Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 7

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

1. Ufalme wa Mungu ni nini?

Kwa nini Yesu ni Mfalme anayefaa?​—MARKO 1:40-42.

Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Serikali hiyo itaziondoa serikali nyingine zote nayo itafanya mapenzi ya Mungu yatendeke hapa duniani kama ilivyo mbinguni. Habari kuhusu Ufalme wa Mungu ni yenye kupendeza. Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utatosheleza uhitaji wa wanadamu wa kuwa na serikali nzuri. Itawaunganisha watu wote duniani.​—Soma Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10; 24:14.

Lazima ufalme uwe na mfalme. Yehova alimchagua Mwana wake, Yesu Kristo, awe Mfalme wa Ufalme Wake.​—Soma Ufunuo 11:15.

Tazama video Ufalme wa Mungu Ni Nini?

2. Kwa nini Yesu ndiye Mfalme anayefaa?

Mwana wa Mungu ndiye Mfalme anayefaa kwa sababu ni mwenye fadhili, anafuata haki. (Yohana 1:14) Pia, ana uwezo wa kuwasaidia watu kwa sababu ataitawala dunia akiwa mbinguni. Baada ya kufufuliwa, Yesu alipaa mbinguni na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Yehova akingoja kupewa ufalme. (Waebrania 10:12, 13) Mwishowe, Mungu alimpa mamlaka ya kuanza kutawala.​—Soma Danieli 7:13, 14.

3. Ni nani watakaotawala pamoja na Yesu?

Kikundi cha watu wanaoitwa “watakatifu” watatawala pamoja na Yesu mbinguni. (Danieli 7:27) Wanafunzi waaminifu wa Yesu ndio waliokuwa wa kwanza kuchaguliwa kuwa watakatifu. Yehova ameendelea kuchagua wanaume na wanawake waaminifu kuwa watakatifu hadi sasa. Kama Yesu, watakatifu hao wanafufuliwa katika mwili wa roho.​—Soma Yohana 14:1-3; 1 Wakorintho 15:42-44.

Ni watu wangapi wanaoenda mbinguni? Yesu aliwaita “kundi dogo.” (Luka 12:32) Mwishowe, hesabu yao itakuwa 144,000. Watatawala pamoja na Yesu juu ya dunia.​—Soma Ufunuo 14:1.

4. Ni nini kilichotokea Yesu alipoanza kutawala?

Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mwaka wa 1914. * Jambo la kwanza ambalo Yesu alifanya alipowekwa rasmi kuwa Mfalme, lilikuwa kumtupa Shetani na mashetani wake duniani. Shetani alikasirika sana naye akaleta matatizo mengi duniani kote. (Ufunuo 12:7-10, 12) Tangu wakati huo, matatizo ya wanadamu yameongezeka sana. Vita, njaa, magonjwa yenye kuenea, na matetemeko ya nchi ni sehemu ya “ishara” inayoonyesha kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utaitawala dunia nzima.​—Soma Luka 21:7, 10, 11, 31.

5. Ufalme wa Mungu unatimiza nini?

Kupitia kazi inayofanywa duniani kote ya kuhubiri, tayari Ufalme wa Mungu unaunganisha umati mkubwa wa watu kutoka katika mataifa yote. Mamilioni ya watu wapole wanakuwa raia wa Yesu. Ufalme wa Mungu utawalinda wakati ambapo mfumo mwovu wa mambo uliopo utakapoharibiwa. Hivyo, wote wanaotaka kufaidika kutokana na Ufalme wa Mungu wanapaswa kujifunza kuwa raia watiifu wa Yesu.​—Soma Ufunuo 7:9, 14, 16, 17.

Katika kipindi cha miaka 1,000, Ufalme huo utatimiza kusudi la Mungu la tangu awali kuelekea wanadamu. Dunia yote itakuwa paradiso. Mwishowe, Yesu atamrudishia Baba yake Ufalme. (1 Wakorintho 15:24-26) Je, unamjua mtu yeyote ambaye ungependa kumweleza kuhusu Ufalme wa Mungu?​—Soma Zaburi 37:10, 11, 29.

 

^ fu. 6 Unaweza kupata habari kamili kuhusu jinsi unabii wa Biblia ulivyotabiri kuhusu mwaka wa 1914, katika ukurasa wa 215-218 kwenye kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?