Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Mutu Fulani Mwenye Unapenda Anagonjwa

Wakati Mutu Fulani Mwenye Unapenda Anagonjwa

Wakati Baba alikaribia kutoka katika hospitali, tulimuomba muganga wake atuonyeshe tena majibu ya uchunguzi wenye ulifanywa juu ya damu ya Baba. Muganga huyo alituhakikishia kama majibu ya uchunguzi yalikuwa muzuri, lakini kwa upole, alikubali kuyaangalia tena. Alishangaa kuona kama majibu mbili hayakukuwa muzuri! Aliomba musamaha na akaita muganga mwengine mwenye kujua muzuri magonjwa ya Baba. Sasa Baba anajisikia muzuri. Lakini tunafurahi sana kwa sababu tuliuliza maulizo.”—Maribel.

Mbele ya kuenda kuonana na muganga, uandike namna mugonjwa anajisikia na dawa zenye anatumia

Kuenda kuonana na waganga na kubakia kwenye hospitali kunaweza kuhangaisha akili. Kama vile Maribel alijionea, musaada wa rafiki ao mutu wa jamaa unaweza kusaidia sana, pengine hata kuokoa uzima. Namna gani unaweza kusaidia mutu fulani mwenye unapenda?

Mbele ya kuenda kuonana na muganga. Usaidie mugonjwa kuandika namna anajisikia na dawa yoyote yenye anatumia ao matunzo mengine. Tena, uandike ulizo lolote lenye munaweza kuuliza muganga. Usaidie rafiki yako akumbuke mambo yote juu ya ugonjwa wake ao ikiwa ugonjwa huo umekwisha kupata mutu fulani katika jamaa yake. Usiwaze kama muganga anajua mambo hayo ao atayauliza.

Usikilize kwa uangalifu, uulize maulizo ya heshima, na uandike mambo ya lazima

Wakati munazungumuza na muganga. Uhakikishe kama wewe na mugonjwa munaelewa mambo muganga anasema. Uulize maulizo, lakini uepuke kukazia mawazo yako. Umuache mugonjwa aulize maulizo na ajisemee. Usikilize kwa uangalifu na uandike mambo ya lazima. Uulize juu ya namna mbalimbali za matunzo. Katika hali fulani, inaweza kuwa muzuri umuombe mugonjwa atafute mawazo kwa muganga mwengine.

Uchunguze maagizo ya muganga, na dawa zenye aliandikia mugonjwa

Kisha kuonana na muganga. Uchunguze pamoja na mugonjwa ni siku gani ataenda tena kuonana na muganga. Uhakikishe kama anapata dawa yenye muganga alimuandikia. Umutie moyo akunywe dawa kama vile muganga aliandika na ajulishe muganga bila kukawia ikiwa dawa inaleta tatizo fulani. Umuombe mugonjwa aendelee kuwa na mawazo ya muzuri, na umutie moyo afuate maagizo mengine yoyote, kama vile yenye anapewa wakati anachunguzwa kila mara na muganga. Umusaidie ajue mengi zaidi juu ya ugonjwa wake.

Wakati Muko Katika Hospitali

Uhakikishe kama fomu zote zinajazwa muzuri

Ukuwe mutulivu na muangalifu. Wakati mugonjwa anaingia katika hospitali, anaweza kujisikia mwenye woga na bila tumaini. Kama uko mutulivu na muangalifu, unaweza kusaidia kila mutu atulizane na aepuke kufanya makosa. Uhakikishe kama fomu za kukubaliwa kubakia katika hospitali zinajazwa muzuri. Uheshimie haki ya mugonjwa ya kukamata maamuzi ya muzuri juu ya matunzo. Lakini kama ni mugonjwa sana na anashindwa kufanya hivyo, uheshimie mambo aliandika na mamlaka ya mutu wa karibu wa jamaa yake ao ya mutu mwenye alichagua ili kumutetea katika matunzo. *

Kwa heshima, ujulishe waganga mabadiliko yenye unaona kwa mugonjwa

Ukuwe tayari kuzungumuza. Usiogope kuzungumuza. Sura yako yenye kuonyesha heshima na adabu vinaweza kuchochea waganga wamuhangaikie zaidi mugonjwa, na hata wamutunze muzuri zaidi. Katika hospitali nyingi, wagonjwa wanachunguzwa na waganga mbalimbali. Unaweza kuwasaidia kwa kuwaelezea mambo yenye waganga wengine walisema. Kwa sababu unamujua mugonjwa muzuri, useme mabadiliko yoyote yenye unaona juu ya afya yake ya kimwili ao ya kiakili.

Ufanye yote unaweza bila kusema pa nafasi ya mugonjwa

Uonyeshe heshima na shukrani. Mara nyingi, waganga wanatumika katika hali zenye kuhangaisha akili. Uwatendee namna ungependa kutendewa. (Mathayo 7:12) Uwaonyeshe heshima kwa ajili ya mazoezi na uzoefu wao, uwaonyeshe kama unatumainia uwezo wao, na uwaonyeshe shukrani kwa ajili ya bidii yao. Kufanya hivyo kunaweza kuwachochea watumike muzuri zaidi.

Hakuna mutu mwenye anaweza kuepuka kugonjwa. Lakini kwa kufikiri mbele ya wakati na kutoa musaada wenye kufaa, unaweza kusaidia rafiki ao mutu wa jamaa apambane muzuri na hali ngumu.—Methali 17:17.

^ fu. 8 Sheria na mambo mengine juu ya haki na mapashwa ya mugonjwa viko tofauti mahali mbalimbali. Uhakikishe kama maandishi ya mugonjwa yenye kuwa na mambo anapenda juu ya matunzo yanaenea na yangali ya mupya