Hamia kwenye habari

Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?

Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?

Je, ulimwengu wetu . . .

  • utabaki jinsi ulivyo?

  • utakuwa mbaya hata zaidi?

  • utaboreka?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Mungu . . . atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

Kazi yenye maana na inayoridhisha.—Isaya 65:21-23.

Hakutakuwako tena na magonjwa au mateso ya aina yoyote ile.—Isaya 25:8; 33:24.

Maisha yenye furaha yasiyo na mwisho pamoja na familia na marafiki.—Zaburi 37:11, 29.

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa angalau sababu mbili:

  • Mungu ana uwezo wa kutimiza ahadi hiyo. Katika Biblia, ni Yehova Mungu peke yake anayeitwa “Mweza-Yote,” kwa kuwa ana nguvu zisizo na mipaka. (Ufunuo 15:3) Kwa hiyo anaweza kutimiza kabisa ahadi yake ya kuubadili ulimwengu wetu uwe mzuri zaidi. Kama Biblia inavyosema, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” —Mathayo 19:26.

  • Mungu anatamani kutimiza ahadi hiyo. Kwa mfano, Yehova anatamani sana kuwafufua watu waliokufa.—Ayubu 14:14, 15.

    Pia, Biblia inaonyesha kwamba Mwana wa Mungu, Yesu, aliwaponya wagonjwa. Kwa nini alifanya hivyo? Ni kwa sababu alitaka kufanya hivyo. (Marko 1:40, 41) Yesu alimwiga Baba yake kikamili kwa kutamani kuwasaidia waliokuwa na uhitaji.—Yohana 14:9.

    Kwa hiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova na Yesu wanataka kutusaidia tufurahie maisha wakati ujao!—Zaburi 72:12-14; 145:16; 2 Petro 3:9.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Mungu ataubadilishaje ulimwengu wetu uwe mzuri zaidi?

Biblia inajibu swali hilo kwenye MATHAYO 6:9, 10 na DANIELI 2:44.