Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Mambo Gani Unajua Juu ya Mashahidi wa Yehova?

Ni Mambo Gani Unajua Juu ya Mashahidi wa Yehova?

Unatuona tunahubiria watu. Pengine umesoma mambo fulani juu yetu katika vyombo vya habari ao watu wengine wamekuelezea mambo fulani juu yetu. Lakini, unajua kabisa Mashahidi wa Yehova?

PIMA IKIWA UNAJUA

Onyesha ikiwa kila musemwa ni kweli ao uongo.

KWELI UONGO

  1. Mashahidi wa Yehova ni Wakristo.

  2. Mashahidi wa Yehova ni wanauumbaji.

  3. Mashahidi wa Yehova hawaitike matunzo.

  4. Mashahidi wa Yehova wanaitika Biblia yote.

  5. Mashahidi wa Yehova wanatumia tu tafsiri yao ya Biblia.

  6. Mashahidi wa Yehova walibadilisha Biblia yao ili ipatane na mambo yenye wanaamini.

  7. Mashahidi wa Yehova hawasaidiake watu wengine.

  8. Mashahidi wa Yehova wanazarau watu wa dini zingine.

    Ili kupata majibu, ona kurasa zenye kufuata.

  1. 1 KWELI. Tunafanya yetu yote ili kufuata sana mafundisho na tabia ya Yesu Kristo. (1 Petro 2:21) Lakini, kuko mambo mengi yenye kutufanya tukuwe tofauti na dini zingine zenye kujiita kuwa za Kikristo. Kwa mufano, tunaamini kama Biblia inafundisha kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu; yeye haiko sehemu ya Utatu. (Marko 12:29) Tunaamini kama nafsi inakufaka, na kama hakuna andiko lolote lenye kuonyesha kuwa Mungu anatesa watu katika moto wa milele. Tena, hatuamini kama wale wenye kuongoza katika makanisa wanapaswa kuwa na majina ya cheo yenye kuwainua juu ya wengine.—Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4; Mathayo 23:8-10.

  2. 2 UONGO. Tunaamini kama Mungu aliumba kila kitu. Lakini hatuitike mawazo ya wanauumbaji wengi. Sababu gani? Kwa sababu mawazo mengi ya wanauumbaji yanapingana na Biblia. Kwa mufano, wanauumbaji fulani wanasema kama dunia iliumbwa katika siku sita za saa 24 kila moja. Lakini neno “siku” katika Biblia linaweza kumaanisha kipindi kirefu cha wakati. (Mwanzo 2:4; Zaburi 90:4) Tena, wanauumbaji fulani wanafundisha kama dunia imefanya tu maelfu kidogo ya miaka. Lakini, Biblia inaonyesha kama dunia na ulimwengu wote tayari vilikuwa kwa miaka mingi mbele ya siku sita za uumbaji. 1Mwanzo 1:1.

  3. 3 UONGO. Tunaitika matunzo. Kwa kweli, wengine kati yetu ni wanganga, kama vile Luka, Mukristo wa wakati wa mitume. (Wakolosai 4:14) Lakini, tunakataa matunzo yote yenye kupingana na kanuni za Biblia. Kwa mufano, hatuitike kutiwa damu katika mishipa, kwa sababu Biblia inakataza kutumikisha damu.—Matendo 15:20, 28, 29.

    Hata hivyo, tunafanya yetu yote ili kutafuta matunzo ya muzuri kwa ajili yetu na familia zetu. Kwa kweli, ufundi wa kusaidia damu isivuje sana wakati wa upasuaji wenye ulifanywa ili kusaidia Mashahidi wa Yehova, unatumiwa sasa ili kusaidia pia watu wengine. Leo katika inchi nyingi, mugonjwa yeyote anaweza kuchagua matunzo yenye hayaombe kutiwa damu, ili kuepuka magonjwa yenye kutokea kwa sababu ya kutiwa damu katika mishipa, matatizo ya mufumo wa kinga, na makosa ya watu.

  4. 4 KWELI. Tunaamini kuwa Biblia yote ‘imeongozwa na roho ya Mungu nayo ni yenye faida.’ (2 Timotheo 3:16) Biblia yote iko na sehemu mbili zenye watu wengi wanaita Agano la Kale na Agano Jipya. Kwa kawaida, tunaita sehemu hizo za Biblia Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Katika njia hiyo, tunaepuka kuonyesha kama sehemu fulani za Biblia ni za zamani ao haziko za maana leo.

  5. 5 UONGO. Tunatumikisha tafsiri nyingi za Biblia ili kujifunza Biblia. Lakini tunafurahia kutumikisha zaidi sana Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga ambamo inapatikana, kwa sababu inatumia jina la Mungu, haikosee, na iko wazi. Tuzungumuzie kutumiwa kwa jina la Mungu, Yehova. Katika maneno ya utangulizi ya tafsiri moja ya Biblia, kuko liste ya majina ya watu 79 wenye walichangia, katika njia moja ao nyingine, ili kutafsiri Biblia hiyo. Hata hivyo, tafsiri hiyohiyo inaondoa jina la Mutungaji mwenyewe wa Biblia, ni kusema, Yehova Mungu! Tofauti na tafsiri hiyo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inarudisha jina la Mungu katika maelfu ya nafasi kwenye lilipatikana katika maandishi ya kwanza ya Biblia. 2

  6. 6 UONGO. Mara nyingi, wakati tulivumbua kama mambo yenye tuliamini hayakupatana na Biblia, tulibadilisha uelewaji wetu. Zamani sana mbele ya kuchapisha Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika mwaka wa 1950, tulitumikisha tafsiri zingine za Biblia zenye zilipatikana wakati huo na mambo tuliamini yalipatana na tafsiri hizo.

  7. 7 UONGO. Kazi yetu ya kuhubiri inaletea watu wengi faida. Tumesaidia watu wengi kuachana na mazoea fulani yenye kuwafanya watumwa, kama vile kunywa pombe sana na kutumikisha dawa za kulewesha. Masomo yetu ya kufundisha watu kusoma na kuandika yanasaidia watu wengi katika dunia yote kujua kusoma na kuandika. Tena, wakati musiba wa asili unatokea, tunasaidia Mashahidi na wenye hawako Mashahidi. Tunajikaza kuwatia moyo na kuwatolea musaada wa kiroho wenye wako nao lazima kabisa katika hali kama hizo. 3

  8. 8 UONGO. Tunafuata shauri la Biblia lenye kusema, “Muheshimu watu wote,” hata kama wako na dini zao. (1 Petro 2:17, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Kwa mufano, hata kama katika inchi fulani tuko wengi sana, hatujaribu kuchochea wakubwa wa serikali ao watu wenye kutunga sheria ili wakataze kazi ya dini zingine. Na hatufanye kampanye za kuomba sheria zitungwe ili kulazimisha watu wengine wafuate kanuni zetu za mwenendo na imani yetu. Lakini, tunaonyesha watu wengine uvumilivu wenye tunapenda watuonyeshe pia.—Mathayo 7:12.

Habari hii iko na maelezo fulani yenye kutoka kwenye adresi yetu ya Internete, jw.org. Ili kujua mengi, fungua kichwa KUTUHUSU > MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI.

^ 1. Kwa sababu hiyo, kama wanauumbaji, hatupinge uchunguzi wenye kutegemeka wa wanasayansi wenye kuonyesha kama inawezekana dunia imefanya mamiliare ya miaka.

^ 2. Kuko jambo lingine lenye kufanya Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ikuwe tofauti na tafsiri zingine: Tunaipatia watu bila kulipa. Matokeo ni kwamba, mamilioni ya watu wanaweza kusoma Biblia katika luga yao ya kizalikio. Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inapatikana leo katika luga 130 hivi. Unaweza hata kuisoma kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com.

^ 3. Tunatumia michango yetu katika njia nyingi. Njia moja kati ya hizo ni kusaidia watu wenye wamepatwa na misiba ya asili. (Matendo 11:27-30) Kwa kuwa kazi hiyo inafanywa na watu wenye kujitolea wasiolipwa, feza zenye zilichangwa zinatumiwa zaidi sana ili kutoa misaada wala haiko ili kulipa watu.