alikuwa muimbaji wa opera na muchezaji wa piano. Tulikuwa wakatoliki wenye bidii, nilikuwa ninatumika kwenye altare, na nilipenda kuwa misionere wa dini ya Katoliki. Wakati huohuo, nilikuwa ninapenda filme za karaté. Kadiri nilivyokuwa nikiangalia filme hizo, ndivyo nilivyoendelea kuwa mwenye hasira kali.

Katika muji wa Puebla, niliingia kwenye masomo ya kidini iliyotumika kama seminere. Nilikuwa na muradi wa kuwa padiri wa dini ya Katoliki. Lakini, katika mwaka wangu wa mwisho wa masomo, nilivunjwa moyo na Dini ya Katoliki. Mutawa mwanamuke kijana alinishawishi nilale naye. Nilipinga kishawishi hicho, lakini hali hiyo ilinifanya niwe na tamaa ya kuoa. Zaidi ya hiyo, nilitambua kwamba mapadiri wengi walikuwa wanaishi maisha ya unafiki. Mwishowe, nikaachana na muradi wangu wa kuwa padiri.

Nilipokuwa ninatumika kwenye altare, nilipenda kuwa misionere wa dini ya Katoliki, lakini pia nilikuwa ninapenda filme za karaté na niliendelea kuwa mutu mwenye hasira kali

Niliamua kujifunza muziki kwenye masomo kubwa ya muziki katika muji wa Mexique. Nilipomaliza masomo, nilioa, na kisha tukazaa watoto wane. Nilitegemeza familia yangu kwa kuimba katika Misa ya Dini ya Katoliki.

Kuanzia mwanzo, ndoa yetu ilikuwa na matatizo. Mimi na bibi yangu tulikuwa wakali mumoja na mwenzake, sababu kubwa ni kwamba tulikuwa tunasikiliana wivu. Kwanza tulikuwa tunagombana kwa maneno, kisha tukaanza kupigana. Mwishowe, kisha miaka 13, tuliamua kuachana na kisha tukavunja ndoa yetu.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Nilikutana kwa mara ya kwanza na Mashahidi wa Yehova mbele ya kuachana na bibi yangu. Mashahidi wawili waligonga kwenye mulango wetu na wakapenda kuzungumuzia Biblia pamoja nami. Niliwaza kwamba nilijua mingi juu ya dini, kwa hiyo nikapenda kuwaonyesha kama wanasema uongo. Niliwauliza maulizo magumu ambayo niliwaza hayana majibu. Lakini, nilishangaa kwamba walinitolea majibu mazuri yenye kutegemea Biblia. Nilianza kujiona kuwa sijue kitu. Hata hivyo, bibi yangu hakupendezwa kabisa na Mashahidi wa Yehova, na mimi nilikuwa na kazi nyingi, kwa hiyo wakaacha kututembelea.

 

Kisha miaka tano, nilipokutana tena na Mashahidi wa Yehova, tayari nilikuwa ninaishi na bibi mwengine anayeitwa Elvira. Elvira yeye hakupinga Mashahidi, na hilo liliniwezesha kujifunza Biblia kwa ukawaida. Hata hivyo, iliniomba miaka mingi ili kubadilisha maisha yangu.

Nilitambua kwamba ikiwa ninataka kumuabudu Yehova kwa moyo wote, nilihitaji kufanya mabadiliko fulani makubwa. Kwanza, nilipaswa kuacha kazi yangu ya kuimba katika Misa ya Kanisa Katoliki, jambo lililomaanisha kwamba nilipaswa kutafuta njia nyingine ya kutosheleza mahitaji yetu. (Ufunuo 18:4) Tena nilihitaji kuandikisha kisheria ndoa yangu pamoja na Elvira.

Kuzuia hasira yangu kali ni jambo moja kati ya mambo ambayo yalikuwa magumu kwangu kubadilisha. Kuna maandiko mawili ya Biblia yaliyonisaidia kabisa: Andiko la Zaburi 11:5, ambalo linaonyesha kama Yehova anachukia jeuri, na andiko la 1 Petro 3:7, ambalo lilinifundisha kwamba ikiwa ninapenda Yehova asikilize sala zangu, nilipaswa kumutendea bibi yangu kwa heshima. Nilipoendelea kutafakari ao kufikiri sana juu ya maandiko hayo na kusali Yehova anisaidie, niliweza hatua kwa hatua kuzuia hasira yangu kali.

Biblia ilinifundisha kama ikiwa ninapenda Yehova asikilize sala zangu, nilipaswa kumutendea bibi yangu kwa heshima

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Leo ninafurahia maisha ya familia yenye furaha. Ninajikaza kutengeneza uhusiano wangu pamoja na watoto ambao nilizaa na bibi yangu wa kwanza na kusaidia familia yangu ya sasa iendelee kuwa na imani yenye nguvu.

 

Wakati nilikuwa mutoto, nilipenda kuwa padiri na kuwasaidia watu. Sasa ninajisikia kuwa na maisha yenye maana kabisa. Ninategemeza familia yangu kwa kufundisha muziki. Ninamushukuru sana Yehova kwa kuwa alinivumilia, kwa kunipatia nafasi ya kubadilika na kuwa mutu muzuri!