Ufunuo kwa Yohana 16:1-21

  • Mabakuli saba ya hasira ya Mungu (1-21)

    • Yamwagwa duniani (2), baharini (3), kwenye mito na chemchemi (4-7), kwenye jua (8, 9), kwenye kiti cha ufalme cha mnyama-mwitu (10, 11), kwenye Mto Efrati (12-16), na hewani (17-21)

    • Vita vya Mungu, Har-magedoni (14, 16)

16  Nami nikasikia sauti kubwa kutoka katika patakatifu+ ikiwaambia wale malaika saba: “Nendeni mkamwage yale mabakuli saba ya hasira ya Mungu juu ya dunia.”+  Malaika wa kwanza akaenda na kumwaga bakuli lake juu ya dunia.+ Na kidonda chenye maumivu na kilicho hatari+ kikawapata watu waliokuwa na alama ya yule mnyama wa mwituni+ na waliokuwa wakiiabudu sanamu yake.+  Malaika wa pili akamwaga bakuli lake ndani ya bahari.+ Nayo ikawa damu+ kama ya mwanadamu aliyekufa, na kila kiumbe aliye hai akafa,* ndiyo, vitu vilivyo ndani ya bahari.+  Malaika wa tatu akamwaga bakuli lake ndani ya mito na chemchemi za maji.*+ Nazo zikawa damu.+  Nikamsikia malaika aliye juu ya maji akisema: “Wewe, Ambaye uko na uliyekuwako,+ Mshikamanifu,+ wewe ni mwadilifu, kwa kuwa umetoa hukumu hizi,+  kwa sababu waliimwaga damu ya watakatifu na ya manabii,+ nawe umewapa damu wanywe;+ wanastahili hivyo.”+  Nikasikia madhabahu ikisema: “Ndiyo, Yehova* Mungu, Mweza-Yote,+ hukumu zako* ni za kweli na za uadilifu.”+  Malaika wa nne akamwaga bakuli lake juu ya jua,+ nalo jua likapewa ruhusa ya kuwaunguza watu kwa moto.  Na wale watu wakaunguzwa na joto hilo kali, lakini wakalikufuru jina la Mungu, aliye na mamlaka juu ya mapigo haya, nao hawakutubu wala kumpa utukufu. 10  Malaika wa tano akamwaga bakuli lake juu ya kiti cha ufalme cha yule mnyama wa mwituni. Na ufalme wake ukatiwa giza,+ nao wakaanza kuzitafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu yao, 11  lakini wakamkufuru Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu yao na vidonda vyao, nao hawakutubu matendo yao. 12  Malaika wa sita akamwaga bakuli lake juu ya mto mkubwa Efrati,+ na maji yake yakakauka+ ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme+ wanaotoka mashariki.* 13  Nami nikaona maneno matatu machafu yaliyoongozwa na roho* ambayo yalionekana kama vyura yakitoka katika kinywa cha yule joka+ na katika kinywa cha yule mnyama wa mwituni na katika kinywa cha yule nabii wa uwongo. 14  Kwa kweli, hayo ni maneno yanayoongozwa na roho waovu nayo yanafanya ishara,+ nayo yanakwenda kwa wafalme wa dunia nzima inayokaliwa, ili kuwakusanya pamoja kwa vita+ vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.+ 15  “Tazama! Ninakuja kama mwizi.+ Mwenye furaha ni yule anayekaa macho+ na kutunza mavazi yake ya nje, ili asije akatembea uchi na watu waitazame aibu yake.”+ 16  Nayo yakawakusanya pamoja mahali panapoitwa katika Kiebrania Har-Magedoni.*+ 17  Malaika wa saba akamwaga bakuli lake juu ya hewa. Ndipo sauti kubwa ikatokea katika patakatifu+ kwenye kile kiti cha ufalme, ikisema: “Imetimia!” 18  Kukawa na radi na sauti na ngurumo, na kukatokea tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu wanadamu walipoumbwa duniani,+ tetemeko hilo la ardhi lilikuwa kubwa sana na lilienea sana. 19  Lile jiji kubwa+ likapasuka na kuwa sehemu tatu, na majiji ya mataifa yakaanguka; na Babiloni Mkubwa+ akakumbukwa mbele za Mungu, ili kumpa kikombe cha divai cha hasira ya ghadhabu yake.+ 20  Pia, kila kisiwa kikatoweka, na milima haikupatikana tena.+ 21  Ndipo mvua kubwa ya mawe, kila jiwe likiwa na uzito wa karibu talanta moja,* ikanyesha kutoka mbinguni juu ya watu,+ nao watu wakamkufuru Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe,+ kwa kuwa pigo hilo lilikuwa kubwa mno.

Maelezo ya Chini

Au “kila nafsi ikafa.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Au “maamuzi yako ya hukumu.”
Au “mawio ya jua.”
Tnn., “roho waovu.”
Neno la Kigiriki, Har Ma·ge·donʹ, kutokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “Mlima wa Megido.”
Talanta ya Kigiriki ilikuwa sawa na kilogramu 20.4. Angalia Nyongeza B14.