Ona video zinazopatikana

Dini, Mungu, ao Biblia, Vinaweza Kunisaidia Niwe na Furaha?

Dini, Mungu, ao Biblia, Vinaweza Kunisaidia Niwe na Furaha?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Biblia, ambayo ni kitabu cha zamani chenye hekima, inajibu maulizo yanayowasumbua watu wengi maishani na inaweza kukusaidia ujisikie vizuri zaidi na uwe na maisha yenye maana. Fikiria maulizo fulani ambayo Biblia inajibu.

  1.   Je, kuna Muumbaji? Biblia inasema kwamba Mungu “aliumba vitu vyote.” (Ufunuo 4:11) Kwa kuwa Mungu ndiye Muumbaji wetu, anajua mambo tunayohitaji na ili tuwe na furaha na maisha yenye maana.

  2.   Je, Mungu ananihangaikia? Biblia haizungumuzie Mungu kuwa mutu asiyehangaikia wanadamu, lakini inasema kwamba ‘hayuko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Mungu anaona mambo yanayokupata katika maisha na anataka kukusaidia uwe na maisha mazuri.—Isaya 48:17, 18; 1 Petro 5:7.

  3.   Namna gani kumujua Mungu kunaweza kunisaidia niwe na furaha zaidi? Mungu alituumba na “uhitaji wa kiroho,” ni kusema, tamaa ya kiasili ya kuelewa maana na kusudi la maisha. (Mathayo 5:3) Uhitaji wetu wa kiroho unatia ndani tamaa ya kujua Muumbaji wetu na kuwa na urafiki wa karibu pamoja naye. Mungu atafurahia sana jitihada ambayo utafanya ili kumujua, kwa sababu Biblia inasema hivi: ‘Mukaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.

 Mamilioni ya watu wametambua kwamba kuwa na urafiki pamoja na Mungu kumefanya maisha yao yawe mazuri na kumewaonyesha mambo ya kufanya ili kuwa na furaha katika maisha. Kumujua Mungu hakutamaliza matatizo yako yote, lakini hekima ya Biblia inaweza kukusaidia

 Dini nyingi zinazotumia Biblia hazifundishe yale ambayo Biblia inafundisha kabisa. Lakini, dini ya kweli, ambayo inafuata kabisa yale ambayo Biblia inasema, itakusaidia umujue Mungu.