Hamia kwenye habari

Ninawezaje Kujilinda Dhidi ya Kusumbuliwa Kingono?

Ninawezaje Kujilinda Dhidi ya Kusumbuliwa Kingono?

Jibu la Biblia

 Fikiria mapendekezo haya yanayotegemeka na yanayopatana na hekima ya Biblia:

  1.   Kazia fikira kazi yako. Pendezwa na kuwaheshimu wafanyakazi wenzako, lakini usiruhusu urafiki ambao unaweza kuwafanya wafikiri unapendezwa nao kimapenzi.​—Mathayo 10:16; Wakolosai 4:6.

  2.   Valia kwa kiasi. Kuvaa nguo zinazoamsha ashiki kutafanya wengine watuelewe vibaya. Biblia inatutia moyo tuvalie kwa “kiasi na utimamu wa akili.”​—1 Timotheo 2:9.

  3.   Chagua marafiki wako kwa hekima. Ikiwa unatumia wakati mwingi pamoja na wale ambao wanapenda kuchezewa kimapenzi, ni rahisi kutendewa kama wao.​—Methali 13:20.

  4.   Epuka mazungumzo machafu. Usijihusishe kwenye mazungumzo yenye ‘hadithi chafu, au mizaha kuhusu ngono’.​—Waefeso 5:4.

  5.   Epuka vishawishi. Kwa mfano, uwe mwangalifu kuhusu mialiko ya kubaki kazini baada ya muda wa kazi ikiwa si lazima​—Methali 22:3.

  6.   Uwe imara na useme waziwazi. Ikiwa unasumbuliwa kingono, mweleze waziwazi mtu huyo kwamba hupendi tabia yake. (1 Wakorintho 14:9) Kwa mfano, unaweza kusema hivi: “Unanishika-shika, na sipendi tabia hiyo. Usiniguse.” Unaweza kumwandikia barua na kumweleza kilichotokea, jinsi ulivyohisi na kwamba hutaki arudie tena. Sema waziwazi kwamba msimamo wako unategemea maadili na mambo unayoamini.​—1 Wathesalonike 4:​3-5.

  7.   Tafuta msaada. Ikiwa unaendelea kusumbuliwa kingono, mweleze rafiki yako unayemwamini, mshiriki wa familia, mfanyakazi mwenzako au mtu mwenye uzoefu wa kusaidia watu wenye tatizo kama lako. (Methali 27:9) Waathiriwa wengi wamepata msaada kupitia sala. Hata kama hujawahi kusali, usipuuze msaada unaoweza kupata kutoka kwa Yehova “Mungu wa faraja yote.”​—2 Wakorintho 1:3.

 Kusumbuliwa kingono hufanya mazingira ya kazi kuwa yenye kuogopesha kwa watu wengi, hata hivyo Biblia inaweza kutusaidia.