Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanavurugaka Familia za Watu ao Wanazisaidiaka Zikuwe Nguvu?

Mashahidi wa Yehova Wanavurugaka Familia za Watu ao Wanazisaidiaka Zikuwe Nguvu?

 Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kusaidia familia zao na familia za majirani wao zikuwe nguvu. Tunajua kama Mungu njo alianzishaka familia, na tunamuheshimia kabisa juu ya ile. (Mwanzo 2:21-​24; Waefeso 3:14, 15) Mu Biblia, muko mashauri yenye imesaidia watu mu dunia yote wakuwe na ndoa zenye ziko nguvu na zenye ziko na furaha.

Namna Gani Mashahidi wa Yehova Wanasaidiaka Familia Zikuwe Nguvu?

 Tunajikazaka kufuata mashauri ya Biblia juu inatusaidiaka tukuwe bwana wazuri, bibi wazuri, na wazazi wazuri. (Mezali 31:10-​31; Waefeso 5:22–​6:4; 1 Timoteo 5:8) Mashauri ya Biblia inasaidia hata familia zenye watu hawana imani moja zikuwe na furaha. (1 Petro 3:1, 2) Ona ushuhuda wa mwanaume moya mwenye bibi yake ni Shahidi na wa mwanamuke moya mwenye bwana yake ni Shahidi:

  •   “Miaka sita ya kwanza ya ndoa yetu ilikuwa tu ya fujo na kukosana. Lakini, wakati Ivete alikuwa Shahidi wa Yehova, alianza kunipenda na kunivumilia sana. Mabadiliko yenye alifanya iliokoa ndoa yetu.”​—Clauir, wa Brazili.

  •   “Wakati bwana yangu, Chansa, alianza kujifunza na Mashahidi wa Yehova, sikufurahi hata kidogo, juu niliwaza kama Mashahidi wa Yehova wanavurugaka familia za watu. Lakini, kusema kweli, nilifikia kuona kama Biblia imesaidia sana ndoa yetu.”​—Agness, wa Zambia.

 Wakati tunahubiriaka watu, tunawaonyeshaka namna mashauri ya Biblia inaweza kuwasaidia:

Kama watu wa familia hawako mu dini moya, ile inaletaka muvurugo mu familia?

 Kusema kweli, wakati fulani inakuwaka vile. Kwa mufano, mu 1998, ripoti yenye ilifanywa na kompanyi ya uchunguzi yenye kuitwa Sofres ilionyesha kama mu ndoa 1 kati ya ndoa 20 mulikuwa matatizo ya nguvu wakati bibi ao bwana aligeuka na kuwa Shahidi wa Yehova.

 Yesu alisemaka kama wakati fulani watu wenye kufuata mafundisho yake watachukiwa na watu wa familia zao. (Matayo 10:32-​36) Will Durant, mwenye kujifunza historia, anasema kama mu Utawala wa Roma, “Wakristo walikuwa wanashitakiwa kuwa walikuwa wanavunja familia za watu,” a na Mashahidi fulani wa Yehova wanashitakiwa vile leo. Lakini, ile inamaanisha kama Shahidi wa Yehova njo analetaka muvurugo mu familia?

Tribinali ya Ulaya ya Haki za Wanadamu

 Wakati fulani, Mashahidi wa Yehova walishitakiwa kama wanavurugaka familia za watu. Wakati Tribinali ya Ulaya ya Haki za Wanadamu iliamua ile mambo, ilisema kama ni watu wa familia wenye hawako Mashahidi njo wanaletaka hali ya kukosa kuelewana wakati wanakosa “kuheshimia haki ya mutu wa familia yao ya kujichagulia dini.” Ile tribinali iliongeza hivi: “Ile hali inatokeaka mu ndoa zote zenye bibi na bwana hawana imani moya, haifikiake Mashahidi wa Yehova tu.” b Hata wakati watu wa familia yao wanawatendea mubaya juu ya imani yao, Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kufuata hii shauri ya Biblia: “Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu. . . . Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani na watu wote.”​—Waroma 12:17, 18.

Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanaamini kama wanapaswa tu kuoana na Shahidi mwenzao?

 Mashahidi wa Yehova wanafuataka amri ya Biblia ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu,” ni kusema, kuoa ao kuolewa na mutu mwenye wako naye imani moya. (1 Wakorinto 7:39) Ile ni amri ya Biblia na inasaidiaka sana. Kwa mufano, mu 2010, habari moya yenye ilitolewa mu gazeti Journal of Marriage and Family ilisema kama “mara mingi bibi na bwana wenye wako mu dini moya, wenye wanaabudu pamoya, na wenye wako na imani moya” wanaelewanaka muzuri. c

 Hata vile, Mashahidi wa Yehova hawaambiake mutu aachane na bibi ao bwana yake mwenye haiko Shahidi wa Yehova. Biblia inasema hivi: “Kama ndugu yeyote iko na bibi mwenye haamini na bibi huyo anakubali kubakia pamoja naye, basi asimuache; na kama mwanamuke iko na bwana mwenye haamini na bwana huyo anakubali kubakia pamoja naye, basi asimuache bwana yake.” (1 Wakorinto 7:12, 13) Mashahidi wa Yehova wanafuataka ile amri ya Biblia.

a Ona kitabu Caesar and Christ, ukurasa wa 647.

b Ona uamuzi wenye ulitolewa mu kesi Mashahidi wa Yehova wa Moscow na Wengine wanasamba na Serikali ya Urusi, ukurasa wa 26-​27, fungu 111.

c Ona gazeti Journal of Marriage and Family, Buku ya 72, Namba 4, (Mwezi wa 8, 2010), ukurasa wa 963.