Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

alfa27/stock.adobe.com

KAMPANYE YA UKUMBUSHO

Yesu Atamaliza Jeuri

Yesu Atamaliza Jeuri

 Yesu anajua vile mutu anajisikiaka wakati wanamutendea mubaya na bila haki. Walimushitaki mambo ya uongo, walimupiga hata kama hawakukuwa na sheria ya kufanya vile, walimusambisha bila haki, walimuhukumu hata kama hakufanya kosa, na aliuawa kifo ya maumivu mingi. Hata kama hakufanyaka kosa, alikuwa tayari kutoa “uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” (Matayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni, akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu ataleta haki mu dunia yote na kumaliza kabisa jeuri.​—Isaya 42:3.

 Biblia inaonyesha namna dunia itakuwa wakati Yesu atafanya vile:

  •   “Waovu hawatakuwa tena; utaangalia mahali walikuwa, nao hawatakuwa pale. Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”​—Zb. 37:10, 11.

 Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani juu ya mambo yenye Yesu alishatufanyia na mambo yenye atatufanyia? Mu andiko ya Luka 22:19, Yesu aliambia wanafunzi wake wakumbuke kifo yake. Njo maana kila mwaka, ku tarehe yenye Yesu alikufa, Mashahidi wa Yehova wanakutanaka juu ya kukumbuka kifo yake. Tunakukaribisha na weye ukuye kufanya Ukumbusho wa kifo ya Yesu pamoya na siye Siku ya Yenga, tarehe 24, Mwezi wa 3, 2024.

Ona Fasi Kwenye Ukumbusho Utafanyika