Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 6

Faida ya Kuongozwa na Kanuni za Mwenendo

Faida ya Kuongozwa na Kanuni za Mwenendo

KUONGOZWA NA KANUNI ZA MWENENDO MAANA YAKE NINI?

Watu wenye wanaongozwa na kanuni za mwenendo wanatambua waziwazi tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye kuwa makosa. Kujua ikiwa jambo fulani ni la muzuri ao ni la mubaya hakutegemee namna wanajisikia ile wakati. Lakini kunategemea kanuni zenye hazibadilike zenye zinaongoza mwenendo wao, hata wakati wengine hawawaone.

JUU YA NINI KANUNI ZA MWENENDO NI ZA MAANA?

Watoto wanasikia habari mingi za uongo kuhusu mwenendo, ikuwe kupitia watu wenye wanaenda nao ku masomo, muziki wenye wanasikiliza, ao kupitia filme na programu za televizyo. Habari hizo zinaweza kufanya watoto wakuwe na mashaka juu ya mambo yenye walifundishwa kuhusu mambo ya muzuri na mambo ya mubaya.

Ile ni tatizo kubwa kwa watoto wenye kuwa kati ya miaka 13 na 19. Kitabu Beyond the Big Talk kinasema kama, ile wakati watoto “wako na lazima ya kuelewa kama watu wengi watawakaza watende mu njia fulani ili wengine wawapende, na wanapaswa kujifunza kufanya mambo yenye wanajua kuwa ni ya muzuri hata kama marafiki wao hawapendi ile mambo.” Ni wazi kwamba, wazazi wanapaswa kuzoeza watoto wao mbele wafikie miaka ya ujana.

NAMNA YA KUWAFUNDISHA KANUNI ZA MWENENDO

Uwafundishe wajue tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye kuwa makosa.

KANUNI YA BIBLIA: “Watu wakomavu . . . wamezizoeza [nguvu zao za utambuzi] kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.”​—Waebrania 5:14.

  • Tumia maneno yenye kuonyesha wazi kama mambo fulani ni ya muzuri ao ni ya mubaya. Tumia hali za kila siku na uonyeshe waziwazi tofauti kwa kusema hivi: “Kufanya hivi ni kutenda kwa uaminifu; kufanya hivi ni kukosa uaminifu.” “Ukifanya hivi watu watakutumainia; ukifanya hivi watu hawatakutumainia.” “Kufanya hivi ni muzuri; kufanya hivi haiko muzuri.” Ile itasaidia mutoto wako afikie kujifunza mambo ya muzuri yenye anapaswa kufanya na mambo ya mubaya yenye hapaswe kufanya.

  • Umufasirie ni juu ya nini jambo fulani ni la muzuri ao la mubaya. Kwa mufano, unaweza kumuuliza hii maulizo: Juu ya nini ni muzuri zaidi kuwa musema-kweli? Namna gani kusema uongo kunaweza kuharibisha urafiki? Juu ya nini kuiba ni mubaya? Ufikiri muzuri na mutoto wako ili kumusaidia akomalishe uwezo wake wa kutambua mambo ya muzuri na ya mubaya.

  • Umuonyeshe faida za kufuata kanuni za muzuri za mwenendo. Unaweza kusema: “Kama uko musema-kweli, wengine watakutumainia” ao “Kama uko mupole, watu watafurahia kuwa pamoja na wewe.”

Uhakikishe kama familia yako inajulikana kuwa yenye kuishi kulingana na kanuni za muzuri za mwenendo.

KANUNI YA BIBLIA: “Muendelee kuhakikisha namna ninyi wenyewe muko.”​—2 Wakorinto 13:5.

  • Kanuni za mwenendo zenye unaweka zinapaswa kuwa sehemu ya familia yako, ili uweze kusema hivi waziwazi:

    • “Mu familia yetu hatusemake uongo.”

    • “Hatupiganake ao kulalamikia wengine.”

    • “Hatutukane wengine.”

Mutoto wako ataona kuwa kanuni za mwendo zenye unaweka haziko tu sheria zenye zinapaswa kufuatwa, lakini kuwa ni kanuni zenye zinatambulisha familia yenu.

  • Kila mara uzungumuze na mutoto wako kuhusu mambo yenye familia yenu inaona kuwa ya maana. Utumie mambo yenye kufanyika kila siku ili kufundisha watoto wako. Unaweza kulinganisha kanuni zako na kanuni zenye kuzungumuziwa ku televizyo na ku masomo. Uliza mutoto wako hii maulizo: “Wewe ungefanya nini?” “Familia yetu ingefanya nini mu ile hali?”

Utie nguvu azimio lao la kufanya mambo ya muzuri.

KANUNI YA BIBLIA: “Muendelee kuwa na zamiri ya muzuri.”​—1 Petro 3:16.

  • Usifu tabia yake ya muzuri. Kama mutoto wako anaonyesha tabia za muzuri mu mambo yenye anafanya, umusifu na uonyeshe ni juu ya nini unamusifu. Kwa mufano, unaweza kusema hivi: “Ulitenda kwa uaminifu. Unanifurahisha sana.” Kama mutoto wako anasema waziwazi kama alifanya jambo fulani la mubaya, umusifu kabisa kwa kukuambia kweli yote mbele umurekebishe.

  • Umusaidie arekebishe tabia ya mubaya. Saidia watoto wako wakubali matokeo ya matendo yao. Watoto wanapaswa kujua ni jambo gani la mubaya lenye walifanya na namna mwenendo wao unapingana na kanuni za mwenendo zenye kuongoza familia. Wazazi fulani wanajizuia kuambia watoto wao kuwa wamekosea, juu hawapendi wavunjike moyo. Lakini kuambia watoto ni juu ya nini jambo fulani lenye walifanya ni la mubaya kutazoeza zamiri yao na kuwasaidia waepuke kufanya jambo fulani la mubaya wakati wenye kuja.