Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Chura Mwenye Kuzaa kwa Njia Isiyo ya Kawaida

Chura Mwenye Kuzaa kwa Njia Isiyo ya Kawaida

WATU wanafikiri kwamba Chura ambaye anazaa kwa njia isiyo ya kawaida amekosekana tangu mwaka wa 2002. Chura wa kike alimeza mayai yake yaliyokuwa yamekutana na ya chura wa kiume na kuchunga vitoto vyake katika tumbo lake kwa muda wa karibu majuma sita. Baadaye, vitoto vyake vilitoka katika tumbo vikiwa vyenye kukomaa.

Ili mama asisage mayai yake katika tumbo, iliomba aache kukula na atokeze asidi katika tumbo. Ni wazi kwamba kemikali zilizotoka kwenye mayai na vitoto vilivyo katika mayai hayo vilizuia kutengenezwa kwa asidi hiyo.

Mama angeweza kuchunga mayayi karibu 24 katika tumbo. Wakati alizaa, kitoto chake kilikuwa na uzito wa karibu kilo 40 juu ya 100 ya uzito wake. Ni kama mwanamuke aliye na kilo 68 mbele awe na mimba ya watoto 24, na kila mutoto akiwa na kilo 1.8! Vitoto vilipanua tumbo la chura huyo mupaka kufinya sana mapafu yake, na kwa hiyo alilazimika kupumua kupitia ngozi.

Kwa kawaida vitoto vya chura huyo vilitoka katika tumbo kisha kipindi fulani kwa wakati ambao vilikuwa vimekomaa. Hata hivyo, ikiwa mama aliona hatari, alilazimika kuzaa kwa kutapika vitoto hivyo. Siku moja wachunguzi wamekwisha kuona mama akitapika vitoto vyake sita kwa wakati uleule; akivitupa hewani umbali wa karibu meta 1.

Kama watu fulani wanavyodai, ikiwa namna yake ya kuchunga mayayi ndani ya tumbo ilitokana na mageuzi, basi mwili wote na tabia za chura huyo zingebadilika mara moja na kwa njia kubwa. Mwanasayansi Michael J. Tyler aliandika hivi: “Haiwezekane chura huyo aendelee kufanya mabadiliko polepole katika namna yake ya kuchunga mayayi ndani ya tumbo. Ikiwa ingekuwa hivyo, asidi iliyo katika tumbo lake ingeharibu mayayi.” Tyler anasema kwamba mafasirio yenye kukubalika ni kwamba kuna “hatua moja kubwa.” Watu fulani wanawaza kwamba hatua kubwa hiyo ni uumbaji. *

Unawaza nini? Chura mwenye kuzaa kwa njia isiyo ya kawaida alitokana na mageuzi ao aliumbwa?

^ fu. 7 Katika kitabu chake L’Origine des espèces, Charles Darwin aliandika hivi: “Uteuzi wa asili (ao kuponyoka kwa viumbe vyenye nguvu na kufa kwa viumbe zaifu) unawezekana tu katika mabadiliko madogo madogo, hautokee haraka-haraka ao kwa gafula . . .”