Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tabia-Pole—Njia Yenye Kuonyesha Hekima

Tabia-Pole—Njia Yenye Kuonyesha Hekima

Toñi, mwanamuke mumoja mwenye kuwa na uzoefu wa kutunza watu wenye kuzeeka alipiga hodi kwenye mulango, na mwanamuke mumoja mwenye kuwa na miaka 50 hivi alijibia. Mwanamuke huyo alimuchambua Toñi na kumufokea kwa sababu hakufika mbele ya wakati ili kutunza mama mwenye kuzeeka wa mwanamuke huyo. Toñi hakuchelewa kwenye kazi. Lakini, aliomba mwanamuke huyo musamaha kwa upole kwa sababu hawakuelewana.

SIKU ingine, mwanamuke huyo alitombokea tena Toñi. Alitenda namna gani? Alisema hivi: “Ilikuwa hali ngumu sana; hakukuwa na sababu ya kunitukana vile.” Hata hivyo, Toñi aliomba tena musamaha na kuambia mwanamuke huyo kama alielewa magumu yenye alikuwa nayo.

Ungekuwa Toñi, unafikiri wewe ungetenda namna gani? Ungejikaza kuonyesha tabia-pole? Ingekuwa vigumu kuzuia hasira yako? Kusema kweli, inaweza kuwa vigumu kuzuia hasira katika hali kama ile yenye kuzungumuziwa hapo juu. Wakati tuko na mahangaiko ao wakati watu wanatuchokoza, ni vigumu kabisa kuonyesha tabia-pole.

Lakini, Biblia inatia moyo Wakristo wakuwe na tabia-pole. Kwa kweli, Neno la Mungu linapatanisha sifa hiyo na kuwa na hekima. Yakobo anauliza hivi: ‘Ni nani aliye na hekima na mwenye uelewaji kati yenu? Na aonyeshe kutokana na mwenendo wake muzuri matendo yake kwa upole ulio wa hekima.’ (Yak. 3:13) Ni katika njia gani sifa ya tabia-pole inaonyesha hekima yenye kutoka juu? Na ni nini inaweza kutusaidia kukomalisha sifa hiyo yenye kumupendeza Mungu?

HEKIMA YENYE KUTOKANA NA ROHO YA TABIA-POLE

Tabia-pole inaweza kutuliza hasira. ‘Jibu, linapokuwa la upole, linageuza gazabu [hasira], lakini neno linaloumiza linafanya hasira ipande.’Met. 15:1.

Kujibia kwa hasira kunaweza kufanya hali ya mubaya ikuwe ya mubaya zaidi kwa sababu hilo linaongeza mafuta kwenye moto. (Met. 26:21) Lakini, jibu lenye kutolewa kwa tabia-pole mara nyingi linatuliza. Linaweza hata kutuliza mutu mwenye kuwa mukali sana.

Toñi alijionea jambo hilo. Wakati aliona namna Toñi alimujibia kwa tabia-pole, mwanamuke huyo alianza kulia. Alimuelezea kama alikuwa anahangaika sana kwa sababu ya magumu yake mwenyewe na ya familia yake. Toñi alitoa ushahidi wa muzuri, na funzo la Biblia lilianzishwa; aliweza kufanya hivyo kwa sababu alionyesha sifa ya upole na roho ya kufanya amani.

Sifa ya tabia-pole inaweza kutuletea furaha. ‘Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairiti dunia.’Mt. 5:5.

Sababu gani wale wenye kuwa na tabia-pole wako na furaha? Watu wengi wenye walikuwa wakali zamani, wamekuwa na furaha sasa kwa sababu wanaonyesha sifa hiyo. Wamekuwa na maisha ya muzuri, na wanajua kama watakuwa na maisha ya muzuri zaidi wakati unaokuja. (Kol. 3:12) Adolfo, mwangalizi mumoja wa muzunguko katika inchi ya Uhispania, anakumbuka namna maisha yake yalikuwa mbele ajue kweli.

Adolfo anasema hivi: “Maisha yangu hayakukuwa na kusudi; nilikuwa na tabia ya kukasirika haraka sana; kwa hiyo, hata marafiki wangu fulani wanaume walikuwa wananiogopa kwa sababu ya matendo yangu yenye kiburi na jeuri. Mwishowe mambo yalibadilika. Katika pigano moja, niliumizwa vidonda sita kwa kunitoboa na kisu na damu ilinilitoka karibu kufa.”

Lakini sasa, kupitia maneno na mufano wake, Adolfo anafundisha wengine wakuwe na tabia-pole. Watu wengi wanajisikia huru kumukaribia na wanapendezwa na sifa zake za muzuri. Adolfo anasema kama yeye ni mwenye furaha kwa sababu ameweza kufanya mabadiliko. Na ni mwenye shukrani kwa Yehova kwa sababu amemusaidia kukomalisha sifa ya tabia-pole.

Tabia-pole inamufurahisha Yehova. ‘Ukuwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumujibu anayenizihaki [anayenichokoza].’Met. 27:11.

Kwa kweli, Yehova anachokozwa na adui wake mukubwa zaidi, ni kusema, Shetani. Mungu ana sababu zote za kuwa na hasira juu mambo yote ya mubaya yenye kusemwa kimakusudi juu yake, lakini Biblia inaonyesha kuwa Yehova “si mwepesi wa hasira.” (Kut. 34:6) Wakati tunajikaza kuiga sifa ya Mungu ya kutokuwa mwepesi wa hasira na upole wake, tunafuata njia ya hekima yenye kumupendeza sana Yehova.—Efe. 5:1.

Watu wa ulimwengu huu ni wakali kila mara. Tunaweza kukutana na watu “wenye kujidai [wenye kiburi], wenye majivuno, wakufuru, . . . wachongezi, wasiojizuia, wakali.” (2 Tim. 3:2, 3) Lakini, hilo haliwezi kuzuia Mukristo kukomalisha roho ya upole. Neno la Mungu linatukumbusha kama “hekima inayotoka juu ni . . . yenye kufanya amani, yenye usawaziko.” (Yak. 3:17) Wakati tunaonyesha roho ya kufanya amani na ya usawaziko, tunaonyesha wazi kama tumepata hekima yenye kutoka kwa Mungu. Hekima hiyo itatuchochea tujibie kwa upole wakati watu wanatuchokoza na itafanya tukaribie hata zaidi Chanzo cha hekima yenye haina mipaka, ni kusema, Yehova.