Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kushoto: Yasser Qudaih/Anadolu via Getty Images; kulia: RONALDO SCHEMIDT/AFP via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?

Vita Vitakwisha Lini?​—Biblia Inasema Nini?

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema hivi kuhusu shambulizi la moja kwa moja la Iran dhidi ya Israel Jumamosi, Aprili 13, 2024: “Huu ndio wakati wa kujaribu kupunguza uhasama unaongezeka. Sasa ndio wakati wa kujidhibiti kikamili.”

 Vita vinavyoendelea katika Mashariki ya Kati ni mfano mmoja tu wa kinachoendelea ulimwenguni pote.

 “Sasa hivi kuna mapambano mengi zaidi yanayoendelea ulimwenguni pote kuliko wakati mwingine wowote tangu Vita vya Pili vya Ulimwengu na vinawaathiri watu bilioni 2, yaani, robo ya wanadamu wote.”​—Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Januari 26, 2023.

 Maeneo ambayo yanahusika katika vita yanatia ndani Israel, Gaza, Siria, Azerbaijan, Ukrainia, Sudan, Ethiopia, Niger, Myanmar, na Haiti. a

 Vita vitakwisha lini? Je, viongozi wa ulimwengu wanaweza kutokeza amani? Biblia inasema nini?

Ulimwengu uliojaa vita

 Mapambano yenye jeuri yanayoendelea leo ulimwenguni pote yanaonyesha kwamba hivi karibuni vita vyote vitakwisha. Vita vinavyoendelea vinatimiza unabii wa Biblia kuhusu kipindi cha wakati tunamoishi. Biblia inaita kipindi hicho “umalizio wa mfumo wa mambo.”​—Mathayo 24:3.

  •    “Mtasikia kuhusu vita na habari za vita. . . . Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.”​—Mathayo 24:6, 7.

 Soma makala yenye kichwa “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?” ili uone jinsi vita vinavyoendelea vinavyotimiza unabii wa Biblia?

Vita vya kukomesha vita vyote

 Biblia inatabiri mwisho wa mapambano ya wanadamu. Hilo litatukiaje? Si kwa jitihada za wanadamu, bali kupitia Har-Magedoni, “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Baada ya vita hivyo, Mungu atatimiza ahadi yake kwa wanadamu ya kuwaletea amani ya kudumu.​—Zaburi 37:10, 11, 29.

 Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu vita vya Mungu vya kukomesha vita vyote, soma makala yenye kichwa “Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?

a Orodha ya ACLED ya Mapambano, “Inaorodhesha mapambano yenye jeuri zaidi ulimwenguni pote,” Januari 2024