Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Siko Tena Mutumwa wa Jeuri”

“Siko Tena Mutumwa wa Jeuri”
  • Alizaliwa Mwaka wa: 1956

  • Inchi: Kanada

  • Alikuwa: Mwenye kuvunjika moyo, mwenye kuwa na mwenendo muchafu, na mwenye kupenda jeuri

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

 Nilizaliwa katika muji wa Calgary mu Alberta, Kanada. Wakati nilikuwa mutoto mudogo, wazazi wangu walivunja ndoa, kisha miye na mama yangu tukahamia kwa wazazi wa mama, wenye walitupenda sana. Ile wakati nilikuwa mutoto mwenye furaha sana. Ningali nakumbuka ile miaka ya amani yenye nilipitisha wakati nilikuwa mutoto.

 Wakati nilikuwa na miaka saba, maisha yangu ilibadilika mubaya sana siku mama aliamua kuolewa tena na baba. Tulihamia St. Louis, Missouri, mu Inchi ya Amerika. Nilifikia kutambua kama baba yangu alikuwa mutu wa jeuri sana. Kwa mufano, siku ya kwanza wakati nilirudia ku nyumba na niko natoka ku masomo ya mupya, baba alitambua kama kuko watoto wenye walinipiga lakini sikufanya kitu. Alikasirika sana kisha akanipiga sana kuliko vile wale watoto walinipiga! Ile ikafanya nijifunze jambo fulani, na miye nilianza kupigana na watoto wenzangu wakati nilikuwa tu na miaka saba.

 Ile tabia ya baba yangu ilimukasirisha sana mama, na mara mingi walikuwa wanagombana. Nilianza kutumia dawa za kulewesha na kunywa pombe wakati nilikuwa na miaka 11. Hatua kwa hatua niliendelea kuwa mutu wa kugombana-gombana na mara mingi nilikuwa napigana na watu mu barabara. Kufikia wakati nilimaliza masomo ya segondere, nilibadilika kabisa na kuwa mutu wa jeuri sana.

 Wakati nilikuwa na miaka 18, nilijiandikisha mu Jeshi la askari wa bahari la Inchi ya Amerika. Nikapata mazoezi ya kujua namna ya kuua watu. Kisha miaka tano, niliacha kazi ya jeshi juu nisome masomo ya saikolojia nikiwa na kusudi ya kufanya kazi mu Shirika la Upelelezi la Inchi ya Amerika (FBI). Nilianza masomo ya université wakati nilikuwa mu Inchi ya Amerika, kisha nikaendelesha mu Kanada.

 Ku université, tumaini yote yenye nilikuwa nayo katika mwanadamu ilipotea, ile ikanivunja moyo sana. Niliona kama watu hawahangaikie wengine, mambo mu dunia haikukuwa na maana, na matatizo ya wanadamu haitaishaka. Niliona kabisa kama wanadamu hawawezi kufanya hii dunia ikuwe muzuri.

 Juu sikukuwa tena na kusudi mu maisha, basi nikaanza tu kutafuta feza, kunywa pombe, kutumia dawa za kulewesha, na kufanya uasherati. Maisha yangu ilikuwa tu raha na kubadilisha wanamuke saa manguo. Kwa kuwa nilipata mazoezi ya kiaskari, nilijiaminia sana na mara mingi nilikuwa napigana na watu. Nilijiamulia mwenyewe jambo la haki na lenye haliko la haki na nilikuwa nagombana na mutu yeyote mwenye niliona kama alikuwa anaonea wengine. Kwa kweli, nilikuwa sasa mutumwa wa jeuri kabisa.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

 Siku moja, miye na rafiki yangu tulikuwa ku sehemu ya chini ya nyumba yangu, tulikuwa tulishalewa bangi na tulikuwa tunafunga bangi ya marijuana ya kuuzisha kwa uficho. Kisha ule rafiki yangu akaniuliza kama naamini ikiwa Mungu iko. Nikamujibu hivi: “Kama Mungu njo mwenye anatesaka watu, sipendi kujua mambo yake!” Siku yenye ilifuata, wakati nilienda ku kazi ya mupya yenye nilipata, mufanyakazi mwenzangu mwenye alikuwa Shahidi wa Yehova aliniuliza hivi: “Unawaza kama hii mateso ya mu dunia inatoka kwa Mungu?” Ile ulizo ilinishangaza, juu jana nilitoka tu kusema maneno ya kufanana na ile; nikapenda kujua zaidi. Mu miezi sita yenye ilifuata tulikuwa na mazungumuzo ya mingi. Alinitolea majibu ya Biblia ku maulizo fulani ya nguvu yenye nilikuwa nayo kuhusu maisha.

 Muchumba wangu, mwenye nilikuwa naishi naye ile wakati, hakupenda nimuambie mambo yenye nilikuwa najifunza. Siku ya Yenga moja, nilimuambia kama nilialika Mashahidi wakuye kwetu ili kujifunza Biblia pamoja na siye. Siku yenye ilifuata, wakati nilitoka ku kazi, nilikuta amebeba kila kitu mu nyumba, akaenda na kuniacha. Nilitoka inje na nikaanza kulia. Pia nilisali kwa Mungu na kumuomba anisaidie. Ilikuwa njo mara yangu ya kwanza kusali kwa Mungu kwa kutumia jina lake la pekee, Yehova.​—Zaburi 83:18.

 Kisha siku mbili, nilianza kujifunza Biblia pamoja na ndugu mumoja na bibi yake. Wakati walienda niliendelea kusoma kitabu yenye tulikuwa tunajifunza, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, na nikamaliza kuisoma yote ile usiku. * Mambo yenye nilijifunza juu ya Yehova Mungu na Mwana wake, Yesu Kristo, ilinigusa sana. Niliona kama Yehova ni mwenye huruma na kama anaumia mu moyo wakati tunateseka. (Isaya 63:9) Jambo lenye lilinigusa moyo kabisa ni kuona vile Mungu ananipenda, na vile Mwana wake alitoa uzima wake kwa ajili yangu. (1 Yohana 4:10) Nilifikia kuona kama Yehova alinivumilia “kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.” (2 Petro 3:9) Niliona kama Yehova njo alinivuta kwake.​—Yohana 6:44.

 Mu ile juma, nilianza kuhuzuria mikutano ya kutaniko. Nilikuwa na nywele za murefu, nilikuwa nilishavala ma bijoux, na namna nilionekana kwa inje iliogopesha. Lakini Mashahidi walinitendea kama mutu wa jamaa yao mwenye walionaka zamani. Walitenda kama Wakristo wa kweli. Nilijisikia sawa vile narudia ku nyumba kwa tate (ao nkambo) yangu, lakini fasi ya muzuri zaidi.

 Polepole, mambo yenye nilikuwa najifunza mu Biblia ikaanza kubadilisha maisha yangu. Nilikata zile nywele za murefu, nikaachana na mambo ya uasherati, nikaacha kutumia dawa za kulewesha na nikaacha kulewa. (1 Wakorinto 6:9, 10; 11:14) Nilitaka kumufurahisha Yehova. Kwa hiyo, wakati nilijifunza kama hakubali jambo fulani lenye nilikuwa nafanya, sikutafuta kisingizio hata kidogo. Lakini, nilisikia roho inaniuma sana. Nilijiambia, ‘Siwezi kuendelea kufanya ile jambo.’ Na bila kuwa na mashaka, nilijaribu kubadilisha mawazo na matendo yangu. Kisha, nilianza kuona faida ya kufanya mambo yenye Yehova anapenda nifanye. Tarehe 29 Mwezi wa 7, 1989, miezi sita tu kisha kuanza kujifunza Biblia, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

FAIDA YENYE NIMEPATA:

 Biblia imenisaidia kubadilisha utu wangu. Zamani, mutu angenichokoza, ningepigana naye. Lakini sasa najikaza sana ‘kufanya amani na watu wote.’ (Waroma 12:18) Kama nimefanya mabadiliko, haiko kwa nguvu yangu, lakini namushukuru Yehova kwa sababu ya nguvu ya Neno lake na roho yake takatifu.​—Wagalatia 5:22, 23; Waebrania 4:12.

 Kuliko kuwa mutumwa wa dawa za kulewesha, jeuri, na tamaa za mubaya, sasa najaribu kumupendeza Yehova Mungu na kumutumikia kwa nguvu zangu zote. Ile inatia ndani kuwasaidia wengine wamujue. Miaka kidogo kisha kubatizwa, nilihamia fasi ingine kwenye kulikuwa lazima kubwa ya wahubiri. Kwa miaka mingi, nimepata furaha ya kufundisha watu wengi Biblia na kuona vile ilibadilisha maisha yao na kuifanya ikuwe muzuri sana. Tena, niko na furaha sana juu mama yangu amekuwa Shahidi wa Yehova. Kati ya mambo yenye ilimuvutia sana ni kuona namna mwenendo yangu ilibadilika.

 Mu mwaka wa 1999, nilimaliza masomo ya Biblia, yenye inaitwa sasa Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme, mu El Salvador. Ile masomo ilinifundisha mambo mingi yenye ilinisaidia nikuwe na bidii mu kazi ya kuhubiri, kazi ya kufundisha na ya kuchunga kutaniko. Kisha, mu ile mwaka, nilimuoa bibi yangu mupendwa, Eugenia. Sasa tunatumika pamoja tukiwa wahubiri wa wakati wote mu inchi ya Guatemala.

 Leo, kuliko kuwa mutu mwenye kuvunjika moyo niko na furaha sana mu maisha. Kutumia mafundisho ya Biblia kumenifanya nikuwe huru kwa kuachana na mwenendo muchafu na jeuri na kumefanya maisha yangu ikuwe na upendo wa kweli na amani ya mingi.

^ Leo, ili kujifunza Biblia na watu, kwa kawaida Mashahidi wa Yehova wanatumia kitabu Furahia Maisha Milele!