Ona video zinazopatikana

Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova Ni Nini?

Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova Ni Nini?

 Baraza Yenye Kuongoza ni kikundi ya Wakristo wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi na wao njo wameongoza kazi ya Mashahidi mu dunia yote. Kazi yao iko na sehemu mbili:

 Mu karne ya kwanza, “mitume na wazee katika Yerusalemu” njo walikuwa wanakamata maamuzi ya maana kwa ajili ya Wakristo wote. (Matendo 15:2) Baraza Yenye Kuongoza inafuata mufano wao. Mitume na wazee hawakukuwa viongozi wa kutaniko ya Kikristo. Vilevile, ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza hawako viongozi wetu. Wanasomaka Biblia juu wapate muongozo na wanajua kama Yehova Mungu amemuweka Yesu kuwa kichwa cha kutaniko.​—1 Wakorinto 11:3; Waefeso 5:23.

Nani njo wako mu Baraza Yenye Kuongoza?

 Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza ni Kenneth Cook, Jr., Gage Fleegle, Samuel Herd, Geoffrey Jackson, Stephen Lett, Gerrit Lösch, Mark Sanderson, David Splane na Jeffrey Winder. Wanatumikia kwenye makao yetu makubwa katika Warwick, New York, Amerika.

Baraza Yenye Kuongoza imepangwa namna gani?

 Baraza yenye kuongoza imeweka halmashauri sita juu ya kusaidia kusimamia sehemu mbalimbali za kazi yetu, na kila ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza anatumikia mu halmashauri moya ao zaidi.

  •   Halmashauri ya Waratibu: Inasimamia mambo ya sheria, inasaidia wakati kunatokea misiba, wakati Mashahidi wanateswa kwa sababu ya imani yao, na wakati kunatokea mambo ingine ya haraka yenye inahusu Mashahidi wa Yehova.

  •   Halmashauri ya Wafanyakazi: Inahangaikia mahitaji ya Wanabeteli.

  •   Halmashauri ya Uchapishaji: Inasimamia kazi ya kuchapisha na kusafirisha vichapo, kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Mikusanyiko, biro za kutafsiri, na biro za tawi.

  •   Halmashauri ya Utumishi: Inasimamia kazi yetu ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme.”​—Matayo 24:14.

  •   Halmashauri ya Ufundishaji: Inasimamia kazi ya kutayarisha mafundisho ya Biblia yenye inatolewa ku mikutano, ku masomo mbalimbali, na kupitia audio na video.

  •   Halmashauri ya Uandikaji: Inasimamia kazi ya kutayarisha mafundisho ya Biblia yenye inatolewa kupitia vichapo na kupitia site yetu ya Enternete, na inasimamia pia kazi ya kutafsiri.

 Zaidi ya kutumika na zile halmashauri, ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanafanyaka mukutano kila juma juu ya kuchunguza mahitaji ya tengenezo yetu. Mu ule mukutano, ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanazungumuziaka mambo yenye Biblia inasema na wanaachaka roho ya Mungu iwaongoze juu wakamate maamuzi ya muzuri.​—Matendo 15:25.

Wasaidizi wa Baraza Yenye Kuongoza ni nani?

 Ni Wakristo wenye kutumainika wenye wanatumikaka mu halmashauri za Baraza Yenye Kuongoza. (1 Wakorinto 4:2) Wanatumia uwezo wao na uzoefu wao juu ya kusaidia mu halmashauri yenye wako ndani, na wanakuwaka ku mukutano wa kila juma wa halmashauri yao. Hata kama haiko wao njo wanakamataka maamuzi, wanatoaka mapendekezo ya muzuri na wanasaidiaka kuhakikisha kama maamuzi yenye ilikamatwa inatimizwa. Pia, wanaendeleaka kuchunguza mambo kwa ukawaida juu ya kuona kama ile maamuzi inaleta matokeo ya muzuri ao hapana. Baraza Yenye Kuongoza inaweza kuwatuma watembelee ndugu na dada wa sehemu mbalimbali za dunia yote ao watoe hotuba ku matukio sawa vile ku mukutano wa kila mwaka ao wakati wanafunzi wa Gileadi wanapewa diplome.

LISTE YA WASAIDIZI

Halmashauri ya

Jina

Waratibu

  • Ekrann, John

  • Gillies, Paul

  • Snyder, Troy

Wafanyakazi

  • Grizzle, Gerald

  • LaFranca, Patrick

  • Molchan, Daniel

  • Scott, Mark

  • Walls, Ralph

Uchapishaji

  • Butler, Robert

  • Corkern, Harold

  • Glockentin, Gajus

  • Gordon, Donald

  • Luccioni, Robert

  • Reinmueller, Alex

  • Sinclair, David

Utumishi

  • Breaux, Gary

  • Dellinger, Joel

  • Georges, Betty

  • Griffin, Anthony

  • Hyatt, Seth

  • Jedele, Jody

  • Mavor, Christopher

  • Perla, Baltasar, Jr.

  • Rumph, Jacob

  • Smith, Jonathan

  • Turner, William, Jr.

  • Weaver, Leon, Jr.

Ufundishaji

  • Banks, Michael

  • Curzan, Ronald

  • Flodin, Kenneth

  • Malenfant, William

  • Noumair, Mark

  • Schafer, David

Uandikaji

  • Ahladis, Nicholas

  • Christensen, Per

  • Ciranko, Robert

  • Godburn, Kenneth

  • Mantz, James

  • Marais, Izak

  • Martin, Clive

  • Myers, Leonard

  • Smalley, Gene

  • van Selm, Hermanus