Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Umasikini

Umasikini

Hata kama watu fulani wanajikaza ili kumaliza tatizo la umasikini, kuko mamilioni ya watu katika dunia wenye kuishi katika umasikini.

Namna gani watu masikini wanaweza kuwa na furaha?

MAMBO WATU WANASEMA

Watu wengi wanaamini kwamba kuwa na vitu vingi vya kimwili kunaleta furaha na kutosheka na kama kiasi cha feza zenye mutu iko nazo kitamufanya akuwe na maisha ya muzuri. Watu wanawaza kama masikini hawawezi kuwa na furaha kwa sababu hawana uwezo wa kusoma masomo ya muzuri ao masomo yoyote, kupata matunzo ya muzuri ao matunzo yoyote, na mambo mengine ya muzuri.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inafundisha kama, haiko feza zenye mutu iko nazo ndizo zinaweza kumuletea furaha ya kweli, lakini ni hali yake ya muzuri ya kiroho na urafiki wake pamoja na Mungu. Biblia inasema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Hata kama wako na feza nyingi ao hapana, watu wenye kutambua uhitaji wao wa kiroho wanachochewa kutafuta mawazo ya Mungu juu ya hali mbalimbali za maisha. Kwa kufanya hivyo wanaweza kujifunza mafundisho ya Biblia yenye kuwaletea faraja ya kweli na amani ya akili. Jambo hilo ndilo linaleta furaha ya kweli.

Wale wenye kuelewa na kufuata mashauri ya Biblia wanajua muzuri namna ya kupambana na umasikini. Kwa mufano, mashauri ya Biblia yanatia watu moyo kuepuka tabia mbaya, kama vile kuvuta tumbako na kunywa pombe sana. Tabia kama hizo zinapoteza feza bure na baada ya muda zinaweza kumuletea mutu magonjwa yenye kuomba matunzo ya bei sana.—Methali 20:1; 2 Wakorintho 7:1.

Tena, Biblia inatupatia angalisho juu ya matokeo ya tamaa mbaya na kupenda vitu vya kimwili. (Marko 4:19; Waefeso 5:3) Shauri hilo linaweza kusaidia mutu aepuke kupoteza feza bure katika michezo ya feza ao “kupenda pesa [feza].” Biblia inasema kama kupenda feza ni “chanzo cha mambo mabaya ya namna zote.” (1 Timotheo 6:10) Maandiko yanatoa angalisho hili: ‘Hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokane na vitu alivyo navyo.’ (Luka 12:15) Kwa kifupi, hakuna kiasi fulani cha feza chenye kinaweza kuuza uzima. Lakini, kufuata mashauri ya hekima ya Biblia kunafanya maisha yakuwe na maana na kunaleta furaha ya kweli.

Hata kama watu wenye kuishi katika umasikini wanaweza kuteseka ili kupata chakula, nguo, na makao, wanaweza kupata furaha nyingi kwa kufurahia yenye wako nayo, kutumia maisha yao ili kumupendeza Muumbaji wao, na kuishi kupatana na mapenzi yake. Wanajua kama ahadi hii ya Biblia ni ya kweli: “Baraka ya Yehova—hiyo ndiyo inatajirisha, naye haongezi maumivu pamoja nayo.”—Methali 10:22.

ANDIKO LA MAANA: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”Mathayo 5:3.

Umasikini utaisha siku fulani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Wanadamu wamejikaza kutoa misaada ili kumaliza tatizo la umasikini, lakini hawajaweza hata kidogo. Hata hivyo, kwa wakati wake wenye kufaa, Mungu atamaliza jambo lenye kuleta tatizo hilo, ni kusema, tabia ya wanadamu ya kujipenda wenyewe na serikali zenye kutafuta faida zao wenyewe. (Mhubiri 8:9) Muumbaji wetu ataweka Ufalme wake, ao serikali yake ya mbinguni, mahali pa serikali za wanadamu zenye kutafuta faida zao wenyewe. Ufalme huo utatolea wakaaji wote wa dunia vitu vingi, bila ubaguzi. Biblia inaahidi waziwazi kama Mufalme wa Ufalme wa Mungu atatimiza kwa huruma mahitaji ya masikini. ‘Atamukomboa masikini anayelilia musaada . . . Atamusikitikia mutu wa hali ya chini na masikini, naye ataziokoa nafsi [uzima] za masikini.’—Zaburi 72:12-14.

Dunia itakuwa paradiso ya kweli na watu wote watakuwa na nyumba na chakula; umasikini hautakuwa tena. Katika kitabu cha Biblia cha Isaya, Mungu anaahidi hivi juu ya watu wake: “Watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. . . . Watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.” (Isaya 65:21, 22) Kuliko kuteseka ili kutafuta namna ya kuishi, wote watafurahia “karamu ya vyakula vinono” na vitu vingine vya muzuri vyenye Yehova atawapatia.—Isaya 25:6.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Kufikiri sana juu ya ahadi ya Mungu ya kuleta dunia isiyokuwa na umasikini kunasaidia watu wenye kuishi katika hali ngumu wakuwe na uhakika kama Mungu anawahangaikia na kama shida zao ziko karibu kuisha. Kukaza akili juu ya tumaini hilo kunaweza kusaidia mutu apate nguvu za kuvumilia hali ngumu leo.

ANDIKO LA MAANA: ‘Atamukomboa masikini anayelilia musaada . . . Atamusikitikia mutu wa hali ya chini na masikini, naye ataziokoa nafsi za masikini.’ Zaburi 72:12, 13.