Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Mujusi wa Miiba-Miiba Mwenye Ngozi Yenye Kukokota Maji

Mujusi wa Miiba-Miiba Mwenye Ngozi Yenye Kukokota Maji

MUJUSI wa miiba-miiba wa Australia (Moloch horridus) anakokota maji katika ukungu (mawingu mazito meupe yenye kusababisha giza), katika hewa yenye umaji-maji, na katika muchanga wenye kulowana. Kisha anasukuma maji hayo katika kinywa chake ili kuyakunywa. Namna gani? Inawezekana ngozi yake yenye kushangaza ndiyo inamuwezesha kufanya hivyo.

Mikunjo yenye kuwa kwenye ngozi inaunganishwa na njia zingine za chini ya ngozi ili maji yaongozwe kwenye kinywa cha mujusi wa miiba-miiba

Fikiria jambo hili: Ngozi ya miiba-miiba ya mujusi huyo inafunikwa na magamba. Wanasayansi fulani wanawaza kama umande ao maji yenye kukusanywa kwenye magamba yanapita kwenye sehemu ya ngozi yake isiyokuwa teketeke na kuingia katika njia zenye kufunguliwa kidogo, ao mikunjo, zenye kuwa katikati ya magamba. Njia hizo zinaunganishwa na zinaongoza kwenye kinywa cha mujusi huyo.

Lakini namna gani mujusi huyo anakokota maji kupitia miguu yake, anayapandisha kwenye mwili wake, na kuyafikisha katika kinywa chake bila kufuata nguvu za uvutano? Na namna gani mujusi huyo anakokota maji kwenye nafasi zenye kulowana kwa kugeuza-geuza tumbo lake kwenye nafasi hizo?

Inawezekana wachunguzi wamevumbua siri yake. Kupitia mifereji, njia zenye kuwa kwenye ngozi zinaunganishwa na njia zingine za chini zenye kuwa katika ngozi. Namna njia hizo zinafanywa inawezesha kukokota maji na kuyaingiza katika nafasi ndogo-ndogo bila hata kufuata nguvu za uvutano. Kwa hiyo, ngozi ya mujusi huyo inatumika kama sponji (éponge).

Janine Benyus, kiongozi wa shirika moja lenye kutumia njia za kuiga uumbaji, anasema kama kuiga njia za kukokota maji za mujusi huyo kunaweza kusaidia mafundi kutengeneza njia ya kutosha umaji-maji katika hewa, ili kufanya majengo yenye kuwa na hewa ya muzuri na tena ili kupata maji ya kunywa.

Unawaza namna gani? Ngozi ya miiba-miiba yenye kukokota maji ya mujusi huyo ilijitokeza yenyewe? Ao iliumbwa?

Photograph: © Minden Pictures/SuperStock