Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kweli Kumuhusu Mungu na Kristo

Kweli Kumuhusu Mungu na Kristo

Hata kama wanadamu wanaabudu miungu mingi, kuko tu Mungu mumoja wa kweli. (Yohana 17:3) Yeye ni “Mwenye Kuwa Mukubwa Zaidi,” Muumbaji wa kila kitu na Chanzo cha uzima wote. Ni yeye tu njo anastahili ibada yetu.​—Danieli 7:18; Ufunuo 4:11.

Mungu Ni Nani?

Jina la Mungu linapatikana katika maandishi ya kwanza-kwanza MARA 7000 HIVI

YEHOVA ni jina la Mungu

BWANA, MUNGU, BABA​—Majina fulani ya heshima ya Yehova

Jina la Mungu Ni Nani? Mungu mwenyewe anasema hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Isaya 42:8) Jina la pekee la Mungu linapatikana mara 7000 hivi katika Biblia. Hata hivyo, tafsiri mingi za Biblia zinatumia kimakosa jina la heshima, kama vile “Bwana” pa nafasi ya jina hilo. Mungu anataka ukuwe rafiki yake, kwa hiyo anakutia moyo ‘uitie jina lake.’​—Zaburi 105:1.

Majina ya Heshima ya Yehova. Biblia inazungumuzia Yehova kwa kutumia majina ya heshima kama vile “Mungu,” “Mweza-Yote,” “Muumbaji,” “Baba,” “Bwana,” na “Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi.” Katika sala mingi zenye kuwa mu Biblia, watu walisali kwa Yehova kwa kutumia ile majina ya heshima na pia jina lake la pekee, Yehova.​—Danieli 9:4.

Mungu Iko na Umbo Gani? Mungu ni roho, hatuwezi kumuona. (Yohana 4:24) Biblia inaunga mukono ile kweli kwa kusema kama “hakuna mwanadamu mwenye amemuona Mungu.” (Yohana 1:18) Biblia inafunua namna anajisikiaka. Watu wanaweza kumuhuzunisha, ao ‘kumufurahisha.’​—Mezali 11:20; Zaburi 78:40, 41.

Sifa za Mungu Zenye Kuvutia. Mungu hana ubaguzi kuelekea watu wa mataifa yote na desturi. (Matendo 10:34, 35) Pia, ni “mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu na kweli.” (Kutoka 34:6, 7) Lakini, kuko sifa ine za Mungu zenye kuvutia zaidi.

Nguvu. Juu yeye ni “Mungu Mweza-Yote,” iko na nguvu zenye hazina mipaka ili kutimiza kila ahadi yenye anatoa.​—Mwanzo 17:1.

Hekima. Hekima ya Mungu inapita hekima ya mutu mwingine yeyote. Njo maana Biblia inasema kama ni yeye peke yake njo “mwenye hekima.”​—Waroma 16:27.

Haki. Sikuzote Mungu anafanya mambo yenye kuwa sawa. Matendo yake ni “kamilifu,” na “hana ukosefu wa haki hata kidogo.”​—Kumbukumbu la Torati 32:4.

Upendo. Biblia inasema kama “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Mungu haonyeshe tu upendo​—yeye ni mufano muzuri zaidi wa upendo. Kila jambo lenye anafanya linachochewa na upendo wake wa juu zaidi, na tunafaidika na ule upendo mu njia mingi.

Urafiki wa Mungu Pamoja na Wanadamu. Mungu ni Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. (Matayo 6:9) Kama tunamutumainia, tunaweza kuwa marafiki wake. (Zaburi 25:14) Kwa kweli, Mungu anakuomba umukaribie katika sala na ‘kumutupia mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakuhangaikia.’​—1 Petro 5:7; Yakobo 4:8.

Kuko Tofauti Gani Kati ya Mungu na Kristo?

Yesu na Mungu Ni Watu Wawili Tofauti. Yesu ni mutu wa pekee​—ni yeye tu njo mwenye aliumbwa moja kwa moja na Mungu. Njo maana Biblia inamuita Mwana wa Mungu. (Yohana 1:14) Kisha kumuumba Yesu, Yehova alimutumia muzaliwa wake wa kwanza kama “fundi wa kazi” ili kuumba kila kitu na mutu mwingine yeyote.​—Mezali 8:30, 31; Wakolosai 1:15, 16.

Yesu Kristo Hajasemaka Kama Yeye Ni Mungu. Lakini, alisema hivi: “Mimi ni mwakilishi kutoka [kwa Mungu], na Yeye alinituma.” (Yohana 7:29) Wakati alikuwa anazungumuza na mwanafunzi wake mumoja, Yesu alimuita Yehova “Baba yangu na Baba yenu” na “Mungu wangu na Mungu wenu.” (Yohana 20:17) Kisha Yesu kufa, Yehova alimufufua ili aishi mbinguni na alimupatia mamlaka makubwa kwenye mukono Wake wa kuume.​—Matayo 28:18; Matendo 2:32, 33.

Yesu Kristo Anaweza Kukusaidia Umukaribie Mungu

Yesu alikuja ku dunia ili kutufundisha kumuhusu Baba yake. Yehova mwenyewe alisema hivi kumuhusu Yesu: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize.” (Marko 9:7) Yesu anamujua Mungu muzuri zaidi kuliko mutu mwingine yeyote. Alisema hivi: “Hakuna mwenye anajua Baba ni nani isipokuwa Mwana, na kila mutu mwenye Mwana anapenda kumufunulia Baba.”​—Luka 10:22

Yesu anaiga sifa za Mungu kwa ukamili. Yesu aliiga sifa za Baba yake kwa ukaribu sana hivi kwamba angeweza kusema: “Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.” (Yohana 14:9) Yesu alifanya watu wamukaribie Mungu kwa kuiga upendo wa Baba yake katika maneno na matendo yake mwenyewe. Alisema hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yohana 14:6) Alisema tena hivi: “Waabudu wa kweli watamuabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anatafuta watu wa namna hiyo ili wamuabudu.” (Yohana 4:23) Wazia jambo hilo! Yehova iko anatafuta watu, kutia ndani wewe, wenye wanapenda kujua kweli kumuhusu yeye.