Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Wanaitwa Mashahidi wa Yehova?

Sababu Gani Wanaitwa Mashahidi wa Yehova?

 Yehova ndilo jina la pekee la Mungu linalopatikana katika Biblia. (Kutoka 6:3; Zaburi 83:18) Shahidi ni mutu anayetangaza kweli ambazo anaamini kabisa.

 Kwa hiyo, jina letu Mashahidi wa Yehova linaonyesha kwamba sisi ni kikundi cha Wakristo wanaotangaza ukweli juu ya Yehova, Muumbaji wa vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Tunawatolea wengine ushahidi kupitia namna yetu ya kuishi na kwa kuwahubiria mambo ambayo tumejifunza katika Biblia.—Isaya 43:10-12; 1 Petro 2:12