Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Ni Dini ya Kiprotestanti?

Je, Mashahidi wa Yehova Ni Dini ya Kiprotestanti?

 Hapana. Mashahidi wa Yehova ni Wakristo. Sisi si Waprotestanti. Kwa nini?

 Waprotestanti wamefafanuliwa kuwa “kikundi cha kidini kinachopinga Ukatoliki.” Ingawa ni kweli kwamba Mashahidi wa Yehova hawaungi mkono mafundisho ya Kanisa Katoliki, sisi si Waprotestanti kwa sababu zifuatazo:

  1.   Mafundisho kadhaa ya dini ya Kiprotestanti hayapatani na yale ambayo Biblia inafundisha. Kwa mfano, Biblia inafundisha kwamba “kuna Mungu mmoja,” haifundishi kuhusu Utatu. (1 Timotheo 2:5; Yohana 14:28) Pia inafundisha kwamba Mungu hatawaadhibu waovu kwa kuwatupa katika moto wa mateso, bali atawaharibu milele.​—Zaburi 37:9; 2 Wathesalonike 1:9.

  2.   Hatujihusishi hata kidogo na harakati za kupinga au kuleta mabadiliko katika kikundi chochote kile cha kidini kutia ndani Ukatoliki. Kinyume kabisa na jambo hilo, kazi yetu ni kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu huku tukiendelea kujitahidi kuwasaidia watu wasitawishe imani katika habari njema za Ufalme huo. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Lengo letu si kuleta mabadiliko katika vikundi mbalimbali vya kidini vilivyomo duniani, lengo letu ni kuwafundisha watu wanyoofu kweli kumhusu Mungu na Neno lake, Biblia.​—Wakolosai 1:​9, 10; 2 Timotheo 2:​24, 25.