Barua ya Kwanza kwa Timotheo 2:1-15

  • Kusali kwa ajili ya watu wa namna zote (1-7)

    • Mungu mmoja, mpatanishi mmoja (5)

    • Fidia inayolingana kwa ajili ya wote (6)

  • Maagizo kwa wanaume na wanawake (8-15)

    • Kuvaa kwa kiasi (9, 10)

2  Basi, kwanza kabisa, ninahimiza kwamba dua, shukrani, sala, na maombi yatolewe kwa ajili ya watu wa namna zote,  kutia ndani wafalme na wote wenye vyeo vya juu,*+ ili tuendelee kuishi kwa amani na utulivu na ujitoaji-kimungu* kamili na kuchukua mambo kwa uzito.+  Jambo hilo ni zuri na linampendeza Mwokozi wetu, Mungu,+  ambaye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe+ na kupata ujuzi sahihi wa kweli.  Kwa maana kuna Mungu mmoja,+ na mpatanishi mmoja+ kati ya Mungu na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+  aliyejitoa kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote*+—hilo litatolewa ushahidi kwa wakati wake unaofaa.  Kwa ajili ya ushahidi huo+ niliwekwa rasmi niwe mhubiri na mtume+—ninasema ukweli, sisemi uwongo⁠—mwalimu wa mataifa+ kuhusu imani na kweli.  Basi ninatamani kwamba kila mahali wanaume waendelee kusali, wakiinua mikono yenye ushikamanifu,+ bila hasira+ wala mabishano.+  Vivyo hivyo, wanawake wanapaswa kujipamba kwa mavazi yanayofaa,* kwa kiasi na utimamu wa akili,* si kwa mitindo ya kusuka nywele, dhahabu, lulu, au mavazi ya bei ghali sana,+ 10  bali kwa njia inayowafaa wanawake wanaokiri kwamba wanamtumikia Mungu,+ yaani, kupitia matendo mema. 11  Mwanamke na ajifunze akiwa kimya* na kwa ujitiisho kamili.+ 12  Simruhusu mwanamke afundishe wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume, bali akae kimya.*+ 13  Kwa maana Adamu aliumbwa kwanza, kisha Hawa.+ 14  Pia, Adamu hakudanganywa, bali mwanamke alidanganywa kabisa+ akawa mtenda dhambi. 15  Hata hivyo, atalindwa kupitia kuzaa watoto,+ maadamu anaendelea* kuwa na imani, upendo, utakatifu, na utimamu wa akili.*+

Maelezo ya Chini

Au “wenye mamlaka.”
Angalia Kamusi.
Au “watu wa namna zote.”
Au “yenye kuheshimika.”
Au “kufanya maamuzi mazuri; busara.”
Au “kwa utulivu.”
Au “awe mtulivu.”
Tnn., “wanaendelea.”
Au “kufanya maamuzi mazuri; busara.”