Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Mageuzi

Mageuzi

Watu fulani wanasema kama uzima ulitokana na mageuzi. Wengine wanasema kama Mungu alianzisha tu uumbaji na kisha akaacha hatua ya mageuzi iendelee. Biblia inasema nini?

Habari ya Biblia juu ya uumbaji inakataa uwezekano wa kwamba ulimwengu ulitokezwa kupitia mulipuko mukubwa?

Biblia inasema tu hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Haionyeshe waziwazi namna Mungu aliumba kila kitu. Hata kama ulimwengu ulitokea kupitia mulipuko mukubwa, hilo halipinge mambo yenye Biblia inasema. Lakini, andiko la Mwanzo 1:1 linatoa jibu la ulizo hili: Ni nani alitokeza mulipuko huo mukubwa?

Kwa kweli, wanasayansi wengi wanaamini kama mulipuko huo mukubwa ulikuwa tukio lenye lilijitokeza lenyewe na bila mupango, na kama tukio hilo lilifanya atomu zijipange kuwa nyota na sayari (planète) mbalimbali kwa kipindi fulani cha wakati. Biblia haiunge mukono mawazo hayo lakini inasema kama ulimwengu ulifanywa moja kwa moja na Mungu, iwe alitumia aina fulani ya mulipuko mukubwa ao njia ingine ya uumbaji.

“Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”Mwanzo 1:1.

Habari ya Biblia inakubali kama viumbe vyenye uzima vinaweza kubadilika kisha wakati fulani?

Ndiyo. Biblia inasema kama Mungu aliumba viumbe vyenye uzima “kulingana na aina zake.” (Mwanzo 1:11, 12, 21, 24, 25) Mabadiliko yanaweza kutokea katika aina fulani? Ndiyo. Hata hivyo, mabadiliko hayo katika aina fulani yanaonyesha kama aina za mupya zinaweza kutokea? Hapana.

Fikiria mufano huu: Kati ya mwaka wa 1971 na 1980, wachunguzi walifanya uchunguzi juu ya shorewanda (aina fulani ya ndege) katika Visiwa vya Galápagos. Walitambua kama mabadiliko ya hali ya hewa yalifanya shorewanda wenye midomo mikubwa wasikufe sana. Watu fulani walisema kama hilo lilihakikisha mageuzi. Lakini, hilo lilihakikisha mageuzi, ao ilikuwa tu kujipatanisha na hali? Kisha miaka fulani, shorewanda wenye midomo midogo walikuwa wengi tena kuliko wale wenye midomo mikubwa. Jambo hilo lilimusukuma Jeffrey Schwartz, profesa wa antropolojia, kusema kwamba, hata kama kujipatanisha na hali kunaweza kusaidia aina mbalimbali za viumbe zisikufe wakati hali zinabadilika, “hilo halitokeze aina fulani mupya.”

Biblia na fundisho la mageuzi vinaweza kupatana?

Biblia inasema kama ‘[Mungu] aliumba vitu vyote.’ (Ufunuo 4:11) ‘Alipumzika’ tu wakati alimaliza kuumba kila kitu. (Mwanzo 2:2) Hilo linamaanisha kama Mungu hakuumba kiumbe fulani chepesi na kisha akapumzika, ao kungoja tu kwa miaka mingi wakati kiumbe hicho kilikuwa kinageuka-geuka na kutokeza aina mbalimbali za samaki, sokwe (makako), na wanadamu. * Fundisho hilo lenye kuitwa mageuzi makubwa, linapinga daraka la Muumbaji mwenye Biblia inasema kama ‘aliumba mbingu na vitu vilivyo ndani yake na dunia na vitu vilivyo ndani yake na bahari na vitu vilivyo ndani yake.’—Kutoka 20:11; Ufunuo 10:6.

“Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”Ufunuo 4:11.

Ili kujua mengi zaidi: Biblia inasema kama ‘sifa zake [Mungu] ambazo hazionekane, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa.’ (Waroma 1:20) Kujifunza juu ya Mungu kunaweza kufanya maisha yakuwe na maana kabisa, kwa sababu ana kusudi lenye upendo juu ya watu wote wenye kumutafuta kwa moyo wote. (Mhubiri 12:13; Waebrania 11:6) Ili kupata habari zingine, fungua adresi yetu ya Internete www.pr418.com/sw ao uzungumuze na Mashahidi wa Yehova. Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA.

^ fu. 12 Biblia haikubali kama Mungu aliumba dunia katika kipindi cha siku sita zenye urefu wa saa 24 kila moja, kama vile watu fulani wanaamini. Ili kupata habari zingine, soma broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? kwenye ukurasa wa 24-27. Broshua hiyo ilichapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza pia kuichukua bila kulipa kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com/sw