Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Yasser Qudaih/Anadolu via Getty Images; kuume: RONALDO SCHEMIDT/AFP via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?

Vita Itaisha Wakati Gani?​—Biblia Inasema Nini?

 Le 13 ya Mwezi wa 4, 2024, Secrétaire Général wa Umoja wa Mataifa alisema hivi juu ya vita kati ya Iran na Israeli: “Hii njo wakati ya kupunguza vita na kusaidia batu baishi mu usalama. Tena hii njo wakati ya kujikaza kabisa kujizuia.”

 Ile vita ni moya tu kati ya mavita yenye iko napiganiwa mu dunia.

 “Leo, mu dunia, hesabu ya mavita inaongezeka sana kuliko wakati ingine tangu Vita ya Pili ya Ulimwengu, na inagusa batu miliare mbili. Ile ni sehemu moya juu ya ine (1/4) ya batu benye biko mu dunia.”​—United Nations Security Council, le 26 Mwezi wa 1, 2023.

 Maeneo kwenye kuko vita ya nguvu sana ni inchi na miji sawa vile Israeli, Gaza, Siria, Azerbaijan, Ukraine, Sudan, Ethiopie, Niger, Myanmar, na Haiti. a

 Vita itaisha wakati gani? Batawala ba hii dunia banaweza kuleta amani? Biblia inasema nini?

Vita ku dunia

 Mavita yenye iko nafanyika leo mu dunia inaonyesha kama hivi karibuni vita yote itaisha. Hii mavita iko natimiza mambo yenye Biblia ilisemaka juu ya kipindi yenye tuko naishi. Biblia inaita hii kipindi “umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—Matayo 24:3.

  •   “Mutasikia juu ya vita na habari za vita. . . . Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme.”​—Matayo 24:6, 7.

 Soma habari “Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?” juu ujue namna vita yenye tuko naona leo iko natimiza mambo yenye Biblia ilisemaka.

Vita yenye itamalizaka mavita yote

 Biblia inatabiri kama mavita itaisha. Namna gani? Haiko batu njo bataimaliza, itamalizika njo ku Armagedoni, “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufunuo 16:14, 16) Kisha ile vita, Mungu atatimiza ahadi yake ya kufanya batu baishi milele kwa amani.​—Zaburi 37:10, 11, 29.

 Juu ya kujua habari mingi kuhusu vita ya Mungu yenye itamalizaka mavita yote, soma habari “Armagedoni Ni Nini?

a ACLED Conflict Index, “Ranking violent conflict levels across the world,” January 2024