Hamia kwenye habari

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuishi Pamoja Bila Kufunga Ndoa?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Kuishi Pamoja Bila Kufunga Ndoa?

Jibu la Biblia

 Biblia inasema mapenzi ya Mungu ni kwamba watu ‘wajiepushe na uasherati.’ (1 Wathesalonike 4:3) Kama linavyotumiwa katika Biblia, neno “uasherati” linatia ndani uzinzi, ngono kati ya watu wa jinsia moja, na ngono kati ya mwanamume na mwanamke ambao hawajafunga ndoa.

 Kwa nini ni muhimu kwa Mungu ikiwa mwanamume na mwanamke wanafunga ndoa?

  •   Mpango wa ndoa ulianzishwa na Mungu. Aliuanzisha alipowaunganisha mwanamume na mwanamke wa kwanza. (Mwanzo 2:22-24) Hakukusudia mwanamume na mwanamke waishi pamoja bila kufunga ndoa.

  •   Mungu anajua kinachowafaa wanadamu. Alikusudia ndoa iwe mpango wa kudumu kati ya mwanamume na mwanamke ambao ungewanufaisha na kuwalinda watu wote katika familia. Fikiria mfano rahisi. Kama tu maagizo kutoka kwa mtengenezaji wa kifaa fulani yanavyokuonyesha jinsi ya kukiunganisha kwa njia inayofaa, maagizo kutoka kwa Mungu yanatuonyesha jinsi ya kuwa na mahusiano mazuri katika familia. Sikuzote viwango vya Mungu huwanufaisha wale wanaovifuata.—Isaya 48:17, 18.

    Maagizo kutoka kwa mtengenezaji wa kifaa fulani hukuonyesha jinsi ya kukiunganisha kwa njia inayofaa. Maagizo kutoka kwa Mungu hutuonyesha jinsi ya kuwa na familia zenye mafanikio

  •   Ngono nje ya ndoa inaweza kuwa na madhara makubwa. Kwa mfano, inaweza kusababisha mimba zisizotakikana, magonjwa ya zinaa, na maumivu ya kihisia. a

  •   Mungu aliwapa mwanamume na mwanamke uwezo wa kutokeza uhai kupitia ngono. Mungu anaona uhai kuwa mtakatifu, na uwezo wa kutokeza uhai ni zawadi yenye thamani. Mungu anataka tuheshimu zawadi hiyo kwa kufuata mpango wake wa ndoa.—Waebrania 13:4.

 Namna gani kuhusu kuishi pamoja kabla ya kufunga ndoa ili kujaribu ikiwa mnapatana?

 Siri ya kuwa na ndoa yenye furaha si kuwa na “kipindi cha majaribio” ambapo kila mmoja anaweza kumwacha mwenzake wakati anapotaka. Badala yake, uhusiano hunawiri kila mmoja anapowajibika kwa mwenzake na kushirikiana kukabiliana na matatizo. b Ndoa huwafanya watu wawajibike zaidi.—Mathayo 19:6.

 Wenzi wa ndoa wanawezaje kuwa na ndoa imara?

 Hakuna ndoa kamilifu. Hata hivyo, wenzi wa ndoa wanaweza kuwa na ndoa zenye mafanikio kwa kutumia mashauri ya Biblia. Ifuatayo ni baadhi ya mifano: