Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Je, umaskini utaisha?

Mungu ataondoa jinsi gani umaskini ulimwenguni?—Mathayo 6:9, 10.

Ufukara unaosababisha utapiamlo na magonjwa huua mamilioni ya watu kila mwaka. Ingawa nchi nyingi zimeendelea kiuchumi, idadi kubwa ya watu ni maskini sana. Biblia inaonyesha kwamba umaskini umekuwapo kwa muda mrefu.—Soma Yohana 12:8.

Ili kuondoa umaskini ni lazima kuwe na serikali yenye uwezo wa kugawa kwa haki rasilimali za dunia. Serikali hiyo itahitaji kukomesha vita ambavyo ni chanzo kikubwa cha umaskini. Mungu ameahidi kuleta serikali hiyo.—Soma Danieli 2:44.

Ni nani atakayeondoa umaskini?

Mungu amemchagua Mwana wake, Yesu, atawale wanadamu. (Zaburi 2:4-8) Yesu atawakomboa maskini na kukomesha ukandamizaji na jeuri.—Soma Zaburi 72:8, 12-14.

Akiwa “Mkuu wa Amani” aliyetabiriwa, Yesu ataleta amani na usalama duniani. Watu wote wataishi katika nyumba zao, watafurahia kufanya kazi, na kutakuwa na chakula kingi.—Soma Isaya 9:6, 7; 65:21-23.