Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
Je, ulimwengu wetu . . .
-
utabaki jinsi ulivyo?
-
utakuwa mbaya hata zaidi?
-
utaboreka?
BIBLIA HUSEMA HIVI
“Mungu . . . atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO
Kazi yenye maana na inayoridhisha.—Isaya 65:21-23.
Hakutakuwako tena na magonjwa au mateso ya aina yoyote ile.—Isaya 25:8; 33:24.
Maisha yenye furaha yasiyo na mwisho pamoja na familia na marafiki.—Zaburi 37:11, 29.
JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?
Ndiyo, kwa angalau sababu mbili:
-
Mungu ana uwezo wa kutimiza ahadi hiyo. Katika Biblia, ni Yehova Mungu peke yake anayeitwa “Mweza-Yote,” kwa kuwa ana nguvu zisizo na mipaka. (Ufunuo 15:3) Kwa hiyo anaweza kutimiza kabisa ahadi yake ya kuubadili ulimwengu wetu uwe mzuri zaidi. Kama Biblia inavyosema, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” —Mathayo 19:26.
-
Mungu anatamani kutimiza ahadi hiyo. Kwa mfano, Yehova anatamani sana kuwafufua watu waliokufa.—Ayubu 14:14, 15.
Pia, Biblia inaonyesha kwamba Mwana wa Mungu, Yesu, aliwaponya wagonjwa. Kwa nini alifanya hivyo? Ni kwa sababu alitaka kufanya hivyo. (Marko 1:40, 41) Yesu alimwiga Baba yake kikamili kwa kutamani kuwasaidia waliokuwa na uhitaji.—Yohana 14:9.
Kwa hiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova na Yesu wanataka kutusaidia tufurahie maisha wakati ujao!—Zaburi 72:12-14; 145:16; 2 Petro 3:9.
JAMBO LA KUFIKIRIA
Mungu ataubadilishaje ulimwengu wetu uwe mzuri zaidi?
Biblia inajibu swali hilo kwenye MATHAYO 6:9, 10 na DANIELI 2:44.