Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova ni Sekte?

Mashahidi wa Yehova ni Sekte?

 Hapana, Mashahidi wa Yehova haiko sekte. Tofauti na ile, tuko Wakristo na tunajikazaka kufuata mufano wa Yesu na mafundisho yake.

Sekte ni Nini?

 Watu wanaelewaka neno “sekte” mu njia mbalimbali. Kwa hiyo, tuone mambo mbili yenye watu wanasemaka juu ya maana ya neno sekte na juu ya nini ile mambo inaonyesha kama siye hatuko sekte.

  •   Watu fulani wanasema kama sekte ni dini ya sasa ao dini yenye haiko ya kawaida. Mashahidi wa Yehova hawakuanzisha dini ya sasa. Lakini, tunanamuabudu Mungu sawa vile Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa nafanya. Kusema kweli, mambo yenye walikuwa nafanya na kufundisha inaandikwa mu Biblia. (2 Timoteo 3:16, 17) Tunaamini kama ni Maandiko Matakatifu njo inapaswa kuamua ibada yenye inakubaliwa.

  •   Watu fulani wanasema kama sekte ni kikundi ya dini ya mubaya na yenye inaongozwa na mutu. Mashahidi wa Yehova hawaongozwe na mutu. Lakini tunaheshimia mambo yenye Yesu aliambiaka wanafunzi wake: “Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo.”​—Matayo 23:10.

 Njo maana Mashahidi wa Yehova haiko sekte, lakini ni dini yenye inatusaidiaka na yenye inasaidiaka pia wengine. Kwa mufano, kazi yetu ya kuhubiri ilishasaidia watu waachane na mazoea ya mubaya, sawa vile kutumia dawa za kulewesha na ulevi. Tena, tunafundishaka watu wengi kusoma na kuandika. Zaidi ya ile, tunasaidiaka watu wakati wanafikiwa na misiba. Tunajikaza kufanyia wengine mambo ya muzuri, sawa vile Yesu aliambiaka wanafunzi wake.​—Matayo 5:13-​16.