Hamia kwenye habari

Je, Mungu Atanisaidia Nikisali?

Je, Mungu Atanisaidia Nikisali?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, Mungu huwasaidia wale wanaomwomba vitu vinavyopatana na mapenzi yake. Hata kama hujawahi kusali, mifano ya Biblia ya watu waliosali, “Mungu, unisaidie,” inaweza kukutia moyo. Kwa mfano:

  •   “Unisaidie, Ee BWANA Mungu wangu; uniokoe sawasawa na rehema yako.”—Zaburi 109:26, Zaire Swahili Bible.

  •   “Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, unihurumie; ee Mwenyezi-Mungu, unisaidie!”—Zaburi 30:10, Biblia Habari Njema.

 Bila shaka, mwandikaji wa maneno hayo alikuwa na imani kubwa katika Mungu. Hata hivyo, Mungu huwasikiliza wote wanaomjia wakiwa na mwelekeo unaofaa, kama wale “waliovunjika moyo” au “waliopondwa roho.”—Zaburi 34:18.

 Hupaswi kuogopa kwamba Mungu yuko mbali hivi kwamba hawezi kujishughulisha na matatizo yako. Biblia inasema: “Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu; lakini yeye anamjua mwenye kiburi kutoka mbali tu.” (Zaburi 138:6) Hata pindi moja Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote.” (Mathayo 10:30) Mungu huona mambo madogo kukuhusu ambayo hata wewe mwenyewe hujui. Basi, je, hilo halikuhakikishii kwamba atakuwa tayari kukusikiliza ukimwomba akusaidie na mahangaiko yako?—1 Petro 5:7.